Afya yangu leo

Afya yangu leo

Share

19/05/2021

Hi

Photos from Afya yangu leo's post 07/12/2020

UUJUE UGONJWA WA INI

Ini ni kiungo laini sana na kinafanya kazi kubwa sana mwilini ya kuchuja sumu na damu na kuondoa sumu kutoka kwenye mmeng’enyo wa chakula ili kiende mwilini kufanya kazi.

Ini lina uzito wa kilo 1.6 Inapimwa kwa wastani, k**a sentimita 8 kwa usawa (kote), na sentimita 6.5 kwa wima (chini), na ni sentimita 4.5 kwa unene.

Kuna aina nyingi tofauti za ugonjwa wa ini. Lakini haijalishi una aina gani, uharibifu wa ini lako unakuwa sawa kwa kuwa unaathiri ini na kulifanya lisifanye kazi yake, pia tatizo linaweza kusonga mbele kwa njia hiyo hiyo.

Ikiwa ini lako limeambukizwa na virusi, limejeruhiwa na kemikali (sumu), au linashambuliwa na mfumo wako wa kinga, hatari ya msingi ni sawa kwa wote kwa sababu yote huzoofisha ini – kwamba ini lako litaharibiwa sana hivyo ini haliwezi kufanya kazi ya kukuweka kwenye uhai.

AINA ZA MAGONJWA YA INI

Kuna aina mbalimbali za magonjwa ya ini, nazo ni

Ugonjwa wa ini unaotokana na Virusi k**a..
•Hepatitis A,
•Hepatitis B,
•Hepatitis C
•Ugonjwa wa ini unaotokana na Madawa, Sumu (kemikali), na matumizi makubwa ya vilevi na sigara. Kwa mfano ugonjwa wa Ini kuwa na mafuta (fatty liver disease) na cirrhosis.
•Kansa ya Ini (Liver cancer)
•Ugonjwa wa kurithi, k**a hemochromatosis na Wilson disease

CHANZO CHA MAGONJWA YA INI

Magonjwa ya Ini yanavyanzo mbalimbali ambavyo asilimia kubwa yanatokana na mitindo ya maisha.

•Matumizi ya vyakula au bidhaa zenye kemikali (Sumu).

•Matumizi makubwa ya vilezi na sigara

•Matumizi ya dawa zenye kemikali

•Virusi aina ya hepatitis A, hepatitis B, na hepatitis C

•Unene na uzito uliopitiliza (Obesity)

•Kwa Kurithi k**a hemochromatosis na Wilson disease

•Kuto kula au kunywa vitoa sumu mwilini k**a maji na vingine

•Tatoo au kutoboa mwili

HATUA ZA MAGONJWA YA INI

Zipo hatua kadhaa za Ugonjwa ya ini

√Kuvimba. Katika hatua hii ya mapema, ini hupanuka au kuvimba.

√Fibrosis. Tishu nyepesi huanza kuchukua nafasi ya tishu zenye afya kwenye ini iliyochomwa.

√Cirrhosis. Kuporomoka kwa nguvu kumejengwa, na kuifanya tishu iwe ngumu kwa ini kufanya kazi vizuri.

√Ugonjwa wa ini wa hatua ya mwisho (ESLD). Kazi ya ini imezorota hadi kiwango ambacho uharibifu hauwezi kugeuzwa isipokuwa na kupandikiza ini.

√Saratani ya ini. Kukuza na kuzidisha kwa seli zisizo na afya kwenye ini zinaweza kutokea katika hatua yoyote ya kushindwa kwa ini, ingawa watu walio na ugonjwa wa cirrhosis wako kwenye hatari zaidi.

DALILI ZA MAGONJWA YA INI

Aina nyingi za ugonjwa wa ini hazioneshi dalili yoyote katika hatua za mwanzo. Mara tu unapoanza kupata dalili za ugonjwa wa ini, ini lako tayari linakuwa limeharibiwa. Hii inajulikana k**a cirrhosis

•Kujisikia kuchoka na mdhaifu mda mwingi
Kukosa hamu ya kula – hupelekea kupungua uzito

•Kichefuchefu au kutapika hadi kutapika damu

•Maumivu ya tumbo hasa katika eneo la kati la upande wa ini.

•Pia kuvimba sehemu ya ini na miguu.

•Ngozi kuwa ya manjano na weupe wa macho makavu(jaundice)

•Kukosa usingizi na kupumua kiwepesi

•Kasi ya mapigo ya moyo kuongezeka

•Kupoteza uwezo wa tendo la ndoa

•Kupoteza kumbukumbu

•Maumivu katika bega la kulia

•Rangi ya Mkojo na kinyesi kuwa nyeusi

•Damu kutoka puani

JINSI YA KUEPUKANA NA UGONJWA WA INI

Punguza (balansi) kiwango cha lehemu (choresterol)

Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali

Lala vizuri kwa muda mzuri – masaa 7 hadi 9

Punguza Matumizi ya vyakula au bidhaa zenye kemikali (Sumu).

