lavish herbs company

lavish herbs company

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from lavish herbs company, Health/Beauty, kariakoo SIKUKUU na agrey, Dar es Salaam.

16/06/2026

🍀Vagus nerves ni mishipa muhimu sana kwenye mfumo wa usagaji chakula , hio mishipa ipo seheme za shingo pande zote 2 kulia na kushoto
Kazi zake kuu ni kusimamia mfumo wa mishipa na usagaji wa chakula na upumzishaji ,
Pia husaidia umio kufunguka na kufunga wakati wa kumeza chakula ili kuzuia tindikali kupanda juu

🍀 Vagus nerve ni mojawapo ya neva kuu za mwili inayounganisha ubongo na viungo vya ndani hushuka kupitia nyuma ya sikio, mbele ya shingo na kuteremkia kwenye :
Umio ( esophagus)
Moyo
Mapafu
Tumbo
Utumbo wa chakula

🍀Mishipa ya vagus nerve ikiwa imepata athari k**a stress nk. inaweza kuzuia ufanisi wa tumbo (gastroparesis) na kusababisha chakula kukaa kwa muda mrefu bila kusagika kuongeza shinikizo, na kulazimisha asidi kurudi kwenye umio. Na kusababisha mishipa ya vugas nerve kuvimba , wasiwasi , mapigo ya moyo kupiga sana , sauti kukwaruza, kuzidi kiwango cha acid na hata kupelekea kuchelewa uponyaji wa acid reflux

🍀Namna ya kusaidia kujitibu kwa kupitia mishipa ya vugas nerver
🔆Jifanyie massage nyepesi usitumie nguvu sana na tumia mafuta yoyote ya maji
🔆Jikande pembeni mwa masikio nyuma ya shingo , mishipa ya bega na shingo. shuka kifuani , chini ya matiti na shuka tumboni kote
Hii jikande kila mara unapohisi acids imekubana sana inasaidia kuondosha changamoto k**a kizunguzungu, pumzi ya shida. Wasiwasi na hata acidi kupanda kooni

Njia 2. unaweza kuimba kwa sauti ya kubana mdomo na kusema hummmmmmmm yaani kitaalamu tunaita (humming songs) Hii inafanya kwa sauti hali umebana midomo 2 pamoja na inavuta pumzi mpaka ukiona umenyamaza mwenye ndio unafungua mdomo kuvuta pumzi kisha unaendelea tena njia hii inasaidia sana mishipa ya vagus Ku relax na kupunguza izo changamoto

Njia ya 3. Unaweza kusukitua maji kwa kwenye koo kwa kuguggili mpaka ukinyamaza meza maji na fanya tena k**a mara 3

Njia ya 4. Fanya zoezi la pumzi hili pia inatakiwa ufanye kabla ya kula na baada ya kula japo mara 10 inasaidia sana mishipa ku relax na kuwezesha chakula ku Seattle vizuri tumboni
Vuta pumzi kwa taratibu na kwa urefu unaoweza vutia kwa ndani na achilia kwa mdomoni

Njia ya 5. Kutumia vitamin B12 sambamba na vitamin d3

16/06/2026

🌟H pylori
👉 H pylori ni maambukizi ya bacteria huweza kupata mtu yoyote Yule mtoto au mtu mzima
watu wanaweza kumeza bakteria ya H. pylori kutoka kwa chakula kilichochafuliwa, maji, au vyombo vya kulia. Maambukizi ni ya kawaida katika maeneo yenye watu wengi na yale yasiyo na maji safi au mifumo bora ya maji taka. Watu pia wanaweza kupitisha bakteria kupitia mate yao (mate) na maji mengine ya mwili.

👉 H. pylori ni bakteria ambao huharibu safu ya kinga ya tumbo. Bila kutibiwa, maambukizi ya H.pylori yanaweza kusababisha matatizo.

👉 H. pylori ni bakteria ambayo hukua kwenye njia ya usagaji chakula na huelekea kushambulia utando wa tumbo.

