Afya Tips 100% Natural

Afya Tips 100% Natural

Share

Afya Yako Ndiyo Mtaji Wako.

Tunakusaidia kuweza kujua jinsi ya kuweza kuilinda afya yako kwa kutumia chakula na pia kukutatulia changamoto ya magonjwa kwa kutumia dawa zenye mchanganyiko wa vyakula asilia kwa 100%

Jisikie huru kuwasiliana nasi.

05/12/2024

🌹Habari..!
Hedhi kutoka muda mrefu inasababishwa na changamoto nyingi hizi ni baadhi, zifuatazo:-

1. Kuvurugika kwa homoni na mayai kupevuka.

Mabadiliko ya homoni na mayai kupevuka inaweza kupelekea hedhi kutoka muda mrefu.

Kwa mwanamke mwenye afya njema asiye na matatizo ya uzazi anaweza kuona mabadiliko haya hasa anapokaribia kukoma hedhi, au mwanzoni unapoanza kupata hedhi wakati wa kubalehe.
.lakini pia homoni zaweza kuvurugika kutokana na matatizo mbalimbali k**a changamoto za tezi ya thyroid na vimbe kwenye mayai.
.k**a homoni zako zimevurugika au k**a mayai hayatolewi kwenye mifuko ya mayai wakati wa mzunguko wako, ukuta wa mimba utakuwa mnene sana
. Na pale ukuta utakapobomoka na kutoka nje hehdi yako itakuwa ya muda mrefu sana na nzito.

2. Matumizi ya dawa.

Yanaweza kupelekea hedhi kutoka muda mrefu kutokana na dawa ulizotumia katika mwezi husika. Dawa hizi ni pamoja na:-

• dawa za maumvu
kuzuia mimba(contraceptives) na
dawa za kupunguza uvimbe mwilini
• Ujauzito
•Bleed ya muda mrefu inaweza kuwa kiashiria cha mimba kutunga nje yakizazi au mimba kuharibika.
... Unaweza pia kupata bleed ya muda mrefu endapo una tatizo la kondo la nyuma kwenye mimba yako.

K**a ulifanya kipimo cha mimba ukakuta kinasoma positive, na unapata bleed hakikisha unaenda hospitali haraka.

3. Uvimbe Kwenye kizazi(Uterine fibroids or polyps.

Uvimbe kwenye kizazi unaweza kupelekea hedhi kutoka muda mrefu na ikaambatana na mabonge ya damu.

Fibroids hutokea pale misuli ya kuta za kizazi zinapoanza kukua kupita kiasi.
..Kutanuka kwa kizazi (adenomyosis)
Adenomyosis ni tatizo lingine kwenye kizazi ambalo husababishwa na tishu kukua kupita kiasi.

Tatizo linaweza kusababisha kizazi kutanuka na hedhi kutoka muda mrefu zaidi.

4. Matatizo ya tezi ya thyroid(tezi ya shingoni)
K**a tezi ya thyroidi haifanyi kazi vizuri kuzalisha homoni zinazotakiwa kwa shughuli za mwili inaweza kupelekea hedhi kutoka muda mrefu sana.

Tatizo hili la tezi ya thyroid huitwa hypothyroidism.

5. Uzito Mkubwa na Kitambi.

Uzito mkubwa na kitambi husababisha hedhi nzito na kutoka kwa muda mrefu.

Hii ni kwasababu seli za mafuta huzalisha zaidi homoni ya estrogen. Estrogen ikizidi sana huvuruga hedhi yako.

5. Pelvic inflammatory disease(PID)
PID ni maambukizi ya bakteria kwenye njia ya uzazi.

Tatizo lisipotibiwa mapema hupelekea hehdi kuvurugika na hivo upate hedhi ya muda mrefu. PID pia husababisha maumivu chini ya kitovu, maumivu kwenye tendo la ndoa na kutokwa na uchafu ukeni wenye harufu kali au mbaya.

6.Saratani.