Punguza au Acha Matumizi makubwa ya vilezi na sigara

Punguza Matumizi ya dawa zenye kemikali

Tumia vyakula na vinywaji vinavyoondoa taka na sumu mwilini (Detoxifying Agent)

Punguza Unene na uzito uliopitiliza (Obesity)

Usichore Tatoo au kutoboa mwili ovyo

Fanya mazoezi – Angalau dakika 30 kwa siku
Usile vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi

Tiba juu ya ugonjwa wa homa ya Ini inategemea na hali ya ugonjwa ulipofika......
Pure and Brocken Gannodema spores
Refined Yunzhi essence
Reish...
Novel depile ...

Mawasiliano

Call/messege 0743889821
Whatsap 0743889821

04/12/2020

HOMONAL IMBALANCE (KUVURUGIKA KWA HOMONI

:Hili ni tatizo linalowakumba wakina mama(wanawake) wengi ambalo husababishwa na kiwango kidogo cha hormone ya ESTROGEN.

VYANZO VYA KUVURUGIKA KWA HORMONE

👉Utoaji wa mimba
👉Uwepo wa sumu mwilini.
👉kutokula mlo uliokamili au mfumo mbovu wa maisha.
👉Family history(upungufu wa ongezeko ya homoni ya progesterone
👉mabadiliko ya mazingira au hali ya hewa.
👉uzito mkubwa
👉Msongo wa mawazo.
👉Kutofanya mazoezi.
👉Matumizi ya kisasa ya uzazi wa mpango.
👉Kukoma kwa hedhi.

Dalili za kuvurugika kwa homoni

👉Maumivu wakati wa tendo LA ndoa.
👉Kutoshika mimba.
👉Mzunguko wa hedhi kubadilika.
👉Kuongezeka uzito.
👉Kupungua hamu ya tendo LA ndoa.
👉Kupoteza kumbukumbu.
👉Hasira za Mara kwa Mara.
👉Damu kutoka nyingi wakati wa hedhi au kutoa damu yenye mabongemabonge
👉Uke kuwa mkavu.
👉kutoka jasho jingi usiku.
👉maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi
👉mzio wa vyakula/Allerg kuchaguachagua vyakula.

Madhara ya kuvurugika kwa homoni
👉kutoshika ujauzito kwa mda mrefu.
👉Mimba kuharibika Mara kwa Mara.
👉Kuwa mgumba.
👉U.t.I Mara kwa Mara.
👉Uvimbe kwenye via vya uzazi wa mwanamke.(fibroids)
👉kuziba kwa mirija ya uzazi.
👉saratani.

Hormone imbalance inatibika na

Refined Yunzh caps
Zaminacal caps
Femicare

By Dr haule

Follow me on whatsap 0743889821

Jali afya yako.

04/12/2020

HOMON IMBALANCE (KUVURUGIKA KWA HOMONI

:Hili ni tatizo linalowakumba wakina mama(wanawake) wengi ambalo husababishwa na kiwango kidogo cha hormone ya ESTROGEN.

VYANZO VYA KUVURUGIKA KWA HORMONE

👉Utoaji wa mimba
👉Uwepo wa sumu mwilini.
👉kutokula mlo uliokamili au mfumo mbovu wa maisha.
👉Family history(upungufu wa ongezeko ya homoni ya progesterone
👉mabadiliko ya mazingira au hali ya hewa.
👉uzito mkubwa
👉Msongo wa mawazo.
👉Kutofanya mazoezi.
👉Matumizi ya kisasa ya uzazi wa mpango.
👉Kukoma kwa hedhi.

Dalili za kuvurugika kwa homoni

👉Maumivu wakati wa tendo LA ndoa.
👉Kutoshika mimba.
👉Mzunguko wa hedhi kubadilika.
👉Kuongezeka uzito.
👉Kupungua hamu ya tendo LA ndoa.
👉Kupoteza kumbukumbu.
👉Hasira za Mara kwa Mara.
👉Damu kutoka nyingi wakati wa hedhi au kutoa damu yenye mabongemabonge
👉Uke kuwa mkavu.
👉kutoka jasho jingi usiku.
👉maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi
👉mzio wa vyakula/Allerg kuchaguachagua vyakula.

