Amsha Ndoto Zako

Amsha Ndoto Zako

Share

Nasaidia Watu Kuamsha Ndoto Zao Ambazo Wanahisi Zinakufa Na Kuzifanya Zitimie Hasa Ndoto za Kiuchumi

01/10/2024

USITUKANE KAZI YAKO

Kazi uliyonayo haijarishi ni ipi lakini unatakiwa kuiheshimu Sana Kwani hiyo ndiyo Inakupa kula na kununua mahitaji mwengine

Siku moja Nilikuwa kwenye seminar ya mwalimu Fransis Langula alifundisha kuwa Kuna watu hawaziheshimu kazi zao wanaona Ni K**a matesa wanaona Ni kazi ndogo Sana isiyo na kipato

"Basi kazi yenyewe kazi Basi tu Tuende tukapoteze Muda na kuhangaika Huku TU"

Maneno haya Ni moja ya Maneno yanayoonesha kuitukana kazi ambayo upo nayo

Unahisi utafanikiwa kweli kupitia kazi hiyo Kwani husemekana K**a huumpendi mwalimu Basi Ni ngumu Sana kulifaulu somo lake lakini K**a Unampenda mwalimu Basi hata mafunzo yake utayaelewa

K**a utaipenda kazi yako Ni lazima itakupa mafanikio

Namtaka mtu mmoja ambaye anahitaji nimuelekeze kazi ambayo ataifanya kwa moyo na kwa kuipenda Wala hataitukana

Bonyeza button ya WhatsApp hapo chini

grow wise

30/09/2024

MUDA WA KIBONGO

Hivi umeshawahi Kujiuliza Wakati unapanga Appointment na mtu kwanini Mara nyingi Wengi wanapenda kusema Hakikisha usiwe Muda Wa Kibongo

Hivi hii Inamaana gani??

Ukifatilia Sana Kuna baadhi ya Sehemu wanasema Tanzania ni Sehemu pekee ambayo inamuda mwingi Sana zaidi ya Masaa 24

Hii humaanisha sisi watanzania hatuthamini Muda kabisa Yan inafika muda unaamka huna ratiba na mpaka Unasema daaaah Siku ya Leo ndefu sana🤣

Hii Ni kwa sababu huna ratiba ambayo itakufanya uone Muda hautoshi umechukulia maisha kiurahisi Sana hauna Ndoto inayokusukuma kufanya kazi Sana āœšŸ½

Watu wa Nchi nyingine huwa Muda hauwatoshi mpaka wanafanya kazi usiku Yan Muda hautoshi kabisa ila sisi saa MBILI kamili tumeshalala zamani tunakoroma🤭

Kiufupi Ni kwamba Ukiwa Umepanga mikakati yako vizuri Muda hautoshi kabisa Yan Muda Ni mchache Sana utakuja kuona unawexa ukawa unalala saa Saba usiku kila Siku

No way inawezekana huelewi ulale saa 7muda wote unafanya Nini tafuta Ndoto yako Tena iwe kubwa ya kukuzidi halafu jiapie baada ya Miaka 5lazima niitimize Hapo lazima Muda usitoshe

Usilizike na muda wa Masaa 24ukalala ukawa unaona Muda Ni mwingi

Tumia Muda vizuri K**a wazungu ili na wew ujibadilishie taswira upo Tanzania lakini Unamuda wa marekani🤣

*grow wise*

28/09/2024

WEKEZA KWENYE KUJIFUNZA

Siku moja Wakati nimeamua rasmi kuwa mwanauchumi haikuwa rahisi kwangu nilitumia Muda mwingi Sana kuwaza biashara ya kufanya

Na kweli nilianzisha na ilienda lakini baada ya Muda biashara ile ilikufa Hivi unaweza kujua Ni kwanini nilianzisha biashara zilikufa

Nilifanikiwa kuwaza biashara nyingi lakini katika hizo nyingi mbili nilifanikiwa kuzifungua na kuziendesha niligundua kuwa nahitaji Muda mwingi Kujifunza hasa kwa

Walionitangulia
Walionizidi
Waliochini yangu
Na ninaolingana nao

Nikiwa na imani kubwa Sana kwamba mtu aliyekutangulia anauwezo mkubwa Sana kwan anaweza kukifahamisha vitu vingi Sana

Wakati natafakari Mambo mengi niligundua K**a wew Unahitaji kufanikiwa Ni lazima uwekeze Muda mwingi kwenye Kujifunza hasa kwa watu wa uchumi nakuhakikishia kafanikiwa

Na kuelekeza watu watakao kufundisha zaidi kuhusu wew kupiga hatua Kwan mm wamenisaidia Sana
1. Joel Nanauka
2. Dactariwamauzo

Ni Watu Ambao nimetumia nguvu kubwa Sana kuwasikiliza na hata kusoma vitabu vyake(Joel Nanauka)

Ukijifunza Kuna maarifa yatakuingia zaidi na utajua na namna ya kuendesha Mambo

Hata neno la Mungu linasema watu wangu wanaangamia kwa Kukosa maarifa

Usikubali kuangamia jaribu kutafuta maarifa kwa namna yyte ile

Wakati Unahitaji kufanikiwa kuwa tayar Kujifunza

growwiseāœšŸ½

27/09/2024

UNAHISI KUFIKA MWISHO?

