Amsha Ndoto Zako
Nasaidia Watu Kuamsha Ndoto Zao Ambazo Wanahisi Zinakufa Na Kuzifanya Zitimie Hasa Ndoto za Kiuchumi
01/10/2024
USITUKANE KAZI YAKO
Kazi uliyonayo haijarishi ni ipi lakini unatakiwa kuiheshimu Sana Kwani hiyo ndiyo Inakupa kula na kununua mahitaji mwengine
Siku moja Nilikuwa kwenye seminar ya mwalimu Fransis Langula alifundisha kuwa Kuna watu hawaziheshimu kazi zao wanaona Ni K**a matesa wanaona Ni kazi ndogo Sana isiyo na kipato
"Basi kazi yenyewe kazi Basi tu Tuende tukapoteze Muda na kuhangaika Huku TU"
Maneno haya Ni moja ya Maneno yanayoonesha kuitukana kazi ambayo upo nayo
Unahisi utafanikiwa kweli kupitia kazi hiyo Kwani husemekana K**a huumpendi mwalimu Basi Ni ngumu Sana kulifaulu somo lake lakini K**a Unampenda mwalimu Basi hata mafunzo yake utayaelewa
K**a utaipenda kazi yako Ni lazima itakupa mafanikio
Namtaka mtu mmoja ambaye anahitaji nimuelekeze kazi ambayo ataifanya kwa moyo na kwa kuipenda Wala hataitukana
Bonyeza button ya WhatsApp hapo chini
grow wise
30/09/2024
MUDA WA KIBONGO
Hivi umeshawahi Kujiuliza Wakati unapanga Appointment na mtu kwanini Mara nyingi Wengi wanapenda kusema Hakikisha usiwe Muda Wa Kibongo
Hivi hii Inamaana gani??
Ukifatilia Sana Kuna baadhi ya Sehemu wanasema Tanzania ni Sehemu pekee ambayo inamuda mwingi Sana zaidi ya Masaa 24
Hii humaanisha sisi watanzania hatuthamini Muda kabisa Yan inafika muda unaamka huna ratiba na mpaka Unasema daaaah Siku ya Leo ndefu sanaš¤£
Hii Ni kwa sababu huna ratiba ambayo itakufanya uone Muda hautoshi umechukulia maisha kiurahisi Sana hauna Ndoto inayokusukuma kufanya kazi Sana āš½
Watu wa Nchi nyingine huwa Muda hauwatoshi mpaka wanafanya kazi usiku Yan Muda hautoshi kabisa ila sisi saa MBILI kamili tumeshalala zamani tunakoromaš¤
Kiufupi Ni kwamba Ukiwa Umepanga mikakati yako vizuri Muda hautoshi kabisa Yan Muda Ni mchache Sana utakuja kuona unawexa ukawa unalala saa Saba usiku kila Siku
No way inawezekana huelewi ulale saa 7muda wote unafanya Nini tafuta Ndoto yako Tena iwe kubwa ya kukuzidi halafu jiapie baada ya Miaka 5lazima niitimize Hapo lazima Muda usitoshe
Usilizike na muda wa Masaa 24ukalala ukawa unaona Muda Ni mwingi
Tumia Muda vizuri K**a wazungu ili na wew ujibadilishie taswira upo Tanzania lakini Unamuda wa marekaniš¤£
*grow wise*
28/09/2024
WEKEZA KWENYE KUJIFUNZA
Siku moja Wakati nimeamua rasmi kuwa mwanauchumi haikuwa rahisi kwangu nilitumia Muda mwingi Sana kuwaza biashara ya kufanya
Na kweli nilianzisha na ilienda lakini baada ya Muda biashara ile ilikufa Hivi unaweza kujua Ni kwanini nilianzisha biashara zilikufa
Nilifanikiwa kuwaza biashara nyingi lakini katika hizo nyingi mbili nilifanikiwa kuzifungua na kuziendesha niligundua kuwa nahitaji Muda mwingi Kujifunza hasa kwa
Walionitangulia
Walionizidi
Waliochini yangu
Na ninaolingana nao
Nikiwa na imani kubwa Sana kwamba mtu aliyekutangulia anauwezo mkubwa Sana kwan anaweza kukifahamisha vitu vingi Sana
Wakati natafakari Mambo mengi niligundua K**a wew Unahitaji kufanikiwa Ni lazima uwekeze Muda mwingi kwenye Kujifunza hasa kwa watu wa uchumi nakuhakikishia kafanikiwa
Na kuelekeza watu watakao kufundisha zaidi kuhusu wew kupiga hatua Kwan mm wamenisaidia Sana
1. Joel Nanauka
2. Dactariwamauzo
Ni Watu Ambao nimetumia nguvu kubwa Sana kuwasikiliza na hata kusoma vitabu vyake(Joel Nanauka)
Ukijifunza Kuna maarifa yatakuingia zaidi na utajua na namna ya kuendesha Mambo
Hata neno la Mungu linasema watu wangu wanaangamia kwa Kukosa maarifa
Usikubali kuangamia jaribu kutafuta maarifa kwa namna yyte ile
Wakati Unahitaji kufanikiwa kuwa tayar Kujifunza
growwiseāš½
27/09/2024
UNAHISI KUFIKA MWISHO?
