Afaya ya uzazi wanawake

Afaya ya uzazi wanawake

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Afaya ya uzazi wanawake, Health/Beauty, Dodoma.

Dawa za uzazi wanawake
📣Suluhisho ya Ugumba
📣Hormone Imbalance
📣Mimba kuharibika
📣UTI Sugu & PID
📣Harufu mbaya ukeni
📣Ukavu ukeni wakati wa tendo
📣Tunatibu Uvimbe ovarian cyst
📣Miwasho ukeni
📣Kukosa hedhi

TUNATOA ELIMU YA AFYA KWA WANAWAKE

19/08/2024

*USITUMIE HIVI VITU K**A UPO PERIOD*

1.🌸🤝Usitumie Kinywaji Cha Baridi Sana Hata K**a Ni Maji Hakikisha Yanakuwa Ya Joto La Kawaida

2.🌸🤝Epuka Vinywaji Vyenye Kafeina [Caffeine] K**a Kahawa, Soda Za Viwandani Na Kinywaji Chochote K**a Kina Kafeina Inasababisha Kuvurugika Kwa Siku Za Hedhi Na Misuri Ya Tumbo Kukaza Hivyo Kukusababishia Maumivu Ya Tumbo

3.🌸🤝Usibebe Vitu Vizito Sana Au Kufanya Kazi Ngumu Sana Siku Za Hedhi Kutoka.

4.🌸🤝Usitumie Tango Wala Juisi Yake Kipindi Cha Hedhi Maana Ubaridi Wake Hufanya Mwili Kupoa Sana Na Kusababisha Maumivu Wakati Wa Hedhi

Katika Kipindi Hiki Ni Vyema K**a Utapata Vyakula / Viungo Vya Kuongeza Joto Mwilini Mfano Tangawizi, Iliki, Manjano, karafuu, Mdalasini, Kitunguu Swaumu, Lozi [Almonds], Matunda Na Mboga Za Majani.

*AFYA BORA NDIO FURAHA YETU*

19/08/2024

FAIDA ZA KUTUMIA JUISI YA BAMIA KILA SIKU KWA MWANAMKE.

1.🪀🤝 Huondoa chunusi.
2.🪀🤝 Hutibu maumivu yote ya viungo mfano kiuno, miguu kuwaka moto, pingili n.k.
3.🪀🤝 Huleta hamu ya tendo la ndoa.
4.🪀🤝 Huongeza ulaini kooni yaani kwa wenye sauti za kukoroma zinakuwa nyororo.
5.🪀🤝 Hutibu vidonda vya tumbo kwa 100%.
6.🪀🤝 Hukaza kizazi kilicholegea au wenye uke mkubwa akitumia juisi ya bamia uke unabana unakuwa mdogo.
7.🪀🤝 Husafisha damu.
8.🪀🤝 Husawazisha mpangilio wa homoni yaani hutibu homoni imbalance.
9.🪀🤝 Ni dawa ya macho na masikio yanakuwa yanatoa machozi machozi na masikio yanayowasha.
10.🪀🤝 Huondoa mistari ya mafuta mafuta mabaya kwenye mapaja, nyuma ya magoti, kwenye mikono.
11.🪀🤝 Hutibu ngozi iliyokak**aa. Inakuwa nzuri ya kuvutia hata bila kupaka mafuta.
12.🪀🤝 Hutibu UTI.
13. 🪀🤝Hutibu chango la uzazi.
14.🪀🤝 Husaidia mmeng'enyo wa chakula ndo maana kam ulikuwa hupati choo utaanza kupata choo vizuri sana.

*TUENDELEE KUPIGANIA AFYA ZETU BILA KUCHOKA*

Afya Bora Ndio Furaha Yetu.

28/07/2024

SIFA ZA MWANAMKE ANAEWEZA KUSHIKA UJAUZITO/KUPATA MTOTO

1.Asiwe na maambukizi yoyote kwenye mfumo wake wa uzazi K**a vile UTI,FANGASI,PID,BACTERIAL VAGINOSIS na magonjwaa mengine ya zinaa...