Madhara ya kuvurugika kwa homoni

👉kutoshika ujauzito kwa mda mrefu.
👉Mimba kuharibika Mara kwa Mara.
👉Kuwa mgumba.
👉U.t.I Mara kwa Mara.
👉Uvimbe kwenye via vya uzazi wa mwanamke.(fibroids)
👉kuziba kwa mirija ya uzazi.
👉saratani.

Hormone imbalance inatibika na

Zaminacal caps
Refined Yunzhi
Femicare..

Dozi ya miezi mitatu mfululizo...

By Dr haule

Jali afya yako.

08/10/2020

CHANZO, DALILI, TIBA NA MADHARA YA UGONJWA WA VIONDA VYA TUMBO (PUD)

Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya ukuta wa tumbo au utumbo wa binadamu.

Kwa kawaida tatizo hili huleta maumivu makali sana ya tumbo ingawa si lazima kila maumivu ayapatayo mgonjwa husababishwa na vidonda vya tumbo.

Tafiti zimeonesha kwamba karibu asilimia 70 mpaka 90 ya vidonda vya tumbo husababishwa na aina ya vimelea vya bakteria wajulikanao k**a Helicobacter pylori.

Aidha matumizi ya baadhi ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non Steroid Anti-inflamatory Drugs k**a aspirin au diclofenac huweza kusababisha au kuongeza uwezekano wa kupata ugonjwa huu.

Kuna dhana iliyozoeleka kuwa vidonda vya tumbo huathiri zaidi mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (stomach). Dhana hii si kweli kwani sehemu inayoathiriwa zaidi na tatizo hili ni sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo ijulikanayo k**a duodenum.

⛔Makundi ya PUD
Kuna makundi makuu yafuatayo ya ugonjwa huu

🍅Vidonda vinavyotokea kwenye mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (Gastric ulcers)
🍅Vidonda vinavyotokea kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (Duodenal Ulcers)
🍅Vidonda vinavyotokea kwenye koo (Oesophageal ulcers)
Vidonda vijulikanavyo k**a Merckel’s Diverticulum ulcers.
Visababishi vya PUD

⛔Vidonda vya tumbo husababishwa na

👉Maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori
Imeonekana kuwa zaidi ya asilimia 50 ya watu duniani wana vimelea hivi katika utumbo. Aidha, miongoni mwao, karibu asilimia 80 huwa hawaoneshi dalili yeyote ya kuugua ugonjwa wa vidonda vya tumbo.Aina hii ya vimelea vya bakteria husababisha karibu asilimia 60 ya vidonda vinavyotokea kwenye tumbo (gastric ulcers) na zaidi ya asilimia 90 ya duodenal ulcers.

Hali hii husababishwa zaidi na kushindwa kwa mfumo wa kinga mwilini kuwaua na kuwaondoa kabisa vimelea hawa ndani ya mwili. Matokeo ya kushindwa huku husababisha kuwepo kwa maambukizi ya kudumu katika kuta za tumbo (chronic active gastritis), maambukizi ambayo huharibu mfumo na uwezo wa kuta za tumbo kutunza homoni/kichocheo aina ya Gastrin, ambacho ni muhimu katika kuhakikisha mazingira ya tumbo yanakuwa na kiwango salama cha tindikali.

Kwa kawaida, kazi ya gastrin ni kuchochea utolewaji wa tindikali (gastric acid) kutoka kwenye seli za ukuta wa tumbo zijulikanazo k**a Parietal cells. Iwapo bakteria hawa watashambulia na kuharibu ukuta wa tumbo, mfumo wa gastrin pia uharibika, na hivyo kusababisha gastrin kuzalishwa kwa wingi hali ambayo pia huchochea uzalishaji wa gastric acid kwa wingi. Matokeo ya kuzalishwa kwa wingi kwa tindikali hii hupelekea kuchubuka kwa ukuta wa tumbo na hivyo kusababisha vidonda vya tumbo.

👉Matumizi ya muda mrefu ya dawa za kuondoa maumivu za kundi la NSAIDs
Ukuta wa utumbo hujilinda na madhara yatokanayo na tindikali ya utumbo (gastric acid) kwa kuwa na utando laini (mucus) ambao hutolewa na vichocheo vijulikavyo k**a Prostaglandins. Dawa hizi za kundi la NSAIDs huharibu mfumo wa kutengeza vichocheo hivi yaani prostaglandins na hivyo kufanya kuta za tumbo kukosa utando wa kuzilinda na mashambulizi ya tindikali hali ambayo hupelekea kutokea kwa vidonda vya tumbo.

👉Uvutaji wa sigara
Uvutaji sigara sambamba na maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo. Ifahamike tu kuwa uvutaji sigara pekee hausababishi vidonda vya tumbo.