Hili ni Swali kwako wewe?
Kuna Muda ushawahi kuhisi huwezi Kuendelea kabisa na hata Ukitaka Kuendelea huoni pa kuanzia mwisho wa Siku Unahisi nimefika mwisho wa mawazo yangu
Unaweza ukawa umeshafanya biashara zaidi ya mbili lakini zinafel(Huu Ni mfano wangu kabisaš¤£)
Na inawezekana umetafuta ajira kwenye maofisi ya watu lakini Umeshindwa ukahisi labda Mimi ndo nimeubwa Hivi hebu ngoja nisubiri kuolewa tuš¤
Unajua option ya kuolewa bwana(nifatilie kwenye nakala yangu nitakwambia majukumu ya mke katika uchumi wa familia)
Anyway tuendelee usikubali kabisa kufika mwisho kumbuka hata waliofanikiwa walifeli Sana lakini mwisho wa Siku waliofanikiwa kwahiyo usikubali kufika mwisho
Ukihisi kufel tafuta vitabu tafuta watu wanaoweza kukunyanyua kimawazo ukawapigia nakwambia Kuna hatua lazima upige
Kuna dada mmoja alifilisika ikafika hatua akataka kujiua lakini aliponishirikisha nilimtia moyo sana na aliamka Tena
Amka tena kwanza kukata tamaa Ni Dhambi kiimani
Ukihisi kufika mwisho fikiria ukiishia hapo Ndoto zako utazitimizaje?
Amka amsha Ndoto zako Kwani maisha yako ya mbele Ni mazuri sana
Haloo usihisi kufika mwisho kabisaāš½
27/09/2024
UNAIKUMBUKA NDOTO YAKO WAKATI UPO MDOGO
Siku moja Nilikuwa nazungumza na Coach wangu Mr Elia sereka na alisema Kila mtu ndoto yake Ni ile aliyokuwa anaipenda kuifanya Sana Wakati mdogo
Chukua dakika 2 kukumbuka Nini Ulikuwa unapenda kufanya Wakati mdogo.......
Ouky Hicho Hicho wengine tayar wameshapotea njia kabisa ila najua wengine walipenda kuunda watoto kwa udongo ama gari ama kutengeneza nyumba kubwa Sana n.k
Hivi Unafahamu hii Ndoto Ni ya kwel na inaishi K**a Utaamua kuiamsha
Wazungu huangalia Ndoto za watoto wao wakiwa wadogo na hufanya kuwasaidia tu kutimiza zile Ndoto
Hata wewe bado hukachelewa unanafasi ya kujenga ile nyumba ya kifahari uliyokuwa unaitengeneza nikwambie tu unanafasi ya kununua gari lako lile ulilokuwa unalitengeneza Ni wew tu kuamua kuamsha ile ndoto
Na utqiamshaje Ni kwa maamuzi yako ya Leo ya kuanza kufanya vitu vya maendeleo ili uweze kuitimiza ile ndoto
grow wise
27/09/2024
UTAWEZAJE KUISHI BILA AJIRA
Haya Kuna mtu ananiambia mimi sitaki kazi ama biashara ninachohitaji Ni AJIRA tu
Ukweli Unaouma Ni kwamba
Sasa ivi AJIRA zimekuwa ngumu Sana si serikalini wala kwenye Mashirika binafsi
Unajua kwaniniš¤
Wasomi wamekuwa wengi Sana na makampuni ama ofisi zimekuwa chache
Hatuwezi kubanana wote hukoš¤£
Ouk ukikaa kwa dakika tano ukiwa bafuni unaoga ndo utagundua hichi ninachokiongea
Licha ya ukosefu huo wa ajira haina maana tuishi bila hela ila inatubidi tupambane kwa kutafuta kazi ya kufanya itakayotuongizia kipato Cha Kila Siku
Kuna Siku nilifikiria kuhusu Elimu yangu nilitamani nizimie kwa Nusu saa𤣠story hii nitakuletea endelea kunifatulia
Tuendelee hivyo Tukikwambia Kuhusu Kushikiria Fursa za Kazi tunazokuambia Hebu elewa Usisubiri mpka yakufike shingoni maisha yako Yawe magumu Wakati Unauwezo wa Kuyabadilisha leo
