Afya bora
Nawasaidia wanawake wote kuondokana na changamoto za mfumo wa uzazi k**a U. T. I , Fungus sugu n.k
29/12/2023
*🥦Jiulize haya Kisha ujifunze*
📌Unaugonjwa wowote wa zinaa ambazo bado haujatibu
📌Unampenzi zaidi ya Moja
📌Unampenzi ambaye anawapenzi wengine
📌Huwa unapenda kuosha uke kwa sabuni au kupaka marashi
📌Umewahi kuugua PID
📌 Umewahi kutoa mimba kwa njia salama au isiyo salama na haukusafishwa
📌Unatumia njia za vipandikizi zaidi za Uzazi wa mpango
*Upo hatarini sana kupata Ugonjwa wa PID (pelvic inflammatory disease)*
Kwa sababu hasa hizo ndio sababu za wengi kuugua PID
*Nini nifanye kuepuka maambukizi haya*
🔖Tumia condom kuepuka maambukizi haya
Kwa asilimia 80 husambaa kwa njia ya zinaa isiyo salama
🔖Kuwa na mpenzi mmoja unayemuamini
Kitendo Cha kuwa na wapenzi wengi kinakupa uharari wake kupata maambukizi haya
*Nitajuaje k**a nina maambukizi ya PID*
Kwanza ni lazma ujue kwamba hakuna kipimo Cha PID
Zaidi maelezo na historia yako inaweza kukufanya ukapewa dawa za PID
Wengi hawapendi dalili ila kwa wanaonyesha dalili ni hizi....
📌kutokwa na Ute mchafu unaweza kuwa mweupe k**a maziwa au njano
Hapa unaweza kuambatana na harufu au usiwe na harufu kabisa
📌Maumivu ya tumbo la chini na kiuno
Maumivu maeneo ya kizazi, yaani kitovu kwa chini na mda mwingine kiuno
📌 Maumivu wakati tendo la ndoa
📌Kuchoma choma wakati wa kukojoa
📌Siku za hedhi kubadilika pia inaweza kuambatana nayo
*Nini kitatokea nisipotibu PID*
🔖Makovu kwenye mirija ya Fallopia
Makovu haya yanaweza pelekea kutoboka kwa mrija huu na hivyo wengi hukatwa
🔖 Maumivu sugu ya kiuno na tumbo la chini
Haya maumivu unaweza kupitia miaka mingi bila kupona ukichelewa kupata tiba
🔖Mimba kutungwa nje ya mfuko wa kizazi (ectopic pregnancy)
🔖Ugumba (infertility)
Hapa usipotibu unaweza kuwa tasa Moja kwa Moja na ukaikosa furaha ya mtoto
*P.s* Takwimu za shirika la Afya duniani *WHO* zinasema ....
"Kila kwenye kundi la wanawake 8 waliowahi kuugua *PID*, mmoja *(01)* ni mgumba"
Stamani ufikie hatua hiyoo
Kwa msaada na ushauri wa kiafya wasiliana nasi
*🌹 kwanza*
*0784707985*
01/12/2023
*🌹Je WAJUA SABABU KUU ZA KUHARIBIKA KWA MIMBA?*
Vyanzo vikubwa vinavyoweza kusababisha kuharibika kwa mimba👇👇
⛔Chromosome abnormalities
Mimba nyingi ambazo huharibika hadi
wiki ya ishirini husababishwa na tatizo hili,
Chromosomes huwa
zinabeba genes ambazo huyatambulisha
maumbile ya mwanadamu kwa nje, yaani
Jinsia yake, ngozi yake itakuaje, macho yake
na vitu vingine vingi,
Nisingependa tuingie
ndani sana lakini matatizo haya ya
chromosomes huchangia sana kuharibika
kwa mimba.
⛔Maambukizi katika mji wa uzazi wa
mwanamke {Infections},
Kuna kitu kinaitwa Pelvic Inflammatory
Diseases *{PID}*
Yaani kuvimba kwa kuta za mji wa mimba au kuvimba kwa mirija ya
uzazi nayo pia huchangia sana kuharibika
kwa mimba kwa mwanamke,
Lakini pia Candida
au
fangasi nazo pia huchangia sana kuharibika
kwa mimba.