Hedhi kutoka muda mrefu inaweza kuwa ni kiashiria kwamba una saratani ya kizazi au saratani ya shingo ya kizazi.

Tafadhali naomba nisaidie KUSHARE ujumbe huu na mwingine.
_______________________

28/10/2024

*VIDONDA VYA TUMBO*

Vidonda vya tumbo (Peptic Ulcers) ni majeraha yanayojitokeza kwenye kuta za ndani za tumbo au sehemu ya mwanzo ya utumbo mdogo, kutokana na kudhoofika kwa utando unaozuia asidi za tumbo.
Hapa kuna maelezo ya Sababu, Dalili, na Madhara yake:

*SABABU*

Sababu za Vidonda vya Tumbo:

1. Maambukizi ya bakteria ya Helicobacter pylori: Bakteria huyu huishi katika kuta za tumbo na huweza kusababisha uvimbe na vidonda.

2. Matumizi ya muda mrefu ya dawa za kuondoa maumivu (NSAIDs), k**a vile aspirin, ibuprofen, na naproxen, zinaweza kuharibu utando wa tumbo.

3. Matumizi ya pombe kwa muda mrefu yanaweza kuharibu utando wa tumbo na kuongeza hatari ya vidonda.

4. Uvutaji sigara, huongeza uzalishaji wa asidi na kuathiri mchakato wa uponyaji wa vidonda.

5. Mkazo (stress) kupita kiasi unaweza kuchangia kuharakisha kutokea kwa vidonda ingawa si sababu ya moja kwa moja.

6. Chakula chenye viungo vikali: Inaweza kuchangia hali ya kuumia kwa tumbo, lakini si sababu kuu ya vidonda.

*DALILI*
Dalili za Vidonda vya Tumbo:

1. Maumivu ya kuchoma kwenye eneo la tumbo, hasa katikati ya kifua na kitovu.

2. Kichefuchefu na kutapika mara kwa mara.

3. Kupungua uzito bila sababu.

4. Kuvimba au kujisikia tumbo limejaa baada ya kula chakula kidogo.

5. Kuharisha au kupata choo cha rangi nyeusi (ishara ya damu katika mfumo wa mmeng'enyo).

6. Kutopata hamu ya kula kutokana na maumivu baada ya kula.

*MADHARA*

Madhara ya Vidonda vya Tumbo (Komplikesheni):

1. Kutokwa na damu ndani ya tumbo: Hii inaweza kusababisha upungufu mkubwa wa damu mwilini (anemia).

2. Kupasuka kwa tumbo: Vidonda vinaweza kuchimba hadi kwenye kuta za tumbo na kusababisha matundu, hali inayohitaji upasuaji wa dharura.

3. Kuziba kwa njia ya chakula: Vidonda vinaweza kusababisha uvimbe, ambao huzuia chakula kupita kwenye njia ya mmeng’enyo.

4. Saratani ya tumbo: Kwa baadhi ya watu, hasa wale walio na maambukizi ya muda mrefu ya H. pylori, hatari ya kupata saratani ya tumbo huongezeka.

*ILI KUPATA SULUHISHO NJOO INBOX*

28/10/2024

KUFINYIA KWA NDANI

Kufinyia kwa ndani ni ile hali ya kukaza misuli ya uke ndizi 🍆ikiwa ndani ya uke🍑.

Zoezi hili ni jepesi sana na wanawake wengi hawalijui.

NAMNA YA KUFINYIA KWA NDANI
💯🤯🍆
Unajibana kana kwamba unabana mkojo,na ukizoea kufanya hivyo mara kwa mara pia inasaidia uke kubana.