2.Asiwe na shida ya Mvurugiko wa homones/homonal imbalnce:Kuna uhusiano mkubwaaa Sana Kati ya mwanamke kushika mimba na mzunguko wake wa hedhi ama Aina ya hedhi anayopata...

3.Mayai yawe yanapevukaa yaani awe anapata ute wa ovulation...

4.Mirija iwe Safi,isiwe imezibaa kwa namna yoyote ile

5.Asiwe na changamoto ya ukavu ukeni, Kwani mbegu za mwanaume hutegemeaa Sana uwepo wa majimaji ukeni ili ziweze safiri kwa Kasi inayotakiwa...

6.Asiwe na uvimbe wa Aina yoyote iwe kwenye kizazi (fibroids) ama kwenye vifuko vya mayai (overian cyst)...

IKUMBUKWE MATUMIZI YA NJIA ZA UZAZI WA MPANGO ZA KISASA K**A vijiti,kitanzi,vidonge,sindano na hata p2 huchangiaa Sana mwanamke kupoteza uwezo wake wa kushika mimba sababu ya sumu yake...

K**A UMESHAJARIBU KUBEBA MIMBA BILA MAFANIKIO YOYOTE NIPIGIE KWA MSAADA ZAIDI...

25/07/2024

KWANINI PID INAKURUDIA MARA KWA MARA(SABABU #2 NI YA KUZINGATIWA SANA)

Kuna sababu kadhaa ambazo zinaweza kusababisha Pelvic Inflammatory Disease (PID) kurudi baada ya matibabu:
📣 Maambukizi Yasiyokamilika:
📣Wakati mwingine, matibabu ya PID hayamalizi kabisa maambukizi ya bakteria au haukufuata muda wote wa matibabu ulooshauriwa na daktari. Hii inaweza kuruhusu bakteria kuendelea kuwepo na kusababisha kurudi kwa maambukizi.
📣Bakteria Kustahimili Dawa:
📣Baadhi ya bakteria wanaweza kubadilika au kuwa na upinzani dhidi ya dawa fulani, hivyo kuwa vigumu kwa antibiotics kutibu maambukizi, na hivyo kurudi kwa PID.
📣Mfumo wa Kinga ya Mwili:
📣Katika hali fulani, mfumo wa kinga ya mwili wa mtu unaweza kuathiriwa, ukifanya iwe vigumu kwa mwili kupigana na maambukizi ya bakteria, na hivyo kuongeza hatari ya kurudi kwa PID.
📣Mienendo ya Kingono:
📣 Mabadiliko katika mienendo ya kingono, mabadiliko/kubadilisha washirika wa kingono, au kutofuata mbinu bora za kinga dhidi ya maambukizi ya kingono kunaweza kusababisha kurudi kwa maambukizi ya bakteria yanayosababisha PID.
Kwa kuzingatia maelekezo ya daktari, kutumia dawa kikamilifu, na kufuata mbinu za kinga dhidi ya maambukizi ya kingono, inaweza kupunguza hatari ya kurudi kwa PID. Ni muhimu kushauriana na daktari k**a kuna dalili za kurudi kwa PID ili kupata matibabu sahihi na kuzuia madhara zaidi.
Tuwasiliane Kwa matibabu yatakayokomesha kujirudia rudia kwa PID

Kwa ushaur na tiba wasiliana nasi

22/07/2024

FAHAMU MADHARA YA KUFANYA MAPENZI KIPINDI CHA HEDHI KWA MWANAMKE

Kufanya mapenzi wakati wa hedhi ni kitendo cha kujihusisha na mapenzi na msichana au mwanamke aliye katika siku zake za kisichana..Kuna madhara mengi yanaweza yakatokea na kwa kawaida si mazuri kwa afya ya wote wawili.Hivyo kwa ushauri huwa tunapenda watu wajali sana afya zao na si kuzidumaza na kuendekeza hisia kwani hiloo ndilo kosa kubwa la vijana wengi wa siku hizi...

