AbdiFitness
I USED TO MAKE PEOPLE LOOK AND FEEL BETTER
10/09/2024
Ni group Letu Jipya kabisa la WhatsApp la afya.
Tunatoa Elimu ya afya na Namna ya kuimarisha afya yako haswa afya ya mmeng’enyo wa chakula.
Na tunatoa miongozo kidogo kidogo kuhusu Afya na Lishe kiujumla.
Ni bure kabisa
Ukitaka kuungwa nicheki. 0755810575.
05/09/2024
Katika WhatsApp Group Letu tutaenda kujifunza kuhusu Afya ya Mfumo wa mmeng’enyo Next week.
Karibu Sana
0755810575.
02/09/2024
30/08/2024
Je? Unapata changamoto hizi katika Mfumo wako wa Mmeng'enyo?
1. Tumbo kujaa gesi
2. Tumbo kunguruma
3. Kukosa Choo na kupata Choo kwa Mara chache mnoo
4. Kupata choo kigumu Sana na kutoka kwa maumivu makali.
5. Kuvimbewa tumbo.
Usihofu tena Nimekuandalia Program Maalumu na itakusaidia kuondokana na Changamoto Tajwa Hapo Juu.
Bofya Neno " LEARN MORE " Kuifahamu Program Hiyo.
23/08/2024
Karibu Sana Hii ni free kwenye WhatsApp Group
Nicheki 0755810575. Nikuunge bure kabisa ujifunze kuhusu Afya yako.
17/06/2024
JINSI GANI UZITO MKUBWA HULETA CHANGAMOTO YA MAUNGIO (ARTHRITIS)
Uzito mkubwa unauhusiano mkubwa Sana na changamoto ya viungo. Kwa uelewa wa haraka viungo vya mifupa k**a magoti,vifundo vya miguu,kiuno na mgongo ndivyo vinahusika na kubeba uzito wa mwili. Kwa Hali hiyo uzito mkubwa husababisha viungo hivyo kulika na kutengeneza inflammation yaani kuwaka moto na maumivu makali.
Hii sio kwa magoti tu hata viungo vingine k**a vidole na viganja pia vinaweza kuathirika.
Kwahiyo uzito mkubwa ni hatari Sana kwa joints zako unapaswa kupunguza uzito ili kulinda afya yako ya maungio.
14/06/2024
12/06/2024
UGONJWA WA ARTHRITIS NI NINI?
Arthritis ni ugonjwa unaotokana na namna yo yote ya hitilafu katika maungio ya mifupa ya binadamu ambao husababisha maumivu na pengine kuvimba katika sehemu moja au zaidi ya maungio hayo. Neno arthritis halilengi ugonjwa mmoja bali jamii ya magonjwa ambayo kwa ujumla yapo zaidi ya 100. Tabia kuu ya magonjwa haya ni maumivu kwenye maungio ya mifupa ( joints) ambayo ni endelevu na ambayo hutokea eneo hilo moja. CHANZO_CHA_ARTHRITIS_NI_NINI?
Kusudi kuelewa chanzo cha ugonjwa huu, hebu kwanza tutazame muundo wa joint au sehemu mifupa miwili inapokutana. Fikiria goti ambapo mifupa miwili mmoja wa paja na mwingine wa mguu vinapokutana: Ligaments: Ndicho kitu kinachoshikilia mifupa hii miwili pamoja. Hii ni k**a utepe wa plastiki au mpira unaonyumbuka uliozunguka eneo hilo kwa nje, ukikunja goti inanyumbuka na ukinyoosha mguu inarudi. Cartilage: Huu ni utando unafunika eneo ambalo mifupa hugusana ili kuzuia mifupa hii isisuguane moja kwa moja. Utando huu ambao kwa kiswahili tunauita gegedu huyawezesha maungio hayo kufanya kazi kiulaini pasipo kusababisha maumivu. Capsule: Hiki ni kitu kinachofunika maungio haya kikizunguka pande zote. Ndani ya mfuko huu wa capsule kuna synovial fluid ambayo huzalishwa na synovial membrane. Synovial fluid ni ute wa kulainisha sehemu hiyo ya maungio na synovial membrane ni utando ulio kwenye kuta za ndani za capsule. Ugonjwa wa arthritis unasababishwa na hitilafu yoyote katika sehemu hizo za maungio ya mifupa. Inaweza kuwa cartilage inalika, upungufu wa synovial fluid, maambukizi ya vijidudu katika moja ya maeneo hayo au mchanganyiko wa matatizo.
Endelea kufuatilia kujifunza Zaidi.
06/05/2024
Uzito Mkubwa husababishaje mwanamke kushindwa kubeba ujauzito?
KWANZA.uzito mkubwa kwa mwanamke au hata mwanaume tafsiri halisi ni kwamba mwili una mafuta mengi sana na yanakuwa yametunzwa kwenye sehemu mbali mbali katika mwili ndo mana unakuta baadhi ya sehemu kuna nyama zembe na pia mtu unakuwa na kitambi.
Mafuta hata yanapozidi husababisha mishipa ya Damu kushindwa kupitisha Damu ipasavyo na hivyo kupelekea CHOLESTEROL na maradhi mengine k**a Pressure, kisukari n.k
Hivyo mwanaume au mwanamke mishipa yako ya damu inaposhindwa kupitisha Damu vyema Moja kwa moja inapelekea vyia vyako vya uzazi kwa mwanamke kushindwa kutungisha mimba kwa sababu ya mafuta mabaya yanakaa katika kizazi chako.
NJIA YA KIPEKEE. unapaswa kupunguza uzito k**a una uzito mkubwa na pia unatakiwa kusafisha mwili wako kuepukana na Changamoto zingine za kiafya.
29/04/2024
Tips zilizotumwa hapo juu ni muhimu sana kubadilisha hata lifestyle hasa katika ulaji. Tunakula sana sikuizi kwa wingi
1. Chips K**a zege, kavu n,k
2. Burgers 🍔
3. Fried chicken 🍗
4. Fried meat 🍖 mfano mishikaki pia.
5. Na hatusafishi miili yetu kwa maana ya kutoa mafuta mabaya
K**a ilivyozoeleka ukiendesha Gari lako kwa mda mrefu lazima uifanyie service ndipo uendeshe tena. Hivyo hivyo hata miili yetu hupungukiwa na vitamins, Nutrients na Minerals mbali mbali na pengine hatuvipati kwa kiwango sahihi katika vyakula vyetu vya kila siku.
Hivyo basi ni muhimu utumie Diet iliyojitosheleza kuongeza vitamins, minerals ambazo ni pungufu. Katika lishe yetu ya kila siku.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Dar Es Salaam
Dar Es Salaam