Muda gani sahihi wa kufinyia ndani
Inapendeza zaidi mtu kufinyia ndani mwanaume akikaribia kupizi
Au
Akiwa anaenda spidi sana na ufinyie kwa ndani wakati ndizi inataka kutoka wakati wa kupump kwa maana wakati imeileta juu kabla ya kuikandamiza tena.
🥳🤯

K**A MPENZI WAKO HAJUI KUIFINYIA KWA NDANI USISITE KUMUONESHA HII🍌

24/10/2024

FAIDA ZA MCHANGANYIKO HUU KIAFYA

🫰 Kitunguu saumu ni kiungo cha ajabu ambacho kina faida nyingi, lakini watu wengi hukiepuka sana kwa sababu ya ladha na harufu yake.

🫰 Mchanganyiko wa maziwa na kitunguu saumu unaweza kuwa na faida zenye kufurahisha, lakini kwa kweli ni wa kushangaza na una faida nyingi za kiafya. Unapaswa kujaribu kutumia uone matokeo yake kiafya.

🫰📝VIUNGO/ MCHANGANYIKO

Punje 2-3 za vitunguu
1 kikombe cha maziwa
¼ kijiko cha unga wa manjano
Kijiko cha pilipili nyeusi (manga)
Vijiko 2 vya asali

🫰Namna ya kutengeneza

Andaa sufururia lako, weka maziwa na vitunguu saumu. Chemsha . Wakati maziwa huanza kuchemsha, ongeza pilipili nyeusi na poda ya manjano. Mara baada ya mchanganyiko kisha pooza , chuja maziwa yenye mchanganyiko na kuongeza asali ndani yake, tumia maziwa haya wakati yakiwa moto uranishukuru yafanye sehemu ya mlo wako hata kwa familia

🫰 FAIDA🫰
*HUTIBU PUMU
Tumia glasi ya mchanganyiko huu kila usiku itasaidia kupambana na pumu

👉 KUTIBU KIKOHOZI
Mchanganyiko huu ni antibacterial kwa sababu kubwa ya uwepo wa vitunguu saumu hufanya kuwa dawa bora ya kikohozi. Kijiko kilichoongezwa kwa maziwa ya vitunguu hutoa matokeo bora.

👉INATIBU KIFUA KIKUU
Kitunguu saumu kina wingi wa madini ta sulfur mara nyingi nimeeleza hata week iliyopita ambapo sulphur ina uwezo wa kuua vijidudu vinavyosababisha ugonjwa wa kifua kikuu. NBmaziwa ya kuchemsha na vitunguu ni dawa nzuri ya kutibu kifua kikuu

👉 TIBU PNEUMONIA
Kunywa Aina hii ya maziwa yenye kitunguu mara tatu kwa siku kutibu pneumonia

👉KUPUNGUA KOLESTEROL (MAFUTA MWILINI)
Kunywa maziwa ya kitunguu saumu kila siku kwa wiki husaidia kupunguza kiwango cha kolesteroli mbaya na hivyo kuongeza kolesteroli nzuri mwilini (Hapa sijasema unene 😄😄)

👉 ATHALI ZA MOYO
Kunywa maziwa ya vitunguu huzuia uundaji wa vifundo vya mafuta katika mishipa ya damu kwenye moyo , hivyo kuzuia ugonjwa wa moyo.

👉 AFYA YA UZAZI
Kunywa glasi ya maziwa yenye vitunguu kila siku husaidia kuondokana na utasa kwa wanawake na wanaume kwa sababu ya kupunguza mafuta na kuongeza mzunguko wa damu katika via vya uzazi na husaidia kupunguza maambukizi

18/10/2024

Embu angalia hizi faida hapa za kula Mapera
🍂 Inaboresha kinga ya mwili :