Zifuatazo ni baadhi ya madhara yanayoweza kutokea endapo wawili hawa watafanya ngono wakati mwanamke/binti yupo katika siku zake{period}..

MADHARA KWA MWANAMKE.
1.Kupatwa na maambukizi kwenye viungo vya ndani vya uzazi k**a vile shingo ya kizazi,mirija ya uzazi kwa ujumla wake anaweza kupata  tatizo la PID( PELVIC INFLAMATORY DISEASES) tatizo ambalo linaweza kuathiri mfumo wake wa uzazi.

2.Maumivu makali ya tumbo hasa kwa wale wanaopatwa na maumivu wakati wa hedhi.(Dysmenorrhea).

3.Utokaji wa damu unaweza ukaongeza kuliko vile inavyotoka kwa kawaida yake.

4.Utasa au Ugumba.

5.Kuvimba kwa kuta za ndani za uke kwa kuwa wakati wa hedhi zenyewe huwa tayari zimevimba au kutanuka  pia itamsababishia maumivu kwenye uke wakati wa tendo la ndoa.

6.Athari mbaya ya kisaikolojia:Mwanamke atahisi kuwa mumewe hamjali wala hampendi bali anajali hisia zake za kingono na kwamba yeye anatumika kingono tu.Pia kuona kuwa mumewe hajali afya yake pamoja na maumivu anayoyapata lakini bado huyu mume anataka kusex

22/07/2024

Namna 10 Za Tiba Ya Tatizo La Ugumba (Infertility)
Tiba ni k**a ifuatavyo;
1. Ushauri nasaha na kuwaelimisha wapenzi wawili –
***Matatizo mengi ya ugumba hutokea kutokana na uelewa au ufahamu mdogo wa elimu ya uzazi na ya kujamiana kwa wapenzi au wanandoa.
***Kuna wanaume wengi ambao hufika kilele haraka wakati wa kujamiana na hivyo kutoa shahawa mapema (au kukojoa) kabla ya muda muafaka (premature ej*******on), hii husababisha kutopata ujauzito ambapo lawama zote hupelekwa kwa mwanamke pasipo mwanamume kugundua kuwa tatizo ni lake.
Ifahamike kwamba hakuna muda uliotengwa ambao ni muafaka wa kufika kilele au kukojoa kwa mwanamume lakini watafiti wa mambo ya kujamiana wanashauri angalau mwanamume afike au akojoe baada ya dakika 15 na kuendelea.

2. Tatizo jengine ni kutofahamu lini hasa ni muda muafaka wa kujamiana ili kushika mimba kwa urahisi.
Kuna wanawake ambao hawajui hata mzunguko wao wa hedhi (yaani hawajui wanaanza na kumaliza hedhi lini na wakati wa hedhi wanatumika kwa muda wa siku ngapi).
Ongeza nafasi yako ya kushika ujauzito kwa kujamiana angalau mara 3 kwa wiki kuelekea wakati wa ovulation au kujamiana wakati wa kipindi chote cha ovulation.
Ovulation hutokea wiki 2 kabla ya mzunguko wako mwengine wa hedhi, k**a una mzunguko wa hedhi wa siku 28 (yaani kila baada ya siku 28 unapata hedhi), ni vizuri kujamiana angalau kwa siku 3 kati ya siku ya 7-18 baada ya kupata hedhi.
3. Kupunguza/Acha kunywa pombe kupindukia, kuvuta sigara, kuacha matumizi ya bangi, kokeni nk.
4. Kupunguza kiwango cha mazoezi kwa wanawake.
5. Kupunguza unene uliopitiliza
6. Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu kwani kuwa na wapenzi wengi huongeza athari ya kupata magonjwa ya zinaa.
7. Kuacha tabia ya kuvaa nguo nzito au zenye kuleta joto kali sehemu za siri kwa wanaume kwani joto kali sana hupunguza kiwango na kuathiri utolewaji wa shahawa.
8. Kula mlo kamili na wenye virutubisho vyote muhimu kwa afya njema.
9. Dawa za kutibu magonjwa kwenye mfumo wa uzazi, magonjwa ya zinaa nk.
10. Njia za kitaalamu za kupata ujauzito zijulikanazo k**a in vitro fertilization na intrauterine fertilization.

