Eat Right to Loose Weight
Tunawasaidia watu mbalimbali jinsi ya kula vizuri kuweza kuulinda muonekano wako na kuondokana na ny
28/12/2019
JAMBO MUHIMU KABLA YA KUANZA KUREKEBISHA MUONEKANO
Kabla ya kujua jambo lenyewe, napenda nikumbushe jambo lingine. Ili kurekebisha vizuri muonekano, na kwamba chakula kipi ni bora na kipi sio,ni vyema na ni muhimu kujua muonekano wa sasa uliupatikana kwa sababu zipi kati ya ulaji usiofaa, kutofanya mazoezi au mtindo wa sasa wa maisha.
Hivyo kabla ya kuanzia safari hii inayo tatiza wengi ni vizuri kuifahamu sababu halisi iliyosababaisha na kisha zoezi litakuwa rahisi.
Haya jambo lenyewe ni kufanya yafuatayo kwanza:-
- Fahamu uwiano wa uzito katika kilogramu na urefu katika mita za mraba yaani BMI (body mass index)
- Baada ya kujua uzito wako gawanya kwa urefu wako wakati tayari urefu huo ukiwa umeuzidishwa wenyewe kwa wenyewe, mfano 80÷(1.7×1.7)
Majibu yatakayopatika yanamaanisha yafuatayo:-
▪︎Chini ya 16.0 ~ hii inaonesha utapiamlo mkali, kiasi cha chakula kiongezwe na uchunguzi wa kiafya ufanyike.
▪︎ 16.0 - 18.4 ~ hii inaonesha utapiamlo wa kadiri, kiasi cha chakula kiongezwe na uchunguzi wa kiafya ufanyike.
▪︎ 18.5 - 24.9 ~ hali nzuri ya lishe na ni vizuri okazaki hivyo.
▪︎25.0 - 29.9 ~ uzito uliozidi (overweight), tahadhali ichukuliwe.
▪︎30.0 - 34.9 ~ uzito uliozidi (obesity type I), hatua za kupungua zichukuliwe.
▪︎35.0 - 39.9 ~ uzito uliozidi (obesity type II), hatua za kupungua zichukuliwe.
▪︎40.0 na zaidi ~ uzito uliozidi (obesity type III), hatua za kupungua zichukuliwe haraka katika hatua hii hatari inazidi kuwa kubwa.
Yakizingatwa haya ni rahisi kuepukana na magonjwa sugu yasiyo ambukiza sababu chanzo cha magonjwa hayo ni muonekano mkubwa kupita kiasi.
Tuonane katika somo linalofuata.🚶♂️🚶♀️🙋♀️
05/05/2019
DUMISHA UZITO WA KAWAIDA WENYE AFYA
• Unapaswa kufahamu ya kwamba unapokula zaidi unazidisha kile mwili wako unahitaji.
• Unapokula zaidi na haufanyi mazoezi yoyote, unaweza kupata uzito au unene uliozidi
• Kuwa na uzito wa kawaida ni muhimu kwako na pia ni muhimu kula chakula bora kwa kiasi.
Kudumisha uzito unaofaa, zingatia yafuatayo:-
- Punguza kiasi cha mafuta na sukari unachokula
- Punguza kiasi cha chakula unachojiwekea katika sahani
- Acha kula tu mradi ushibe
- Ongeza kufanya mazoezi
Ukidumisha uzito wako itakusaidia kuepukana na:-
- kuumwa viungo vya mwili
- kupata shinikizi la juu la damu
- ugonjwa wa sukari
- ugonjwa wa moyo
- ugonjwa wa saratani.
'Comment' namba yako ili kujua ule au utumie nini ili kudumisha uzito wako.
31/03/2019
Are you a breastfeeding mum and want to loose weight?
Hello helloo my friends anywhere you are. Hope you're doing great.
Normally, a breastfeeding mum grows big because she eats more than normal as she always want her baby to be healthier more and not with malnutrition. So due to this situation they become overweight.
And so they don't look good as they were before pregnancy.
So if you are a mum and you want to loose that baby weight safely but also healthier you are very much welcomed for more details.
Vijue vyakula ambavyo hutakiwi kula k**a unataka kupunguza uzito na kutambi
Miongoni mwa changamoto kubwa inayowakumba watu siku za hivi karibuni ni katika upatikanaji wa chakula, matumizi yake na namna ya kudhibiti ili kutoleta athari katika mwili. Kwa hivo leo napenda kukushirikisha aina za vyakula vya kupunguza au kuacha kula kabisa k**a unataka kupunguza uzito wa mwili wako.
*Chipsi.* Kwa wakazi wengi wa sehemu za mijini hupedelea sana chips. Pamoja na radha yake nzuri, lakini ni mojawapo ya chakula kinacho sababisha ongezeko la kasi la mwili. Na hii ni kutokana na upatikanaji wake kuwa ni wa urahisi karibu kwenye kila maeneo wanayoishi watu. Kwa mujibu wa tafiti, chakula hiki kinaongeza uzito mwilini kutokana na kuwa na kalori nyingi ndani yake na ni rahisi kuzila nyingi zaidi kwa mpigo.
Tafiti pia zinaendelea kwa kuelezea kuwa chipsi pengine ndiyo chakula kinachochangia kuongeza uzito kuliko chakula chochote. Hivyo basi, kwa afya yako unashauriwa kuvichemsha kwa maji na kula badala ya kukaanga.
Hadi wakati meingine
28/01/2019
HELLOOOOO!
JE, UMEKUWA UKISUMBUKA KUPUNGUZA UZITO NA KITAMBI?
Ipo dhana iliyojengeka kuwa UNENE ni kiashiria cha hali nzuri ya maisha au kuashiria kuwa mtu huyu ana pesa.
Ikumbukwe kuwa UNENE uliopitiliza unaweza kupelekea mtu kupata matatizo ya kiafya k**a KISUKARI, SHINIKIZO LA DAMU, KIHARUSI, UGONJWA WA MOYO, SARATANI AU MAFUTA MABAYA MWILINI.
UFANYE NINI?
Zingatia yafuatayo:-
- Jitahidi kula vyakula vyenye nishati kidogo
- Pendelea vyakula vyenye nyuzinyuzi
- Kunywa maji ya kutosha, safi na salama
- Punguza vyakula vyenye mafuta mengi
- Punguza vyakula na vinywaji vilivyoongezwa sukari
- Kula mbogamboga na matunda kwa wingi
- Fanya mazoezi ya kutosha
Kesho nitaendelea mazoezi gani ufanye lakini pia ni vyakula gani hasa ule ili uweze kupungua au kuondoa kitambi.
K**a umependa somo letu la leo bofya alama ya love au toa maoni.
Karibuni.
27/01/2019
Je, umehangaika na uzito mkubwa na kitambi?
K**a wewe umekuwa ukihangaika kwa muda mrefu, ni kwa jinsi gani unaweza kuondoa kitambi na kupunguza uzito. Basi fuatilia page hii kwa mafunzo ya bure ya jinsi ya kupunguza uzito na kuondoa kitambi kwa njia rahisi sana.
Kikubwa unachotakiwa kufanya ni kuzingatia mwongozo wa mazoezi na chakula.
Lakini pia unatakiwa kujijia mwenyewe kwamba ni tabia gani ambazo mbaya zinazo kusababishia wewe kuongezeka uzito.
Inaweza kuwa ni kutojishughulisha, kutofanya mazoezi au kula vibaya bila kuzingatia ulaji bora.
Karibu katika page hii uweze kupata msaada wa namna bora na kupunguza uzito na kitambi kisicho furahisha.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Dodoma