Hii ni kutokana na kiwango kikubwa cha vitamin C katika Mapera, kiwango cha vitamin C katika pera ni karibu zaidi ya mara tatu ya kile kiwango cha vitaminc katika Chungwa
🍂 Husaidia pia kukukinga dhidi ya maradhi k**a vile Saratani,arthitis (Baridi ya Bisi), magonjwa ya moyo n.K
🍂 Huweka sawa shinikizo la damu ( BP )
Hii ni kutokana na kiwango kikubwa cha Potassium, kwahiyo huupa afya moyo wako pia
🍂 Husaidia kukuepusha na magonjwa k**a vile mawe kwenye figo,stroke na matatizo ya mifupa, haya yote ni kwa sababu ya shinikizo la damu kuwa sawa
🍂 Chanzo kizuri cha nyuzi nyuzi (Fiber)
Sasa hii inakusaidia kupata choo kirahisi, husaidia pia kuweka sawa kiwango cha sukari katika damu
🍂 Kuna kiwango kikubwa cha viondoa sumu katika Mapera
Kiwango kikubwa cha viondoa sumu husaidia mwili kujikinga na magonjwa k**a kisukari, saratani na magonjwa ya moyo
🍂 Majani ya mapera husaidia kumaliza au kuzuia mchafuko wa tumbo (Kuharisha)
Japo hamna ushahidi wa kutosha,ila wengi wanaotumia huwasaidia, hii ni kwasababu ya tabia za majani ya mapera kuwa na uwezo wa kuua bacteria na vijidudu vingine
🍂 Uwezo wa majani ya mapera kumaliza mcharuko,uvimbe na maumivu
Inasemekana ni kutokana na uwepo wa flavonoids kwa kiwango kikubwa, compound hiyo inafanya kazi k**a Antioxidant,kwahiyo husaidia katika kuboresha afya ya mwili na kuukarabati mwili dhidi ya uharibifu,kuumia au uvimbe uliotokea mahali baada ya mtu kuumia,madhara ya vijidudu n.K
🍂 Husaidia pia kuepusha mafuta kujihifadhi pembezoni mwa mishipa ya damu ( atherosclerosis )
NB : Ukila pera moja ni sawa na mtu aliyekula machungwa matatu ( Tukilinganisha viwango vya vitamin C )

17/10/2024

*⚠️⚠️⚠️MUHIMU SANA KILA MWANAMKE HAKIKISHA UNASOMA MAKALA HII⚠️⚠️⚠️*

*KUNA TOFAUTI KATI YA U.T.I & P.I.D USICHANGANYE MAMBO*👇👇👇

*U.T.I*

U.T.I ni maambukizi kwa njia ya mkojo ambayo huathiri mfumo wa mkojo na mfumo wa uzazi ( Kwa mwanaume & mwanamke), wadudu huathiri sana kibofu na Urethra

*HIZI NDIO DALILI ZA U.T.I*

📌Kujihisi mchovu na kutokujisikia vizuri

📌kukojoa kwa shida na kujilazimisha

📌Maumivu wakati wa kukojoa

📌Kukojoa kiasi kidogo na mara kwa mara

📌Mkojo kutoa harufu kali

📌Mkojo muwa na rangi tofauti-tofauti zisizo za kawaida, mfano wekundu kupita kiasi

📌Maumivu ya tumbo,au pande za mwili karibu na tumbo mpaka sehemu za misuli

📌Joto laweza kuongezeka

*P.I.D NI NINI?*

P.I.D ni maambukizi katika via vya uzazi vya mwanamke tu

*DALILI ZA P.I.D NI*

🖍️Maumivu ya tumbo hasa chini ya kitomvu mara kwa mara

🖍️Kupata Maumivu ya mgongo kiuno na nyonga

🖍️Uchafu sehemu za siri k**a maziwa ya mtindi,

🖍️Harufu mbaya Sehém za siri

🖍️Miwasho Sehém za siri

🖍️Maumivu wakati wa tendo la ndoa

🖍️Kutoka damu bila mpangilio wakati wa hedhi

🖍️Kutoka damu baada ya jimai

🖍️Uke kuwa mkavu kutokana na acid iliyipo

🖍️Kuwa na mchubuko pamoja na vipele

*Wengi wakienda kwenye vipimo huwa wanafichwa juu ya tatizo la P.I.D badala yake wanaambiwa kuwa wana U.T.I sugu.*