Je, una tatizo lolote la uzazi?
Tuambie, tunaweza kuwa sehemu ya suluhisho kwako

22/07/2024

Hedhi bora ni dalili ya afya njema ya uzazi, k**a wewe ni mwanamke na unaona kitu hakipo sawa katika hedhi yako ni vema uwahi upate ushauri na msaada kwa wataalamu.
Mwanamke akiwa anapata hedhi yenye sifa hizi hapa chini, hapa tunasema Yuko kwenye Hali ya usalama kwenye upande wa mzunguko wake wa hedhi.
📣Hedhi bora hupatikana mara moja kwa mwezi, yaani mfano k**a mzunguko wako ni siku 28 basi hedhi yako inatakiwa kupatikana kila baada ya siku 28 na k**a hedhi yako haitabiriki ujue kuna shida ambayo unapaswa kutatua kupata hedhi bora.
📣Hedhi bora damu haiwi nyepesi sana au nzito sana, hutakiwi kupata hedhi nzito,hedhi yenye vinyama nyama k**a vipande vya maini.
📣Hedhi bora haiambatani na maumivu makali, Kuna baadhi ya wanawake wanapata maumivu makali kiasi kwamba wanashindwa hata kuendelea na shughuli zao za Kila siku
Je umeshawahi kuona mwanamke siku akiingia kwenye siku zake hupata maumivu NA hushindwa kufanya kazi?
Kwa kawaida maumivu yanapaswa kuwepo ila siyo makubwa ya kufanya MTU asifanye kazi, k**a unapitia kipindi hichi basi unatakiwa kuonana na mshauri kupata hedhi bora.
📣Hedhi isiyo bora husababishwa mwanamke kupata mabadiliko ya mwili mfano kuvimba usoni au kuwa na upele,au chunusi nyingi,
📣Hedhi bora hupatikana siku 3 mpaka 7,katika mzunguko wa mwezi siku za hedhi zinapaswa kuwa 3 mpaka 7 chini ya hapo au zaidi ni ishara ya hatari katika afya yako
Ukijichunguza kwenye mzunguko wako wahedhi je unahisi uko kwenye hedhi salama?
Share na sisi hapa
Matatizo binafsi zungumza namimi kwa kutuma ujumbe whatsapp

19/07/2024

TATIZO LA KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI (FALLOPIAN TUBES)

Mirija ya uzazi kitaalamu inajulikana k**a Fallopian tubes. Hii ni mirija midogo iliyopo kwenye mfumo wa uzazi wa mwanamke ambayo husaidia kupitisha yai lililopevuka hadi kufika kwenye mji wa mimba.

KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI KUNASABABISHA VIPI UGUMBA?
Kila mwezi yai la mwanamke linapopevuka huachiliwa kutoka kwenye mfuko wa mayai na kusafiri kupitia mirija ya uzazi kuelekea kwenye mji wa mimba. Mbegu za kiume pia husafiri kutokea kwenye shingo ya kizazi na kulifata yai kwenye mirija ya uzazi ili kulirutubisha. tuelewe kwamba urutubishwaji wa yai unafanyika kwenye mirija ya uzazi wakati yai linasafiri kuelekea kwenye mji wa mimba.
DALILI ZA MIRIJA YA UZAZI KUZIBA
Sio watu wote wenye tatizo hili huonesha dalili.Asilimia kubwa ya wanawake wenye tatizo hili hawaoneshi dalili zozote.
Aina ya tatizo hili inayojulikana kitaalamu k**a HYDROSALPINX ndo huwa na dalili za maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kutokwa na maji maji mengi ukeni.
Hydrosalpinx ni aina ya tatizo la mirija kuziba ambapo mirija inaziba na kujaa maji.
pia mwanamke huweza kupata dalili k**a maumivu makali wakati wa tendo la ndoa na maumivu makali wakati wa hedhi

VISABABISHI VYA TATIZO LA MIRIJA KUZIBA
Kisababishi kikubwa cha mirija kuziba ni tatizo la maambukizi kwenye viungo vya uzazi (PID)
Na mara nyingi PID husababishwa na maambukizi ya magonjwa ya zinaa japo sio kila mwenye PID imetokana na magonjwa ya zinaa.