👉 H pylori hushambulia utumbo na kufanya mashimo au vidonda ndani ya utumbo na kupeleka maumivu makali Sana na inachukua muda Sana kupata uponyoji wake
Bacteria Kawaida huzaliana kwa wingi ikiwa tumboni hakuna kiwango cha acids kinachostahiki cha kuweza kuchoma au kuuguza bacteria wabaya

👉 H pylori hupelekea kansa ya utumbo

👉 Dalili za h pylori
Brain fog
Kubeuwa Sana
Kuwa na alaji ya vyakula, mazingira , ngozi nk
Choo kigumu
Upungufu wa virutubisho na vitamin mwilini
Neurotransmitter deficiencies
Tumbo kuwaka moto
Maumivu ya tumbo hasa ukiwa na njaa
Kizunguzungu
Kupoteza hamu ya kula
Kupungua uzito
Kutapika damu au weusi
Kuharisha damu
Kukosa usingizi
Tumbo kujaa gesi
Upungufu wa damu
Mdomo kupoteza ladha
Vitu vya kusaidilia
Wacha vyakula vyenye acid , sukari mafuta na punguza wanga
Zingatia mbogamboga na matunda unayotumia

👉 Vinywaji vya kusaidia

Manjano kunywa kutwa mara 2

Green tea kunywa kutwa mara 2

Vidonge vya vitunguu swaumu

📌 Dawa za kutibu text DM
Zingatio
Hili tatizo linachumua muda kupona Kwa hio inahitajia muda wa kutumia dawa Ni endelevu

16/06/2026

Vidonda vya tumbo

📍Vidonda vya tumbo hutokea wakati asidi ya utumbo huharibu utando wa tumbo lako. Matibabu inaweza kutegemea sababu.

📌Sababu zinazopelekea
Bacteria ( h pylori )
Kutumia madawa ya infection
Aspirin
Baadhi ya maradhi
Kensa ya tumbo
Kula chakula Kwa haraka sana na Kwa kiasi chingi
Kutokuwa na nidhamu ya vyakula
Gesi kuzidi tumboni
Ukuta WA utumbo kuwa dhaifu
Dhiki za roho / akili kutokuwa na utulivu
Vyakula vigumu ambavo huchelewa kusagika tumboni
Vyakula vya kuwasha sana
Vyakula vikali
Vyakula vyenye viungo vingi
Kunywa chai au kahawa Hali ya kuwa tumbo kavu
Vyakula vya Moto Sana
Vinywaji vya gesi
Nyongo ikizidi tumboni

💥Dalili zake
Tumbo kuwaka moto
Maumivu ya Tumbo
Kiungulia juu ya kifua
Kujihisi njaa
Kutapika
Choo kigumu
Kutoka damu kwenye Choo kikubwa
Ikizidi Sana huleta Kuzimia
Kiu Kali

🍀Vitu vya kusaidia
Ndizi mbivu
Kitunguu swaumu
Juice ya kabichi Bichi kutwa mara 2
Kula vyakula vya jamii ya ambavo havijakobolewa
Kunywa green tea
Asali kijiko 1 kidogo kutwa mara 3
Mtindi
Tangawizi kunywa kutwa mara 1 au 2
Chemomile tea kutwa mara 2 bei 20,000
manjano kutwa mara 3 au kuchemsha manjano na maziwa na kunywa
Kutumia mbegu za ufuta , sun flower, mbegu za maboga , Flaxseed

❗Zingatio
Kuacha kutumia vyakula vya mafuta, pilipili nyingi , viungo vingi
Usikae na njaa Kwa mda mrefu
Kutumia Sana Vyakula vya nyuzinyuzi
Usilale baada ya Kula Tu
Kuacha kuvuta sigara
Tafuna chakula mpaka kisagike
Chakula Kula Kwa utulivu
Kukaa mkao mzuri wakati wa Kula
Kupunguza uzito mkubwa
Kula vyakula nyepesi usiku
Chakula cha usiku mwisho saa 12 jioni
Kutotumia vidonge vya kupunguza maumivu
Unapomaliza Kula usinywe kinywaji apo apo jipe muda kidogo

💊Dawa zipo dukani text DM kwa maelekezo ya tiba
https://www.instagram.com/p/DA5ouABtnfZ/?igsh=ZWZoMWh4dTdyaDkw