⛔Chanzo kingine kikubwa ni utoaji wa
mimba za mara kwa mara
Wanawake au
wasichana
wenye tabia ya kutoa mimba moja au mbili au
tatu,
Basi nao pia hukutwa na tatizo hili la
kuharibika kwa mimba kwani uingizaji wa
vyuma ndani huweza kuharibu shingo ya
kizazi ya mwanamke,
Pia kukumbwa na
tatizo hili la miscarriage au kuharibika kwa
mimba.
⛔Chanzo kingine kikubwa ni magonjwa ya
zinaa {sexually transmitted diseases},
Magonjwa k**a gonorrhea, kaswende
mara nyingi sana huathili mfumo wa uzazi
wa mwanamke na hasa hasa kwenye mji
wa mimba na kuufanya kuwa legevu,
Na hata ujauzito unapotunga basi huweza
kutoka kwa haraka zaidi
Na hivyo kusababisha tatizo hili la kutoka kwa mimba { *Miscarriage* }.
⛔Chanzo kingine cha mimba kuharibika ni
tatizo la kisukari kwa mwanamke,
Hii nayo huchangia kwa kiasi kikubwa sana
kuharibika kwa mimba
Na mtu ambaye
hafanyi uangalizi wa karibu wa tatizo la
sukari basi husababisha glucose isitumike
k**a energy na hivyo kuleta madhara katika
kizazi hasa ujauzito.
⛔.Kitu kingine ni homoni imbalance)
kwa mfano hormone ya
progesterone mara nyingi hufanya ile kazi
ya kutunza mimba iendelee kukuwa,
K**a haitazalishwa kwa kiwango au itazidi basi uwezekano wa mimba kuharibika
*0784707985*
*Dr. Maximilian*
28/11/2023
*AFYA YA UKE*
*NAMNA YA KUTUNZA UKE*
uke huwa na kawaida ya kujisafisha wenyewe wewe unachotakiwa kufanya ni kujisafisha kwa maji mengi vugu vugu au baridi na maji safi na salama pia kabla ya kujisafisha hakikisha unaosha mikono yako vizuri na hii ni kila baada ya kujisaidia bila kusahau kujikausha vzr kwa tissue au vitambaa maalumu.
Mambo ya kuepuka
❣️Kujiingiza vidole
❣️Kutumia mate k**a kilainishi
❣️Kutumia maji ya moto sana
❣️Kuweka vyakula ukeni k**a majani ya mbaazi , maziwa etc
❣️kula sana vyakula vya sukari
❣️kuvaa nguo za kubana masaa 24 na kila siku
❣️kuweka udi
❣️Usitumie antibiotics mara kwa mara
❣️Acha kabisa kutafuna mchele
❣️Usioshe na sabuni zenye manukato
Hayo ni machache na mambo ya kuzingatia ili uwe na uke wenye afya
🪷Kunywa sana maji na juice za matunda mbalimbali k**a crabberry(sijui ndio huita matunda nyanya☺️) , chai ya tangawizi , juice ya tangawizi , kitunguu swaumu na maji, maji ya madafu.
🪷Jitahidi kushave na kufanya scrub maeneo karibia na uke na kupaka mafuta vzr k**a ya n**i
🪷Kila utakapomalizia kushiriki tendo jitahidi kuoga vzr tumia muda kuoga vzr
🪷vaa chupi za cotton zisizobana sana
🪷Anika chupi zako juani na kumbuka kuzipiga pasi pale inapobidi
🪷Lala bila chupi ama nguo za kubana
🪷Kumbuka kujisafisha kuanzia mbele kurudi nyuma
🪷Kila ukimaliza period jitahdi kufanya sitbath na ukiwa period jitahidi iwe siri yako sio ya kujitangaza 😀
21/11/2023
```ZINGATIA HAYA;
✅Usafi wa Uke kwa maji masafi ya kawaida.
✅Epuka povu la sabuni kuingia ndani ya uke.
✅Anza mbele kurudi nyuma wakati wakujisafisha mara baada ya kumaliza Haja kubwa/ndogo.