Sababu nyingine ni k**a
Magonjwa ya zinaa mfano Kisonono na Chylamidia
Maambukizi kwenye kizazi baada ya mimba kuharibika (abortions)
Historia ya tatizo la kidole tumbo (Appendicitis)
Historia ya Mimba kutunga nje ya kizazi
upasuaji ambao unahusisha mirija ya uzazi

Kwa USHAURI na Tiba wasiliana nasi

18/07/2024

TUONGEE UZAZI

ZITAMBUE DALILI ZA HATARI WAKATI WA UJAUZITO PART 1

Dalili za Hatari Wakati wa Ujauzito, Sababu Zake na Hatua za Kuchukua

Wakati wa ujauzito, ni muhimu kwa mama mjamzito kuwa makini na afya yake na afya ya mtoto aliyepo tumboni. Kutambua dalili za hatari mapema kunaweza kusaidia kuzuia matatizo makubwa na kuchukua hatua mapema Ili kulinda afya ya mama pamoja na mtoto .miongoni mwa dalili hizo ni

Maumivu Makali ya Tumbo
Maumivu makali ya tumbo yanaweza kusababishwa na ujauzito wa nje ya mfuko wa uzazi (ectopic pregnancy), kuharibika kwa mimba( miscarriage)ikiwa ujauzito upo kipindi Cha kwanza(1st trimester), kujitenga kwa placenta( placenta abruptio) hii huambatana na maumivu makali ya tumbo, Uchungu kabla ya mimba kufikisha miezi 9( preterm Labor), au shinikizo la juu la damu (preeclampsia),n.k
Hatua za Kuchukua: Tafuta msaada wa haraka Kwa kwenda kituo Cha Afya au hospitali ya karibu ili kupata uchunguzi na matibabu sahihi.
Kutokwa na Damu NyingiInaweza kuwa ishara ya kuharibika kwa mimba,( 1st trimester )ujauzito wa nje ya mfuko wa uzazi(ectopic pregnancy), kujitenga kwa placenta, placenta previa, au Uchungu kabla ya muda k**a ilivyozoeleka(preterm labor)

Kuona Ukungu (Blurred Vision)Inaweza kusababishwa na shinikizo la juu la Damu wakati wa ujauzito(preeclampsia)i hasa ikiambatana na dalili k**a maumivu makali ya kichwa,kuvimba uso na mikono., maumivu ya tumbo,lakini pia yaweza kuwa kisukari cha ujauzito, mabadiliko ya homoni, au shinikizo la juu la damu lilokuwepo kabla ya ujauzito.

Maumivu Makali ya KichwaMaumivu makali ya kichwa yanaweza kuwa dalili ya preeclampsia au upungufu wa maji mwilini

Kuvimba Kwa Ghafla kwa Uso, Mikono, na Miguu( severe oedema)
Hii inaweza kuwa ishara ya preeclampsia au matatizo mengine ya kiafya yanayohusiana na shinikizo la damu.

KUMBUKA UONAPO DALILI HIZI WAHI HARAKA HOSPITALI AU KITUO CHA AFYA KILICHOPIO KARIBU UWEZEKUPATIWA HUDUMA NA MATIBABU MAPEMA PAMOJA NA KUFANYIWA UCHUNGUZI
Linda Afya yako na ya mtoto aliyeko tumboni

Photos from Afaya ya uzazi wanawake's post 18/07/2024

Sababu 6 za Kujifungua kwa Upasuaji 💉

1️⃣ Leba haiendelei kawaida

👉🏽 Mfano ni kuchelewa kufunguka kwa seviksi au kusukuma wa muda mrefu bila mafanikio

2️⃣ Jinsi mtoto alivyokaa

👉🏽 Upasuaji huwa ndiyo njia salama zaidi ya kuzaa watoto ambao miguu au matako yao huingia kwenye njia ya uzazi kwanza (breech) au watoto ambao pande au mabega yao hutangulia (transverse).