15/06/2026

Dalali za ugonjwa wa acid reflux
📌Sio lazima mgonjwa awe nazo zote

🍀Nazo ni
1. Ngozi kuwa kavu
2. Kukonda
3.kupoteza hamu ya kula
4.kufifia
5. Msongo wa mawazo
6. Maumivu ya mabega na shingo
7. Maumivu ya mgongo
8.mwili kuwasha
9. Kuvimbavimba baada ya miwasho
10.maumivu chini ya mbavu
11. Kukohoa baada ya chakula
12. Mwili kuwa wa moto
13. Ulimi kuwa mweupe
14. Usingizi wa shida
15. Masikio kutoa sauti
16. Kizunguzungu
17. Kwenda mbweu sana
18. Tumbo kukaza
19, pumzi kuwa nzito kutoka
20.maumivu ya juu ya tumbo
22. Moyo kupiga sana
23. Hofu, wasiwasi
24 kiungulia
25.kupata makohozi au marenda kooni
26. Kuhisi kitu kiganda kooni
27. Koo kuwa kavu
28. Sauti kukwaruza
29. Macho kupungua nuru ya kuona
30. Tumbo kunguruma
31. Choo kigumu
32. Kuhisi njaa sana
33.hasira sana
34. Maumivu ya mikono au mabega
35.vichomi, kwikwi, ganzi
35. Kuhisi kuwa na presha au ugonjwa wa moyo
36. Ulimi kuwa mchachu au kupoteza ladha
38. Kichwa kuuma au kukaza misuli ya kichwa
39.mwili kuishiwa nguvu
40. Kupoteza hamu ya s*x
41. Pua kuziba ( sinus )

,📌Maelezo ya tiba na njia za kusaidia kuponya text DM

15/06/2026

🍀TATIZO LA ACID REFLUX AU KIUNGULIA
Uponyaji huchukua muda unahitaji uvumilivu na kutumia vitu sahihi pia kutambua chanzo kilichopelekea ili kuweza kutibu ikiambatana na kuzingatia mlo sahihi ambao utajumuisha kwenye kipindi chote cha kupelekea kwenye uponyaji wako
Jipe muda wa kuponya na jitahidi kuondosha msongo wa mawazo kwani stress inachangia kuamsha acid na kupanda juu

🍀Pia jitahidi kuchunguza kila unapobanwa sana na kuliungilia k**a ni mlo uliokula muda huo au ni stress ndio sababu na kuanza kusawazisha tatizo kutokurudia

🍀Usinywe maji baada ya chakula chukua nusu saa ndio uweze kunywa maji kwa sababu maji hupoza acid na chakula kinahitaji acid ili kiyayuke , unapokunywa maji inaweza kupelekea chakula kurudi juu na kuhisi kimekaba koo au muwako mkali kwenye kifua au mgongo

🍀usiake na njaa mda mrefu na wala usiwe unashiba sana Kula kwa kiwango kidogo kidogo ata mara 5 mpaka 6 kwa siku ata kila baada ya masaa 3 mwisho kula saa 12 jioni ata k**a unalala saa 4 usiku hii inasaidia acid kutokusumbua nyakati za usiku

🍀Zingatia mlo unatumia ukigundua unaleta shida basi utoe kwenye list yako , hakikisha unapanga ratiba ya mlo wako wa wiki nzima

🌼Vyakula vinavokupasa kula ni k**a vifuatavyo

☕Vinywaji hakikisha haviwi moto sana viwe na joto la wastani Kutumia chai k**a chemomile tea, uji wa mtama , uji wa oats bila maziwa

🍲 Kutumia supu ya kuku, nyama au samaki hakikisha hutii viungo zaidi ya chumvi au kutia viungo vya majani ya mimea k**a zatari, oregano, coriander, curry leaves, bay leaves, swaum punje 1 usiitwage, mapilipi mekundu au njano , kijani isitumie, karoti

🥗Salad iwe ya kabichi, kitango na avocado

🍉Matunda k**a tikiti, kitango, ndizi mbivu, peas, apple jekundu

Chemsua wali unaweza kuweka na keroti, mahindi na njegere

Mikate ya slesi na supu

Ugali

Wali supu au wali mboga za mchemsho bila kitunguu au nyanya unaweza weka keroti au hoho

Maboga, mamungunye mchemsho au ya n**i

Pasta na nyama ya kusaga bila nyanya wala kitunguu unaweza weka keroti, hoho, mboga mchanganyiko. Nk

Butternut squash , chickpeas, lentils

Viazi mbatata au vizazi vitamu chemsha au vi bake

Chicken wraps bila nyanya

Post inaendelea party 2

15/06/2026

📍Kusumbuka na tatizo la acid reflux kwa mda mrefu bila kupona mara nyingi sana hutokana na sababu hizi kuu 👇👇