✅Unapohitaji kujikausha Uke wako tumia kitambaa safi na laini kabisa kuzuia michubuko.
✅Usitumie vitu vyenye kemikali/Tindikali au perfumes (manukato) ukeni. Mfano:- whipes
✅Unaweza kutumia Natural Cleanser, Cleanser/kisafisho maalumu (ASILIA kabisa) kwa Usafi salama na kinga ya Uke.
NB; Bacteria wanaoshambulia Kizazi hupitia UKENI TU,siyo puani, sikioni wala mdomoni, hivyo kujali mazingira ya Uke wako ni moja ya HATUA kubwa ya kuwa salama.
Karibu TUKUSAIDIE (USHAURI & TIBA) call me ☎️0784707985🙏🏽🙏🏽🙏🏽```
*KILA MWANAMKE ANAWEZA KUSOMA HII KWA FAIDA YAKE*
*MWANAMKE JALI AFYA YAKO*
__________
Hapa nimekuandikia Mambo Rahisi Ambayo NI Muhimu uyafahamu Kwa ajili ya Kuongeza usalama katika via vyako vya uzazi.
*HATUA BORA ZA KUSAFISHA UKE*
_________________
Kuwa na usafi mzuri wa uke ni muhimu kwa afya ya wanawake. Hapa kuna hatua za kuosha uke kwa njia nzuri:
*1. Osha mikono yako kabla ya kushika sehemu za siri.*
Hakikisha unaosha mikono yako kwa sabuni na maji safi kabla ya kugusa uke wako ili kuzuia maambukizi.
*2. Tumia maji safi na ya joto la Wastani.*
Epuka kutumia maji moto au baridi sana, kwani inaweza kusababisha uke kuwa mkak**avu na hivyo kuchubuka Kwa urahisi.
*3. Tumia sabuni laini na Yenye pH inayofaa (plain soap) kuoshea sehemu ya juu ya uke.*
Epuka kutumia sabuni ngumu au yenye kemikali nyingi (Mfano medicated soap), kwani inaweza kusababisha usumbufu na kuvuruga usawa wa bakteria wa uke (Ambao husaidua kuzuia Maambukizi ya bacteria wabaya). Chagua sabuni inayofaa kwa matumizi ya uke ambayo haina harufu kali au kemikali zenye nguvu.
*4. Usioshe ndani ya uke mara Kwa mara .*
Epuka kuingiza maji ndani ya uke, mara Kwa mara kwani inaweza kusababisha usumbufu na kuvuruga usawa wa bakteria wa uke. Kwa kawaida uke Huwa Una namna yake ya Asili ya kujisafisha, Kwa Hiyo Awamu chache Tu zinatosha.
*5. Futa na kukausha uke vizuri.*
Baada ya kuosha, tumia taulo safi na laini kusafisha uke vizuri na kuukausha. Hakikisha unafuta kutoka mbele kwenda nyuma ili kuepuka kupeleka bakteria kutoka njia ya haja kubwa kwenda ukeni, Maana usipofanya hivyo utapata U.T.I Za mara Kwa mara.
*6. Epuka kutumia dawa za kunukia uke na douching.*
Dawa hizi zinaweza kusababisha usumbufu na kuvuruga usawa wa bakteria wa uke na Uwiano Wa pH ya ukeni. Uke una mfumo wa kujisafisha asili, hivyo hakuna haja ya kutumia bidhaa hizo.
*7. Vaa nguo za ndani safi- za Pamba.*
Badilisha nguo za ndani kila siku na chagua nguo za pamba ambazo zinaweza kupitisha hewa vizuri na kufyonzwa unyevu ili kuzuia Maambukizi ya Fangasi na kusaidia kudumisha usawa wa bakteria wa uke.
Ni muhimu kukumbuka kuwa uke una mfumo wa kujisafisha asili, Ikiwa una wasiwasi wowote juu ya afya yako.
Kutokwa na uchafu wenye Harufu ukeni una dalili za wasiwasi, ni vizuri kuongea na daktari wako.
Kwa Matibabu na Ushauri wasiliana nasi- Tutakuhudumia Kwa Ubora zaidi.