3️⃣ Matatizo ya placenta

👉🏽 K**a placenta previa (placenta inayofunika seviksi) au kupasuka kwa plasenta (placenta inayojitenga na ukuta wa uterasi), ambayo inaweza kuongeza hatari ya kutokwa na damu wakati wa kuzaa kwa uke.

4️⃣ Uzito wa mtoto

👉🏽 K**a mtoto ana uzito wa zaidi ya kilo 4, kuna hatari kubwa ya mabega ya mtoto kukwama nyuma ya mfupa wa pelvic ya mama wakati wa kujifungua (shoulder dystocia au dystocia ya bega). Upasuaji unaweza kupendekezwa ili kupunguza hatari ya dystocia ya bega.

5️⃣ Mjamzito alishawahi jifungua kwa upasuaji

👉🏽 Mara nyingi, wahudumu wa afya wanapendekeza kurudia C-Section ili kupunguza hatari ya mpasuko wa uterasi wakati wa leba.

6️⃣ Pendekezo la mjamzito

👉🏽 Mjamzito mwenyewe anaweza pendekeza ajifungue kwa upasuaji.

18/07/2024

FAIDA ZA MWANAMKE KUFIKA KILELENI.
Unajua kwamba kuna faida mbalimbali za kiafya kwa mwanamke kufika kileleni? Hapa ninakuletea umuhimu wa mwanamke kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa:
1.HUONDOSHA MAUMIVU: Kufika kileleni humsaidia mwanamke kuondokana na maumivu mbalimbali anayoweza kuwa anayahisi mwilini mwake. Hutoa oxtin ambayo husaidia kutoa homoni ya endorphin mwilini. Homoni ya endorphin hufanya kazi ya kupambana na maumivu mbalimbali mwilini.
2.HUIMARISHA MFUMO WA KINGA: Tafiti mbalimbali zimethibitisha kuwa mwanamke kufika kileleni husaidia kuimarisha mfumo wa kinga mwili kutokana na baadhi ya homoni ambazo mwili unazitoa wakati wa tendo la ndoa.
3.HUTUNZA UJANA: kufika kileleni humsaidia mwanamke kukabiliana na alama za uzee? Kufika kileleni hukuondolea wasiwasi na kukupa utulivu dhidi ya mashinikizo ya kimaisha ambayo hukuelemea na kukufanya uonekane mzee. Sambamba na hilo, tafiti mbalimbali zimethibitisha kuwa mshindo una mchango mkubwa katika kutunza uzuri na afya ya ngozi.
4.HUONDOA MFADHAIKO: Kwa upande wa kisaikolojia, kufika kileleni humfanya mwanamke kuwa mtu mwenye furaha zaidi maishani. Mshindo huamsha upya upendo na mahabba jambo linalomuweka karibu zaidi na mumewe na kumfanya kuwa na raha na furaha katika maisha yake ya kimahabba.
5.HUBORESHA UZAZI: Tafiti mpya zimethibitisha kuwa kufika kileleni huboresha na kuimarisha suala la uzazi kwa mwanamke kwa sababu huathiri sana mzunguko wa yai na kuongeza kiwango cha estrogen katika mwili wa mwanamke.
6.HUCHANGAMSHA MZUNGUKO WA DAMU: Mshindo wa tendo huchochea na kuchangamsha mzunguko wa damu katika mwili, jambo linalosaidia kustawisha seli na viungo vya mwili. Faida ninyingi Wala sitoimaliza chamsingi jitahidi kumkojoza mkeo kwa Sana Raha ya tendo la ndoa mkojozane na kuridhiana.

Onyo:ni kwa wanandoa tu..

❤️NDOA NI IBADA ❤️

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dodoma?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Dodoma