Hili ni Swali kwako wewe?
Kuna Muda ushawahi kuhisi huwezi Kuendelea kabisa na hata Ukitaka Kuendelea huoni pa kuanzia mwisho wa Siku Unahisi nimefika mwisho wa mawazo yangu

Unaweza ukawa umeshafanya biashara zaidi ya mbili lakini zinafel(Huu Ni mfano wangu kabisa🤣)

Na inawezekana umetafuta ajira kwenye maofisi ya watu lakini Umeshindwa ukahisi labda Mimi ndo nimeubwa Hivi hebu ngoja nisubiri kuolewa tu🤭

Unajua option ya kuolewa bwana(nifatilie kwenye nakala yangu nitakwambia majukumu ya mke katika uchumi wa familia)

Anyway tuendelee usikubali kabisa kufika mwisho kumbuka hata waliofanikiwa walifeli Sana lakini mwisho wa Siku waliofanikiwa kwahiyo usikubali kufika mwisho

Ukihisi kufel tafuta vitabu tafuta watu wanaoweza kukunyanyua kimawazo ukawapigia nakwambia Kuna hatua lazima upige

Kuna dada mmoja alifilisika ikafika hatua akataka kujiua lakini aliponishirikisha nilimtia moyo sana na aliamka Tena

Amka tena kwanza kukata tamaa Ni Dhambi kiimani

Ukihisi kufika mwisho fikiria ukiishia hapo Ndoto zako utazitimizaje?

Amka amsha Ndoto zako Kwani maisha yako ya mbele Ni mazuri sana

Haloo usihisi kufika mwisho kabisaāœšŸ½

27/09/2024

UNAIKUMBUKA NDOTO YAKO WAKATI UPO MDOGO

Siku moja Nilikuwa nazungumza na Coach wangu Mr Elia sereka na alisema Kila mtu ndoto yake Ni ile aliyokuwa anaipenda kuifanya Sana Wakati mdogo

Chukua dakika 2 kukumbuka Nini Ulikuwa unapenda kufanya Wakati mdogo.......

Ouky Hicho Hicho wengine tayar wameshapotea njia kabisa ila najua wengine walipenda kuunda watoto kwa udongo ama gari ama kutengeneza nyumba kubwa Sana n.k

Hivi Unafahamu hii Ndoto Ni ya kwel na inaishi K**a Utaamua kuiamsha

Wazungu huangalia Ndoto za watoto wao wakiwa wadogo na hufanya kuwasaidia tu kutimiza zile Ndoto

Hata wewe bado hukachelewa unanafasi ya kujenga ile nyumba ya kifahari uliyokuwa unaitengeneza nikwambie tu unanafasi ya kununua gari lako lile ulilokuwa unalitengeneza Ni wew tu kuamua kuamsha ile ndoto

Na utqiamshaje Ni kwa maamuzi yako ya Leo ya kuanza kufanya vitu vya maendeleo ili uweze kuitimiza ile ndoto

grow wise

27/09/2024

UTAWEZAJE KUISHI BILA AJIRA

Haya Kuna mtu ananiambia mimi sitaki kazi ama biashara ninachohitaji Ni AJIRA tu

Ukweli Unaouma Ni kwamba

Sasa ivi AJIRA zimekuwa ngumu Sana si serikalini wala kwenye Mashirika binafsi
Unajua kwaninišŸ¤”

Wasomi wamekuwa wengi Sana na makampuni ama ofisi zimekuwa chache

Hatuwezi kubanana wote huko🤣

Ouk ukikaa kwa dakika tano ukiwa bafuni unaoga ndo utagundua hichi ninachokiongea

Licha ya ukosefu huo wa ajira haina maana tuishi bila hela ila inatubidi tupambane kwa kutafuta kazi ya kufanya itakayotuongizia kipato Cha Kila Siku

Kuna Siku nilifikiria kuhusu Elimu yangu nilitamani nizimie kwa Nusu saa🤣 story hii nitakuletea endelea kunifatulia