*Dr. Maximilian Masalu*
**
*0784707985*
Siku zote afya ya uzazi ndio unatakiwa uipe kipaumbele zaidi, kwani ni ya Muhimu Sana.
Nawasaidia wanawake wote kutatua changamoto zao za Uzazi kwa kutumia virutubisho lishe, je ungependa nikusaidie na wewe?
Niambie sasa hivi, DM me .
07/11/2023
*🌷Kwanini Ndoa Iwe Chungu Kisa Tatizo la Ugumba*
Soma hii mpka mwisho👇
Maana ya Ugumba:- Ni kushindwa Kupata ujauzito Ndan ya mwaka mmoja ukiwa unafanya tendo la ndoa bila kutumia uzazi wa mpango Wala Condoms"
*Aina za Ugumba* :-
Kuna Aina mbili za Ugumba nazo Ni:-
🌑 1: Huu Ni Ugumba ambao wenzi wote wawili wanakuwa wapo Kwenye mahusiano na wanafanya tendo la ndoa kwa MDA wa mwaka mmoja na bila kupata mtoto ikiwa hawatumii uzazi wa mpango Wala Condoms.( *Primary infertility* )
🌑 2: Huu Ni Ugumba ambao wenzi wote wawili wanakuwa walishawahi Kupata ujauzito Mara moja au zaidi na kipindi wakiwa wanahitaji tena wanafanya tendo la ndoa na wanakosa kupata ( *secondary infertility* )
*Sababu kuu za Ugumba kwa mwanamke*
💎Uvimbe kwenye kizazi,(Fibroids)
💎 Hormanal imbalance,
💎 Uvimbe kwenye mfuko wa mayai (ovarian cyst)
💎Magonjwa ya mfumo wa uzazi. mfano' wake Ni ( *PID)*
💎kuwa na Uzito kupita kiasi,
💎 Kuwa na mawazo(Stress)
💎Tabia ya Ulaji hafifu wa Chakula au kula Sanaa,
💎 Kunywa Pombe Sanaa,
💎 Matumiz ya Dawa za UZAZI wa mpango,
💎Mirija ya uzazi kuziba
💎Kuwa na majeraha Kwenye Mirija ya uzazi.
💎 Uvutaji wa sigaraa
*Utawezaje kujua kuwa wewe unaweza kubeba ujauzito,:-👇👇*
⏺️ Kupata hamu ya tendo la ndoa,
⏺️Kupata Ute Ute wa uzazi,
⏺️ Mzunguko wa hedhi yako kwenda vzurii,
⏺️ Joto la mwili kuongezeka,
⏺️Maziwa Kuvimba na kuuma kwa Hali ya kawaida,
*Unawezake kujua kuwa wewe HUWEZI kubeba ujauzito;-👇👇*
⏹️Kupata Maumivu makali Ukiwa kwenye hedhi yako, ukikalibia au unapo maliza hedhi,
⏹️ kutokwa na uchafu ukeni, unaweza kuwa na harufu au hauna,
⏹️ Kukosa Ute Ute wa uzazi,
⏹️ Uke kuwa mkavu,
⏹️ Kukosa hedhi kabisa au kwenda hedhi Mara mbili kwa mwezi.