1. Tatizo Sugu kiungulia haimaanishi kuwa kuna kitu tatizo baya kwako , inamaanisha tumbo lako na mfumo wa stress zinahitaji kurudi kwenye usawa inapofanyika kiungulia hatimaye kutulia kawaida na kwa kasi.
🌼Kanuni ni kwamba
More stress more reflux
More reflux more stress
Hii ni kitanzi ambacho kin**idi kupeleka tatizo kuwa baya zaidi kwenye uponyaji

Stress hupelekea mfumo wa usagaji chakula kuzima kabisa ( shutdown mode )
Stress ya muda mrefu huathiri mishipa ya vagus ambao hudhibiti harakati za tumbo
Wakati mwili wako ni inakuvuta taratibu kwenye mfumo wa usagaji chakula

Motility ya tumbo hupungua wakati tumbo haliwezi kupeleka chakula chini kwa ufanisi chakula kinakaa kwa muda mrefu sana huchachusha gesi na hujenga shinikizo kusukuma asidi juu.
🔆Hata asidi ya kawaida inaweza kupanda juu wakati shinikizo la tumbo ni kubwa

2. Dawa za kutibu acids za hospitali tun**iita ( acid blocker) hizi akizitumia kwa muda mrefu zinaweza kufanya tumbo kuwa sensitive hizi dawa hutuliza dalili kwa muda lakini pia zinaweza kuharibu muundo asili wa asidi yenye afya ya kuweza kusaga chakula dawa unapoitumia unajiona uko sawa na utakapoiacha tatizo huja juu mara 2 yake kwa sababu utumbo imeshapoteza acids yake kutokana na kuzimwa na hii dawa wakati inapoza muwako wa acid tumboni na kupeleka tatizo kutokupana na utumiaji endelevu wa dawa usiokuwa na kikomo
🌼Endapo utataka kuacha kutumia hizi antacids lazima kuna utaratibu upitie

3.Kutokupata choo hupelekea tumbo kusukuma acid na kupanda juu

4. Bacteria zinazozaana tumboni k**a candida, sibo
h pyroly NK. Hizi huzalisha acids nyingi na kupelekea acid kupanda juu ya tumbo

5. Baadhi ya madawa hususani ya mda mrefu

6. Vilevi na kahawa

📌 Zingatia

Dumu kutumia muongo wa tiba na vyakula

Ukila chakula ukiona kinakwama kwa koo au inakuwa ngumu kushuka kwa haraka wacha kula vyakula vikavu kula vya majimaji na matunda

Fanya mazoezi ya kutembea saa moja baada ya kula huo inasaidia kuweka sawa mfumo wa usagaji chakula

Ukilala panga mito kichwa kiwe juu juu
Usilale baada ya chakula kabla y

15/06/2026
15/06/2026

Acid Reflux husababishwa wakati asidi ya tumbo inarudi kwenye koo kwa kutokana na kulegea kwa sphincter ya chini ya esophageal (LES)

🌼 Esophagusni mrija wa misuli, ambao husafirisha chakula na vimiminika kutoka kwenye koromeo (koo) hadi kwenye tumbo. Ni sehemu muhimu ya njia ya juu ya utumbo, kwa kutumia mikazo ya misuli inayojulikana k**a peristalsis kusukuma chakula kuelekea chini, bila kujali mvuto. Jukumu lake kubwa ni ni kusafirisha chakula na vimimina, na kuzuia acid kwenye tumbo isipande juu kwa kutumia ( sphincters )ya juu na ya chini ya umio.
Esophagusni ni msuli hukaa nyuma ya njia ya kuvutia pumzi (trachea) na mbele ya mgongo, ukitokea shingoni kupitia kifua na diaphragm hadi kwenye tumbo.
✨Na diaphragm ni ni misuli nyembamba lakini yenye nguvu ambayo inakaa chini ya mbavu , Imeshik**ana na uti wa mgongo, huunda kizuizi kati ya mapafu/moyo na viungo vya tumbo. Husaidia kupumua, kukohoa, kupiga chafya, kutapika, na kutoa uchafu.
Inapofanya kazi inavyopaswa, misuli inapaswa kufunguka wakati unakula, kuruhusu chakula kupita, na kufunga muda mfupi baadae
✨Misuli ya esophagusni na diaphragm ikiwa imelegea au haifungi vizuri au kufungua mara nyingi sana, hii inaruhusu asidi iliyo ndani ya tumbo lako kutorokea juu kwenye umio lako, na kupeleka.