Wekeza Sana Kwenye Kujifunza endlea kunifatulia ili siku ukiamua kuanza usirudi nyuma Ni kuanza tu na mimi ninampango wa kukusindikiza kuyafikia Yale uliyoyaota Wakati upo mdogoāš½
27/09/2024
*UTOFAUTI WA WATU KATIKA KUYACHUKULIA MAMBO*
Katika fursa hii ya kazi niliyoitangaza Kuna watu Wengi wamenifata na watu Hawa wanatofautiana katika ufatiliaji wa Mambo
Hii hutegemea na uhitaji wa mtu pamoja na Fikra za mtu
K**a mtu ameweza Kutafuta kazi kwa muda mrefu na anashauku ya Mafanikio na mtu akamwambia katika hili utafanikiwa Ni lazima ajaribu ili aweze kafanikiwa
Lakini ambaye bado Hana Ndoto za kafanikiwa HAFAHAMU umuhimu wa ndoto na kufanya kazi kwa makini ili afanikiwe atachukulia hili kawaida Sana na atapotezea ataona K**a alipotezewa Muda
Jambo hili linajulikana kwa watu Hawa wawili tofauti
Hakika Hawa Ni watu wawili tofauti kwanzia mitazamo Yao,Ndoto zao na shauku zao
Unahisi wewe upo upande gani kwenye Hawa watu wawiliš¤
Najua utasema wew unandoto
Hebu Niandikie Ndoto yako kubwa kwenye maisha yako Ni niniš¤
Hivi hujatumia dakika 10 kwelš¤£
Ouky endelea kunifatulia ili Siku moja uje ushirikiane na Mimi kutimiza Ndoto zako
14/08/2024
Usitumie Nguvu Kubwa sana Kujilinganisha na watuā
Ila tumia Nguvu Kubwa sana Kuwekeza nguvu,Muda na Pesa Zako kwenye Kutafuta Mafanikio yako
Kiufupi Mafanikio yapo ila ni wew hujaamua kuyatafuta Mafanikio hivyo weka nguvu na muda na pesa pia Kuwekeza Mafanikio yako ya Mbeleni
Jitahidi kutazama maisha ya badae
Kumbuka Maisha yako yanakuhitaji wew kwa asilimia Mia moja
*Ujumbe Muhimu Kwa Wanawake Wote*
Wanawake wengi wamekuwa Wakisumbuliwa na Changamoto za Uchumi Ikiwemo
āKUSHINDWA KUJISIMAMIA
āKUISHIA NJIANI KWENYE BIASHARA
āKUTOKUONA FAIDA KATIKA BIASHARA
āKUKOSA MUONGOZO
KUTOKA KWA MZOEFU WA BIASHARA
āKUKOSA USHAURI WA KUENDESHA BIASHARA
K**a Wewe ni Mmoja Wao Ningependa Kuongea na Wewe
Kwa Jina Naitwa *LORUHAMA ROBERT*
Ninawasaidia Wanawake Kusimama na Kuendesha Biashara yake Itakayo saidia Kumuinua Kiuchumi na Kuondokana na Tegemezi
Nimejikita kwenye Kusimamia na Kuonesha njia sahihi ya Kupita Ili Kuhakikisha unafanikiwa
Wiki hii Nataka Niandae darasa la Bure la Namna ya Kukuza na Kusimamia biashara Yako chini Ya Usimamizi wangu
K**a Utapenda Kuhudhuria Darasa Hilo
Naomba Ubonyeze Kitufe Cha WHATSAPP Hapo Chini
Kisha Nitawasiliana Na Wewe ilituzungumze na Kukuandalia Wewe Pamoja Na Wanawake Wenzako Darasa bure Kabisa Kupitia Group La WHATSAPP.
Bonyeza Kitufe Cha WhatsApp Hapo Chini, Kabla Ya Darasa Letu Kujaa
Ni Mimi Mwenye Kujali kipato chako,
Loruhama Robert
Mkurugenzi, Amsha Ndoto Zako
27/07/2024
Soma hizi Caption kwa umakini kuna kitu utajifunza
27/07/2024
Soma Hizi Caption kwa umakini kuna Kitu Utakipata
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Dodoma
Dodoma