⏹️ Kukosa hamu ya tendo la ndoa,
⏹️ Kuwa na uzito Mkubwa kupita kiasi,
⏹️kupata maumivu makali wakati wa tendo la ndoa,
⏹️ Kuwashwa Mara nyingi Au kutokwa na vipele ukeni,
*Utajuaje kuwa mume wako Hawezi kutungisha Ujauzito👇👇*
⏏️ Kutoa manii chache
⏏️Kupata Maumivu au Kuvimba kwenye corodani,
⏏️ Kushindwa kusimamisha uume wake vizurii,
⏏️ Kushindwa Kutoa manii kabisa,
⏏️ Kuota Maziwa
⏏️Korodani zake kuwa size ndogo,
⏏️ mwanAume Kushindwa kunusa vizurii kwa pua zake,
⏏️Kukosa hisia za Kufanya tendo la ndoa,
*Namna gani ya kujikinga na Ugumba 👇👇*
🕳️ Tibu na jikinge na magonjwa ya uzazi, mfano, Fungus wa ukeni, Gonnoreah, kaswende, n.k(PID)
🕳️Tibu tatizo la hormonal imbalance,
🕳️ Epuka kutumia UZAZI wa mpango,
🕳️ Punguza uzito,
🕳️usinywe Pombe
🕳️ Punguza mawazo
🕳️ Usivute sigara,
🕳️ Usitumie vinywaji vyenye caffeine,
🕳️Tibu tatizo la Uvimbe kwenye uzazi K**a unalo,
*Mwisho*
Nakushauri wewe Ulie hangaika Sana kwa MDA mrefu juu ya kuto pata Ujauzito,
Unatafta mtoto kwa Miaka mingi na umetumia dawa bado umeambulia patupu,
Nina Suluhisho lako Ambalo litarudisha Tabasamu juu ya maisha yako Sasa
Kwa mawasiliano zaidi
*Maximilian Masalu*
*0784707985*
🌹
31/10/2023
*🌹Utajuaje mzunguko wako wa hedhi haupo kawaida*
Awali ya yote ni lazma kuelewa kwamba Kila mwanamke anapitia kipindi Cha kupata hedhi
Na Kila mtu anaweza kuwa na mzunguko wake licha ya wachache inayoweza kufanana
*Hedhi ni Nini*
Ni Moja ya mabadiliko yanayotokea wakati wa kubalehe au kuvunja ungo kwa mwanamke yoyote
Ambapo inaweza kutokea kuanzia miaka 8 hadi 16 na hedhi hukoma kuanzia miaka 50+ japo kwa wengine huwahi zaidi
Hedhi ni Moja ya dalili ya mtu kupata ujauzito hivyo mtu asiyepata hedhi hawezi kupata ujauzito
Kutokea kwa hedhi ni mchakato mrefu unaohusisha kazi za tezi k**a pituitary, haypotharumus na o***y
Ambazo huzalisha homoni zinazoweza kuwezesha ogani za uzazi kufanya kazi kwa ufasaha
*🕸️Utajuaje kuwa mzunguko wako wa hedhi haupo kawaida...*
Hedhi kuwa tofauti na kawaida inaweza kuwa kiashiri Cha matatizo kwenye mfumo wa uzazi,
Dalili hizi zinaweza kukuelekeza kuwa inashida....
*01* . kuwa na mzunguko wa hedhi wenye siku zaidi ya 35 au chini ya siku 21
Kawaida mzunguko mrefu zaidi unasiku 35, na mfupi zaidi ni 21
Hapa ni lazma ujue jinsi ya kuhesabu siku
*02* Kupata damu ya hedhi zaidi ya siku *07* au chini ya siku *03*
Siku za bleed kawaida ni kuanzia siku 03 hadi siku 07 ni Kawaida nje na hapo ni shida
*03* kupata hedhi mara mbili au zaidi ndani ya mzunguko wako (mwezini)
*04* kupata damu nzito k**a yenye mabonge mabobonge
*05* kuruka miezi mitatu bila kupata hedhi
*06* Kupata hedhi yenye maumivu makali na homa
K**a unapata maumivu kiasi kwamba huwezi kuendelea na majukumu yako ya Kila siku basi ujue unashida
*07* kubleed/ kutokwa na damu nyingi mfano kubadili Pedi kwa siku zaidi ya mara 03
Unapoona dalili k**a hizi chukua hatua za mapema kufanya uchunguzi na vipimo kuhusu Afya yako
Kwa ushauri zaidi
Wasiliana nasi kupitia.
*0784707985*
🍃MAMBO 5 YA KUEPUKA ILI UWE NA AFYA BORA YA UZAZI
1. Zingatia usafi wa nguo za ndani na mwili kwa ujumla
*
2. Epuka matumizi ya vitu vinavyovuruga mfumo wako wa hedhi.
✓ Usitumie P2, usutumie sindano za majira, vijiti, wala vidonge
3. Epuka kushiriki tendo la ndoa na wanaume wengi, tena bila kinga. Ukiweza kaa na mwanaume mmoja tu
Na uwe mwaminifu.