Acid reflux kusababisha k**asi kwenye koo. Hutokana na asidi ya tumbo inakera utando wa koo, na kupelekea mwili kutoa kohozi nyingi k**a utaratibu wa ulinzi wa kinga. Na kupelekea sauti kukwaruza, kihisi kitu kuganda kooni , kukohoa sana

Kizunguzungu ukiwa unatembea

Umoto mgongoni au kifua

Maumivu ya kifua au mgongo

Moyo kupiga sana

Kuhusi acids inapanda mpaka kichwani

Maumivu ya kichwa au mishipa ya kichwa kukaza

Uvutaji wa pumzi kuhisi mzito

Hofu, wasiwasi, woga , hasira /depression

Tumbo kunguruma , kuhisi njaa sana , vichomi

ganzi, kiza cha macho

Acid kuziba njia ya kuvutia pumzi na kupeleka presha , mishipa ya moyo kupiga sana au kukaza , maumivu sehemu za moyo nk

Kuishiwa nguvu au kupata Maumivu ya miguu, mabega hadi kushuka kwenye mikono au upande mmoja wa mwili

Kupata muwako wa moto wa mgongo au kifua wakati wa kutembea au unaponyanyua kitu kizito

Inaendelea party 2

12/06/2026

🌼Dalili za tumbo lako zinaweza kuonekana kuwa sawa ... lakini sababu kuu sisiweze kubwa sawa

🌼 Acid reflux, GERD, H.pylori, vidonda vya tmbo, mara nyingi huweza kujichanga kwenye tiba zake na mbaya zaidi inaweza kukufanya kuendelea na matibabu kwa mda mrefu bila mafanikio
Kila gonjwa lina tiba zake zilizo sahihi vyema kutambua tatizo lako na kuweza kujitibia kwa usahihi

📌Hii ndio tofauti:
Acid reflux hutokea wakati asidi ya tumbo inapita nyuma kwenye umio (gullet). Hii hutokea kwa sababu sphincter ya chini ya esophageal - pete ya misuli inayofanya kazi k**a valve - hudhoofisha au kulegea isivyo kawaida. Hii Ni hali ya kawaida sana kutokea, lakini tatizo likidumu kwa mda mrefu yanaweza kusababisha hali mbaya zaidi inayoitwa Gastroesophageal Reflux Disease (GERD)

• GERD: Aina sugu na kali zaidi ya reflux ya asidi ambayo tatizo hujirudia mara kwa mara.
GERD (Ugonjwa wa Reflux wa Gastroesophageal) ni ugonjwa sugu wa usagaji chakula ambapo acid ya tumbo hutiririka kurudia hadi kwenye umio (bomba la chakula). Hupelekea kuumiza utando wa umio, na kusababisha dalili za kawaida k**a vile kiungulia kinachoendelea, maumivu ya kifua, na asidi kujaa.

• H.pylori: Maambukizi ya Helicobacter pylori ni maambukizi ya kawaida ya tumbo. Husababishwa na vijidudu viitwavyo Helicobacter pylori, bakteria anayejulikana pia k**a H. pylori na huweza kupelekea vidonda vya tumbo na Vidonda vilivyo wazi kwenye utando wa tumbo, au miwasho ya mda mrefu

@ vyote vina dalili kuu sawa k**a
Common symptoms may overlap:
✔️ Muwako wa kifuani ( kuingilia)
✔️ Tumbo kujaa gesi
✔️ Kichefuchefu na kizunguzungu
✔️ Maumivu juu ya tumbo
✔️ Kwenda mbweu mara kwa mara
✔️ Kuhisi kushiba
✔️ Mdomo mchache au mchungu
✔️ Kupata shida ya usagaji chakula baada ya kula

👇🏻Tabia za kiafya ambazo zinaweza kusaidia kudumisha afya ya utumbo:
✨ Kula vyakula vyepesi zaidi
✨ Epuka vyakula vyenye viungo/mafuta kupita kiasi
✨ Kunywa maji ya kutosha
✨ Epuka kulala chini mara baada ya kula
✨ Chagua vinywaji na vyakula vinavyofaa tumbo

📌 Kwa maelezo zaidi zipo post chini pitia zitakusaidia mfumo mzima wa tiba , vyakula na hata kutambua tatizo la

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Kariakoo SIKUKUU Na Agrey
Dar Es Salaam
160702