⛔️⛔️Chukua hatua usiendelee kukaa na tatizo kwasababu madhara yake ni makubwa mnoo

*MATIBABU YAPO*

16/10/2024

*MIMEA MINNE ITAKAYOSAIDIA KUBEBA UJAUZITO KWA HARAKA*

✍️ unga wa uwatu

✍️mkunde

✍️Majani ya mrehani

✍️ habat sawda / Alovera juice

MAANDALIZI
Andaa unga wa mrehani, mkunde na uwatu unachanganya kwa pamoja unga wa mimea hiyo kwenye alovera juice,

k**a utapata habit, utachanganya unga wa mimea hio yote,kisha utakuwa ukitumia kijiko kimoja kwenye chai yako.

Mara tatu kwa siku, Tumia mfululizo kwa muda wa siku 28.

NB; K**a utatumia chai, chai yako ni vyema iwe ya mdalasini, tangawizi, iliki na mchaichai, ni viungo bora sana kwenye afya ya uzazi kwa mwanamke.

16/10/2024

💫Epuka kufanya ngono hovyo hovyo na wanaume tofauti toauti pia zingatia ngono salama kwa mtu usiyemuamini

💫Jiwekee tabia ya kufanya vipimo mara kwa mara hasa vipimo vya mfumo wa uzazi walau kila baada ya miezi sita

💫Usifanye mapenzi mara baada ya kujifungua au mimba kutoka mpaka utakapo hakikisha shingo ya uzazi imefunga vyema, jipe kipindi cha siku 40 bila kufanya ngono baada ya kujifungua au mimba kuharibika

💫kuwahi kuonana na daktari mara tu unapoona dalili za ugonjwa nilizokutajia hapo juu

💫Jitahidi kufanya usafi sehemu yako ya siri na mwili mzima kiujumla pia kula lishe bora.

💫Punguza ulaji wa nafaka za kukobolewa na vya kutiwa mafuta mengi, tumia zaidi maziwa mtindi, kitunguu saumu, apple na vyakula ambavyo vitakusaidia kusafisha njia ya uzazi.

09/10/2024

Uvivu wako wa kula ni soko la watu wengine la kujipatia pesa kupitia wewe hapo baadaye

Ulafi wako pia ni soko la watu wengine la kujipatia pesa kwa baadaye

Unahitaji kula

Unahitaji kupangilia mlo wako... na si kula ili mradi tu umekula

Hakikisha kwamba unapokula chakula unaongeza kinga na virutubisho mwilini na sio kuongeza sumu ambazo zinaenda kupambana na kinga zako za mwili.

09/10/2024

*FAIDA YAMAZIWA MTINDI KWA MWANAMKE.*

👇MAZIWA MTINDI YANA SIRI KUBWA KWA
WANAWAKE NI WENGI HAWAYAPENDI ILA MTOTO
WA K**E JITAHIDI USIKOSE KUNYWA GLASS
MOJA YA MAZIWA HAYA KILA SIKU

➡HAYA HUSAIDIANA NA BAKTERIA WA UKENI
KATIKA KULINDA UKE KUZUIA ATHARI ZA FUNGUS
KWA KUNYWA NA KUPAKA UKENI.

➡PIA UKIYATUMIA HUSAIDIA KURUDISHA UMBO
LA UKE, HATA K**A IMETANUKA UTARUDI K**A
ZAMANI TUMIA KWA KUNYWA
HUONDOA HARUFU MBAYA ukeni NA UKITUMIA
HUIPA HARUFU NZURI YA KUVUTIA NA
KUNOGA KWELI HASA UNAPOKUWA NA MWENZA WAKO.

PIA HUFANYA UKE UWE MNATO WAKATI WA
TENDO.