4. Usifanye arbotion. Ikitokea umeshafanya mara moja, usifanye mara ya pili, ikitokea umeshafanya mara ya pili, usifanye mara ya tatu.
✓ Unahatarisha kizazi chako, kuna uwezekano wa kuja kukosa mtoto kwa badae.
5. *Usikae na tatizo lolote la uzazi kwa muda mrefu.
K**a una tatizo lolote, using'ang'anie kuendelea kutumia dawa za aantibiotics wakati hazikusaidii...
Wasiliana nami akupe msaada usiendelee kuteseka tena.
_Jenga afya bora, uwe na maisha marefu yenye furaha_
12/06/2023
➡️ *U.T.I Ni nini?*
➡️ *Inasababishwa na nini?*
➡️ *Jinsi Gani Unaweza Kujikinga na U.T.I*
➡️ *Na Kupata Tiba Sahihi Kwa Waathirika wa U.T.I Sugu*
*U.T.I Ni kifupisho Cha Urinary Tract infection:* ambayo Kwa lugha yetu ni maambukizi Kwa njia ya mkojo kwahio U.T.I ni ugonjwa unaosambazwa Kwa mkojo
*Mfumo wa mkojo huundwa na figo*
1. Njia ya mkojo inayotoka kwenye figo hadi kwenye kibofu(yureta),
2. kibofu cha mkojo na njia ya mkojo inayotoka kwenye kibofu hadi nje ya mwili(yurethra).
Tatizo hili huwapata Jinsia Zote Ila sana sana wanawake kutokana na mfumo wao wa kimaumbile
*Kwasababu kuu mbili*
1. Njia ya haja ndogo Iko jirani zaidi na njia ya haja kubwa ambapo vijududu vingi vinavyosababisha U.T.I Ndo vinaposhi
2. Mrija wa mkjo wa mwanamke ni mfupi ukilinganisha na wa mwanaume Hivyo kufanya iwe rahisi Kwa maambukizi kufika kwenye kibofu Cha mwanamke kuliko Cha mwanaume
*Visababishi vya U.T.I*
Huwa ni bacteria wanaopatikana katika utumbo mpana na ndo maana huwa wanaopatikana pia kwenye njia ya haja kubwa mfano wa bacteria ni Escherichia coli na wengineo.
Pia Fungus na visababishi vingine japo ni mara chache kupatikana Kwa kesi hii.
*Lakini hizi Hapa njia ambazo mwanamke anaweza kupata U.T.I.*
1. Kuchezea ama kuchezewa na mikono michafu maeneo ya uke kunaweza kusababisha maambukizi.
2. Njia mbaya ya kujisafisha baada ya haja kubwa au ndogo inaweza kuhamisha bacteria walio ktk njia ya haja kubwa na kuingia njia ya mkojo.
3. Matumizi ya pedi za k**e zenye kemikali ya kukata harufu ambao huua bacteria wa asili wa eneo la uke na kukaribisha bacteria wanaosababisha maradhi kuzaliana kwa wingi.
---->Vifuatavyo pia vinaweza vikachangia
4. Ujauzito –mara nyingi hushusha kinga ya mwili ya mjamzito
5. Upungufu wa homon ya ya k**e Oestrogen husababisha bacteria wasababishao U.T.I kuzaliana kirahisi
*c)Kwa wote*
1. Kutokunywa maji na vinywaji kwa wingi –kunywa maji mengi husababisha mkojo kuzalishwa kwa wingi, na kukojoa mara kwa mara na hivyo kusafisha njia ya mkojo
2. Kuwekewa mirija inayosaidia kutoa mkojo nje inaweza pia kukaribisha maambukizi
3. Matatizo ya figo na mengine kwenye njia ya mkojo yanayoweza kuziba njia ya mkojo
29/05/2023
🍃MAMBO 5 YA KUEPUKA ILI UWE NA AFYA BORA YA UZAZI
1. Zingatia usafi wa nguo za ndani na mwili kwa ujumla
*
2. Epuka matumizi ya vitu vinavyovuruga mfumo wako wa hedhi.
✓ Usitumie P2, usutumie sindano za majira, vijiti, wala vidonge
3. Epuka kushiriki tendo la ndoa na wanaume wengi, tena bila kinga. Ukiweza kaa na mwanaume mmoja tu
Na uwe mwaminifu.
