Ayo Habari
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Ayo Habari, Health/Beauty, Kisukuru, Kigamboni.
06/03/2022
Korea Kaskazini imefanya jaribio jingine la kombora leo Jumapili kwa ajili ya kuthibitisha hatua iliyofikiwa katika uimarishwaji wa mfumo wa upelelezi wa kutumia satelaiti, jana pia Korea Kasakzini ilifanya jaribio la kombora na hii inafanya makombora yaliyojaribiwa na Nchi hiyo ndani ya mwaka huu pekee kufikia kumi.
Marekani, Japan na Korea Kaskazini wamelaani majaribio hayo wakihofu kuwa huenda Korea Kaskazini inajiandaa kufanya jaribo ambalo litavuruga amani.
03/03/2022
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepiga kura kwa wingi ya kuunga mkono azimio la kuitaka Urusi kusimamisha mara moja mashambulizi nchini Ukraine na kuyaondoa majeshi yake yote, Mataifa 141 yameunga mkono azimio hilo dhidi ya matano ambayo yamepinga, kura hiyo iliyoitwa uvamizi dhidi ya Ukraine ilipigwa katika kikao cha dharura cha UNGA.
Urusi imeungwa mkono na Belarus, Syria, Korea Kaskazini na Eritrea, dalili inayoashiria namna Taifa hilo lilivyotengwa kimataifa.
Katibu Mkuu wa Umoja huo Antonio Gutteres amesema ujumbe wa UNGA uko wazi na Urusi inatakiwa kusimamisha mashambulizi hayo na kufungua milango ya mazungumzo na diplomasia.
Kwenye kura hizo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Uganda zipo kwenye orodha ya Nchi 34 ambazo zimejizuia kupiga kura kwenye upande wowote, huku Kenya ikiunga mkono Ukraine na kutaka Urusi iondoke Ukraine.
03/03/2022
Millard Ayo, [3/2/22, 7:36 PM]
[Photo]
Manchester Derby...... Mchongo! Kutoka
Kupitia ofa ya Panda tukupandishe wewe mteja wa Bomba Panda sasa na lipia kifurushi cha Shangwe 31,000/= tukupandishe mpaka Compact bila malipo ya ziada utape kufurahia mechi hii Live.
*Vigezo na Masharti Kuzingatiwa *
Millard Ayo, [3/2/22, 9:59 PM]
Bilionea ambaye ni Mmiliki wa Club ya Chelsea ya England Roman Abromavich amethibitisha kuwa anataka kuiuza club hiyo ambapo anafanya hivi kwa maslahi mapana ya Club, Wadhamini na Wafanyakazi wa Club.
“Ningependa kutoa taarifa kuhusiana na tetesi zinazoendelea kwenye vyombo vya habari kuhusiana na umiliki wangu Chelsea, siku zote nimekuwa nikifanya maamuzi kwa sababu ya maslahi ya club, kwa hali inavyoendelea sasa nimeamua kuiuza club” ——— Roman Abromavich.
Roman aliinunua club hiyo 2003 kwa pound milioni 140 (Tsh Bilioni 433) na sasa ameamua kuiuza baada ya vita ya Ukraine kuisababishia Russia na Wawekezaji wake kuwekewa vikwazo au biashara zao kusitishwa sehemu mbalimbali.
Kwa mujibu wa Forbes Chelsea sasa ina thamani ya pound Bilioni 2.4 (Tsh Trilioni 7.4).
Roman katika taarifa iliyotolewa na Chelsea anasema atauza club hiyo na pesa zote alizouza zitaenda katika mfuko maalum wa kusaidia Waathirika wa vita nchini Ukraine na wala hana lengo la kujipatia faida.
03/03/2022
Urusi inadai imeudhibiti kabisa Mji wa Kherson nchini Ukraine, huu utakuwa ni Mji wa kwanza kudhibitiwa na Urusi tangu uvamizi wake ulipoanza nchini humo.
Wakati huohuo Wanajeshi wa Urusi wamewasili katika Mji wa Kharkiv, Mji wa pili kwa ukubwa wa Ukraine, Rais wa Ukraine Volodymir Zelensksy ameikosoa hatua ya Urusi kuishambulia Miji yenye idadi kubwa ya Watu akiitaja kuwa ni kampeni ya ugaidi.
Rais Zelensky amesema hakuna atakayesamehe wala kusahau umwagaji damu katika uwanja wa Kharkiv na shambulizi la bomu dhidi ya mnara wa televisheni katika mji mkuu Kiev, ambalo ameliita kuwa ni kitendo cha ugaidi na uhalifu wa kivita.
Mashambulizi katika Mji wa Kharkiv yameendelea leo huku Urusi ikikishambulia kituo cha polisi na makao makuu ya idara ya ujasusi, Idara ya kitaifa ya huduma za dharura ya Ukraine imeripoti kuwa watu watatu wamejeruhiwa katika hujuma hiyo, wakati hayo yakijiri Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez ameliambia Bunge leo kwamba Nchi yake itatuma silaha Ukraine.