JITAHIDI ASUBUHI UKIAMKA KUNYWA MAJI
YA UVUGUVUGU GLASS MBILI,KAA MASAA MAWILI
KUNYWA MTINDI PAKITI MOJA NDOGO AU GLASS
MOJA KILA SIKU NDANI YA MIEZI SITA HALAFU
LETE MLEJESHO HAPA PIA K**A ULIKUWA
MHANGA WA FUNGUS UTASHANGAA NATURALLY
ZAONDOKA.

07/10/2024

*MADHARA HATARISHI YA HORMONAL IMBALANCE KWA MWANAMKE*
Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone).

Ufanisi wa kichocheo/Hormone unapopungua ama kongezeka huathiri hormone zingine, tatizo hili tunaliita Hormonal Imbalance

*MADHARA YA* *HORMONAL* *IMBALANCE*
*MWILINI*.👇👇

💫Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa

💫 Kutokushika mimba (infertility)

💫 Hupelekea kuharibika kwa mimba kutokana na udhaifu wa kuta za uzazi.

💫 Uke kua mkavu (vaginal dryness)

💫 Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali

💫 Kutokupata usingizi vizuri

💫 Kuongezeka uzito

💫 Kupata choo kwa shida au kuharisha

💫 Kutokua sawa kwa mapigo ya moyo

*Nakazia sana swala la mvurugiko wa homoni, kwasababu napokea kesi nyingi za namna hii, wapendwa tujitahidi kubalance mfumo wa homoni*

07/10/2024

*VYAKULA RAFIKI KWA UKE*💥💥

Leo tunajikita katika vyakula ambavyo ni rafiki kwa uke.

💫 *Maziwa mtindi, mtindi fresh (mtindi usio wa kiwandani)*
ule mtindi wenye mafuta mengi, chachisha mtindi wewe mwenyewe, ni rahisi sana, kunywa glasi moja kila siku asubuhi au jioni.

💫 *Viazi vitamu vya njano*
viazi vya njano vina vitamini A na C na pia vina madini muhimu kwa ajili ya kuzalisha seli za mwili, homoni na kuimarisha kuta za uke. Pia hukuongezea nguvu na uchangamfu.

💫 *Kitunguu swaumu*
ni muuaji wa bacteria, angekua askari basi ni yule askari anayetembea na rungu bakteria huwawezi kuisha karibu na kitunguu swaumu. Kula fresh kabisa, nywea kwenye maji asubuhi sana kabla ya kula chochote, tumia punje 8 ndogo au kubwa 5.

💫 *Liven alkaline powder*
Liven kwa wanawake wenye uke mkavu inamsaada sana, tumia unga wa liven k**a unavyoelekezwa na mtaalamu mahali uliponunua, k**a unaweka liven kwenye chai basi usichemsha na maji, bali weka kwenye kikombe cha chai au Maji ya moto pekee. Sachets moja katika kila kikombe kimoja cha chai kinatosha.

💫 *Matunda k**a parachichi na apple*
Matunda haya hufanya kazi ya kurekebisha ukemkavu kwa kuongeza kiasi cha unyevunyevu ukeni. Kula avocado karibia kila siku na apple pia. Ulimwenguni kote wanawake hupenda apple. Tumia apple ile ya kienyeji ile ya Tanga, fika soko kuu ulizia apple za Tanga. Apple za South Africa na Brazili sio nzuri kwa kuwa zina madawa mengi sana na hvyo usababisha sumu kubaki mwilini na kupelekea madhara mengine K**a matatizo ya kwenye homoni kwahyo kuchangua apple kwa makini ni jambo muhimu sana.

💫 *Maji*
Maji pia ni muhimu nimekuwa nikiwafundisha watu namna ya kupunguza uzito na kuondoa unene kwa kunywa maji mengi k**a lita 3 kwa siku ukianza na galsi 1 asubuhi, moja saa4, moja saa7, moja saa10 na ingine saa12 au saa3 usiku (Jumla glass8). Lakini kuna upinzani mkubwa kutoka kwa wanawake hasa kwa kuogopa kwenda msalani mara kwa mara.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Address


Dar Es Salam
Dar Es Salaam