4. Usifanye arbotion. Ikitokea umeshafanya mara moja, usifanye mara ya pili, ikitokea umeshafanya mara ya pili, usifanye mara ya tatu.
✓ Unahatarisha kizazi chako, kuna uwezekano wa kuja kukosa mtoto kwa badae.
5. *Usikae na tatizo lolote la uzazi kwa muda mrefu.
K**a una tatizo lolote, using'ang'anie kuendelea kutumia dawa za aantibiotics wakati hazikusaidii...
Wasiliana nami akupe msaada usiendelee kuteseka tena.
_Jenga afya bora, uwe na maisha marefu yenye furaha_
Ni mimi ninaejali afya yako ya uzazi.
Maximilian.
0784707985
28/05/2023
*P.I.D NINI,DALILI ZAKE NI ZIPI, MADHARA YAKE NI YAPI?*
P.I.D- Pelvic Inflammatory Disease.
P.I.D Ni maambukizi kwenye via vya uzazi kwa mwanamke ambayo huusisha maambukizi kwenye shingo ya kizazi(CERVICITIS),nyama kwenye mfumo wa wa uzazi(ENDOMETRITIS) na mirija ya uzazi(SALPINGITIS)
Kuna aina mbili ambayo ni chanzo cha maambukizi ya ugonjwa wa P.I.D ni NEISSERIA GONORNOAE na CHLAMYDIA TRACHOMATIC
*WANAMKE ANAUPATAJE UGONJWA WA P.I.D*
-Kupitia ngono zembe
-Kuwa na mpenzi zaidi ya mmoja
-Kufanya mapenzi bila kutumia kinga
-Kupitia magonjwa ya zinaa hususani kaswande na kisonono
-Kupitia kunyonywa ukeni mara kwa mara
-Utoaji wa mimba na kutosafishwa vizuri baada ya kutoa mimba
-Kuweka vitu ukeni ili kuufanye uke ubane au kumvutia mpenzi wako
-Kutumia dawa na njia za kuzuia mimba(vijiti na sindano)
- Kuwa na U.T.I. sugu au fungus ya muda mrefu
*DALILI ZA P.I.D*
-Kutokwa na uchafu mzito sehemu za siri yaweza ukawa njano, mweupe au maziwa
-Uke kutoa harufu mbaya
-Kuwashwa sehemu za siri
-Maumivu ya tumbo chini ya kitovu
-Uke kuwa mlaini sana
-Maumivu wakati wa tendo la ndoa
-Kuvurugika kwa hedhi
-Kutokwa na maji maji ukeni kupita kiasi
-Maumivu wakati wa kukojoa
-Homa, uchovu na kizunguzungu
*MADHARA YA P.I.D*
-Maumivu ya tumbo au nyonga ya mara kwa mara mara baada ya tendo la ndoa. au kipindi cha upevushaji mayai hali hii hutokana na majeraha yaliyopi katika mirija ya uzazi
-Kusababisha majeraha ndani na nje ya mirija za uzazi ambayo hipelekea mirija kuziba
-Kubeba mimba nje ya kizazi husababishwa yai kushindwa kufika kwenywe mji wa uzazi kupitia mirija ya uzazi
-Ugumba kwa mwanamke
-kupata kansa ya shingo ya uzazi
*JINSI YA KUEPUKANA NA P.I.D*
Japo kuwepo na tiba za kujitibu lakini unashauriwa kinga ni bore kuliko tiba hivyo zingatia yafuatayo;-
-Epuka kufanya ngono zembe
-Usifanye mapenzi baada ya kujifungua au mimba kutoka
-Weka tabia ya kufanya vipimo mara kwa mara
-Kuwa msafi na nguo zako za ndani na kula lishe bora
-Epuka kushare nguo za ndani
*UNAPOONA DALILI ZA UGONJWA HUU WAHI KUPATA MATIBABU. KWANI UGONJWA HUU NI HATARI NA HUWEZA KUKUSABABISHIA UGUMBA AU KANSA YA SHINGO YA KIZAZI*
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Miyuji
Dodoma