Tuendelee hivyo Tukikwambia Kuhusu Kushikiria Fursa za Kazi tunazokuambia Hebu elewa Usisubiri mpka yakufike shingoni maisha yako Yawe magumu Wakati Unauwezo wa Kuyabadilisha leo

Wekeza Sana Kwenye Kujifunza endlea kunifatulia ili siku ukiamua kuanza usirudi nyuma Ni kuanza tu na mimi ninampango wa kukusindikiza kuyafikia Yale uliyoyaota Wakati upo mdogoāœšŸ½

27/09/2024

*UTOFAUTI WA WATU KATIKA KUYACHUKULIA MAMBO*

Katika fursa hii ya kazi niliyoitangaza Kuna watu Wengi wamenifata na watu Hawa wanatofautiana katika ufatiliaji wa Mambo

Hii hutegemea na uhitaji wa mtu pamoja na Fikra za mtu

K**a mtu ameweza Kutafuta kazi kwa muda mrefu na anashauku ya Mafanikio na mtu akamwambia katika hili utafanikiwa Ni lazima ajaribu ili aweze kafanikiwa

Lakini ambaye bado Hana Ndoto za kafanikiwa HAFAHAMU umuhimu wa ndoto na kufanya kazi kwa makini ili afanikiwe atachukulia hili kawaida Sana na atapotezea ataona K**a alipotezewa Muda

Jambo hili linajulikana kwa watu Hawa wawili tofauti

Hakika Hawa Ni watu wawili tofauti kwanzia mitazamo Yao,Ndoto zao na shauku zao

Unahisi wewe upo upande gani kwenye Hawa watu wawili🤭

Najua utasema wew unandoto
Hebu Niandikie Ndoto yako kubwa kwenye maisha yako Ni ninišŸ¤”

Hivi hujatumia dakika 10 kwel🤣

Ouky endelea kunifatulia ili Siku moja uje ushirikiane na Mimi kutimiza Ndoto zako

14/08/2024

Usitumie Nguvu Kubwa sana Kujilinganisha na watuāŽ
Ila tumia Nguvu Kubwa sana Kuwekeza nguvu,Muda na Pesa Zako kwenye Kutafuta Mafanikio yako

Kiufupi Mafanikio yapo ila ni wew hujaamua kuyatafuta Mafanikio hivyo weka nguvu na muda na pesa pia Kuwekeza Mafanikio yako ya Mbeleni

Jitahidi kutazama maisha ya badae
Kumbuka Maisha yako yanakuhitaji wew kwa asilimia Mia moja

11/08/2024

*Ujumbe Muhimu Kwa Wanawake Wote*

Wanawake wengi wamekuwa Wakisumbuliwa na Changamoto za Uchumi Ikiwemo
āŽKUSHINDWA KUJISIMAMIA
āŽKUISHIA NJIANI KWENYE BIASHARA
āŽKUTOKUONA FAIDA KATIKA BIASHARA
āŽKUKOSA MUONGOZO
KUTOKA KWA MZOEFU WA BIASHARA
āŽKUKOSA USHAURI WA KUENDESHA BIASHARA

K**a Wewe ni Mmoja Wao Ningependa Kuongea na Wewe

Kwa Jina Naitwa *LORUHAMA ROBERT*

Ninawasaidia Wanawake Kusimama na Kuendesha Biashara yake Itakayo saidia Kumuinua Kiuchumi na Kuondokana na Tegemezi

Nimejikita kwenye Kusimamia na Kuonesha njia sahihi ya Kupita Ili Kuhakikisha unafanikiwa

Wiki hii Nataka Niandae darasa la Bure la Namna ya Kukuza na Kusimamia biashara Yako chini Ya Usimamizi wangu

K**a Utapenda Kuhudhuria Darasa Hilo
Naomba Ubonyeze Kitufe Cha WHATSAPP Hapo Chini

Kisha Nitawasiliana Na Wewe ilituzungumze na Kukuandalia Wewe Pamoja Na Wanawake Wenzako Darasa bure Kabisa Kupitia Group La WHATSAPP.

Bonyeza Kitufe Cha WhatsApp Hapo Chini, Kabla Ya Darasa Letu Kujaa

Ni Mimi Mwenye Kujali kipato chako,

Loruhama Robert

Mkurugenzi, Amsha Ndoto Zako

Photos from Amsha Ndoto Zako's post 27/07/2024

Soma hizi Caption kwa umakini kuna kitu utajifunza

Photos from Amsha Ndoto Zako's post 27/07/2024

Soma Hizi Caption kwa umakini kuna Kitu Utakipata

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dodoma?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Dodoma
Dodoma