👉Vyakula au viungo vya chakula vyenye uchachu
Kinyume na dhana iliyozoeleka miongoni mwa watu wengi, baadhi ya vyakula vyenye uchachu na upilipili k**a vile pilipili, ndimu, limao na masala havina uhusiano na uwezekano wa kupata vidonda vya tumbo.

👉Watu walio katika kundi la damu la O
Imeonekana pia kwamba kundi la damu lijulikanalo k**a blood group O, halina uhusiano wa kusababisha vidonda vya tumbo.

👉Unywaji wa pombe
Unywaji wa pombe pekee hausababishi vidonda vya tumbo. Hata hivyo, unywaji wa pombe sambamba na maambukizi ya vimelea vya Helicobacter pylori huongeza madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo.

👉Vitu vingine
Vitu vinavyohusishwa na uongezaji wa madhara ya vidonda vya tumbo ni pamoja na upasuaji wa tumbo (major abdominal surgeries), kuungua kwa moto (burns), ugonjwa wa figo; na kubadilishwa kwa viungo vya mwili k**a figo au ini.

⛔Dalili au viashiria vya PUD
🍅Maumivu makali au kiungulia maeneo ya chembe moyo (epigastic pains):Maumivu juu kidogo ya tumbo mara nyingi huendana na muda wa kula chakula. Mtu mwenye vidonda kwenye tumbo (gastric ulcers) hupata maumivu makali sana kipindi anapokula au mara tu baada ya kumaliza kula wakati aliye na vidonda kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenal ulcers) hupata maumivu makali anapokuwa na njaa na hupata nafuu pindi anapokula.

🍅Kuvimbiwa au tumbo kujaa gesi.
Hali hii pia yaweza kuendana na kubeua au kujamba mara kwa mara.
🍅Kucheua na kuongezeka kwa mate yanayoshuka tumboni baada ya kucheua.
🍅Kichefuchefu na kutapika
🍅Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito
🍅Kutapika damu
🍅Kupata haja kubwa ya rangi nyeusi au kahawia yenye harufu mbaya sana. Hii humaanisha mgonjwa anapata haja kubwa au choo kilichochanganyika na damu kwa mbali
👉Uwepo wa dalili k**a kiungulia cha muda mrefu, kucheua na kutapika baada ya kula na historia ya kutumia dawa za kupunguza maumivu (NSAIDs) kwa muda muda mrefu bila kufuata ushauri wa daktari ni ishara tosha ya kumfanya mgonjwa kumuona daktari kumpima na kumfanyia uchunguzi ili kujiridhisha kuwa hana tatizo la vidonda vya tumbo.

💊MATIBABU
Matibabu ya Ugonjwa wa vidonda vya tumbo
Habari nzuri ni kuwa ugonjwa huu wa vidonda vya tumbo unatibika. Hata hivyo tabia ya baadhi ya wagonjwa wengi kuacha kumalizia dawa au kutumia dawa chini ya kiwango tofauti na walivyoshauriwa na madaktari husababisha kujirudia kwa tatizo au kufanya tatizo kuwa sugu zaidi.

Madhara ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo
Uvujaji wa damu ndani ya utumbo: Hali hii yaweza kusababishwa na vidonda kuenea hadi kwenye mishipa ya damu na hivyo kufanya damu kuanza kuvuja. Hali hii ni hatari sana na inahitaji tiba ya dharura.

Vidonda vya tumbo huweza kusababisha tundu (kutoboka kwa ukuta wa tumbo) na kufanya vitu vilivyo ndani ya utumbo kutapakaa katika tumbo (abdomen) Hali hii huitwa peritonitis na ni hatari sana na inahitaji matibabu ya dharura.

Aidha, kuenea huko kunaweza pia kuathiri tezi kongosho na kusababisha madhara katika tezi hiyo, ugonjwa unaojulikana k**a pancreatitis.

Vidonda vya tumbo vinaweza pia kuenea na kuathiri pia viungo vya jirani k**a vile ini au kongosho (pancrease)

Kuvimba kwa kuta za tumbo pamoja na makovu yanayosababishwa na vidonda hivi huweza kusababisha kuziba kwa njia ya kupitishia chakula kutoka kwenye tumbo (stomach) kwenda sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo (duodenum) hali ambayo kitaalamu huitwa gastric outlet obstruction.

Iwapo vidonda vya tumbo vimesababishwa na H. pylori, kuna uwezekano wa kati ya mara tatu hadi ya sita ya mgonjwa kupata kansa ya tumbo (stomach cancer).

Tatizo la vidonda vya tumbo linatibiwa na ..
Tiba ya kudumu...
Probio 3

AntiDiarr

Consitrelax solution...

Call 0743889821

WhatsApp 0743889821

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Mbeya?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Mbeya