02/03/2022
"Serikali haijalipia kuweka tangazo la Tanzania katika jengo refu kuliko yote Duniani liitwalo Burj Khalifa lililopo katika Jiji la Dubai, tangazo hilo limewekwa kwa lengo la kuitangaza Tanzania kutokana na uhusiano mzuri uliopo kati ya Nchi yetu na Umoja wa Falme za Kiarabu"
"Utawala wa Dubai umeweka tangazo hilo kwa kutambua ziara ambayo Rais Samia Suluhu Hassan ameifanya Dubai na umeahidi kuendelea kuitangaza Tanzania kupitia jengo hilo maarufu" ——— Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa
02/03/2022
Mtandao wa Instagram umefungia akaunti za Chombo cha Habari cha Urusi cha RT katika Nchi zote Wanachama wa EU baada ya kupokea taarifa kutoka Serikali za Nchi hizo zikidai Chombo hicho kinaeneza propaganda kuhusu mzozo wa Urusi na Ukraine.
Ufungiwaji huo unakuja baada ya Facebook na Youtube pia kukifungia Chombo hicho.
02/03/2022
Meli ya mizigo iitwayo Felicity Ace iliyokuwa imebeba maelfu ya magari ya kifahari imezama katika visiwa vya Ureno vya Azores karibu wiki mbili baada ya kushika moto ilikuwa ikisafirisha magari ya kifahari 4,000 yakiwemo aina ya Porsches na Bentleys.
Meli hiyo ilikuwa njiani kuelekea Rhode Island nchini Marekani kutoka bandari ya Ujerumani ya Emden wakati moto ulipozuka, Wahudumu wote wa meli hiyo waliokolewa wakati moto huo ulipoanza Februari 16.
Joao Mendes Cabecas, Nahodha mmoja ya bandari iliyo karibu katika kisiwa cha Faial, amesema hakuna uvujaji wa mafuta ulioripotiwa hadi sasa lakini alisema kuna hofu kwamba matenki ya mafuta yanaweza kuharibika wakati chombo hicho kikiwa chini ya bahari ya Atlantic katika kina cha mita 3,500 (maili 2.17).
01/03/2022
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta hapa nchini ambapo bei za rejareja na jumla za mafuta ya petrol, dizeli na mafuta ya taa yaliyopokelewa kupitia Bandari ya Dar es salaam zimebadilika ikilinganishwa na toleo lililopita la February 2 2022 ambapo kwa mwezi March bei za rejareja za petroli na dizeli zimeongezeka kwa Tsh. 60 kwa Lita ( sawa na 2.42%) na Tsh. 65 kwa lita (sawa na 2.77%) na mafuta ya taa imepungua kwa Tsh. 83 kwa lita (sawa na 3.63%).
EWURA imesema kuwa bei hizi zingeweza kuwa juu zaidi k**a Serikali isingechukua hatua ya kuahirisha tozo ya Tsh. 100 kwa lita kwenye bidhaa za mafuta ya petrol, dizeli na mafuta ya taa.
"Kwa March 2022 bei za jumla na rejareja kwa mikoa ya Kaskazini (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara) zimeongezeka ikilinganishwa na bei zilizotolewa February 02, 2022, kwa March bei za rejareja za petroli na dizeli zimeongezeka kwa Tsh. 165/lita (sawa na 6.88% ) na Tsh. 207 kwa lita (sawa na 9.09% )
Imeelezwa kuwa mabadiilko haya ya bei yanachangiwa na kubadilika kwa bei za mafuta katika Soko la Dunia, gharama za usafirishaji na thamani ya shilingi ukilinganisha na dola ya Kimarekani.
01/03/2022
DC wa Kinondoni, Godwin Gondwe amevunja Uongozi wa Vijana wanaofanya shughuli zao kwenye Fukwe za Coco (Beach Boys) kufuatia vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia vinavyodaiwa kufanywa na Vijana hao kwa Wanawake wakaokwenda kuogelea ambapo hujifanya wanawasaidia kuogelea na wakiwafikisha kwenye maji mengi huwalazimisha kufanya nao mapenzi (kubrashi) na kuwatishia kuwa wakikataa watawaacha wafie majini.
DC Gondwe amechukua hatua hiyo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Raia wema na Wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao Coco Beach huku akisema malalamiko hayo yamemfikia wakati mwafaka hasa ukizingatia kuwa tunaelekea kwenye kilele cha Siku ya Wanawake na mwaka mmoja madarakani wa Rais Samia March 19,2022 "Hatuwezi kuwaacha Mama zetu, Dada zetu, Wadogo zetu wa k**e wananyayasika"
DC Gondwe pia ametoa maelekezo kwa Polisi na Vyombo vingine kuchukua hatua haraka kwa wote wanaohusika na matukio hayo huku akitoa siku tatu kwa uchaguzi mpya wa Viongozi wapya ufanyike "Naagiza pia maboya ya kuogelea yasajiliwe na Wanaowasindikiza Watu kuogelea wajulikane ili kuepusha uhuni huu"
(📹 via )
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Kisukuru
Kigamboni