Urembo asilia na Biashara

Urembo asilia na Biashara

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Urembo asilia na Biashara, Health/Beauty, Mbeya.

13/09/2023

TIPS ZA KUTUNZA NYWELE

1️⃣fanya protein treatment angalau mara moja kwa mwezi

2️⃣kata ncha za nywele angalau mara 4 kwa mwaka..

3️⃣kula mlo kamili, ukuaji wa nywele unahitaji zaidi amino acid na protein hivyo kula vyakula unavyoweza pata virutubishi hivi k**a parachichi, karanga, yai, samaki, mbegu za maboga, mboga za majani n.k

4️⃣punguza matumizi ya blow drier, kukausha nywele kwa kutumia blow-dryer hufanya nywele kuwa kavu sana kwani hundoa unyevunyevu wote kwenye nywele hivyo ni rahisi kukatika

5️⃣usisuke nywele baada ya kubrow dry, baada ya kukausha nywele huwa kavu sana na ule mvutano wa kus**a hufanya nywele kuwa rahisi kukatika.
Unaweza s**a siku mbili au tatu baada ya kubrow dry ili uzipe muda nywele wa kufyonza mafuta uliyopaka na kurudisha unyevunyevu.

6️⃣usisuke style zinazovuta sana nywele(s**a protective hairstyles)

7️⃣kunywa maji ya kutosha husaidia kuzipa nywele na ngozi unyevunyevu

8️⃣ Tumia leave in conditioner baada ya kuosha huzifanya zibaki na unyevunyevu, kuchambuka, rahisi kuchana na kutokatika hovyo.

9️⃣Tumia chanuo lenye matundu makubwa

🔟Vaa kofia unavyotembea kwenye jua Kali ili kuilinda nywele dhidi ya miale ya jua au vumbi

1️⃣1️⃣Vaa kofia ya kitambaa cha saltine muda wa kulala, hii husaidia mafuta kwenye nywele yasinyonywe na mto hivyo kuzifanya zibaki na unyevunyevu

1️⃣2️⃣ Osha nywele kwa maji ya baridi au uvuguvugu ili kisaidia zisibaki kavu

1️⃣3️⃣ Chagua shampoo nzuri ambayo haina chemicals nyingi na inayosaidia kiziacha nywele na unyevunyevu

Photos from Urembo asilia na Biashara's post 20/05/2023

MAFUTA YA PARACHICHI (Avocado oil)

Ni mafuta yanayotengenezwa toka tunda la parachichi bila kupitishwa kwenye moto au jua. Yana kiwango kikubwa cha vitamin E ambayo inasaidia;
💦kuipa ngozi na kutunza unyevunyevu
💥inasaidia kulinda ngozi na miale ya jua
👌inasaidia kuondoa madoa ya chunusi
😉kuzuia makunyanzi

Pia mafuta haya yana kiwango kikubwa cha oleic acid ambayo inasaidia kulinda ngozi dhidi ya maambukuzi, matatizo ya ngozi na miale ya jua

MATUMIZI YA MAFUTA YA PARACHICHI
1. Yanatumika kwenye nywele na ngozi
2. kulainisha lips
3. kulainisha mikono au miguu
4. kufanya massage
5. kupikia
6. Yanatibu majeraha na makovu
7. Yanatibu na kurudisha ngozi iliyoharibika na viambata sumu au jua
8. yanatumika kuondoa make-up
9. yanaondoa weusi chini ya macho

Ni mazuri sana kuwapaka watoto kwenye ngozi na nywele

yanapatikana kwa ujazo wa ml 100 & 250
ml100 = 6000
ml 250= 10000
Pia kwa bei ya jumla kuanzia chupa 10
mob: 0746597150

Photos from Urembo asilia na Biashara's post 12/10/2020

*JINSI YA KUTUNZA NYWELE YENYE DAWA*

*Tuangalie vitu vya msingi vya kuzingatia ili uwe na nywele nzuri zenye dawa:*

1. Uchaguzi sahihi wa dawa (relaxer) inayoendana na aina ya Nywele yako.

2. Panga muda wa kuweka dawa hii inategemea na aina ya Nywele kwa wake wenye Nywele ngumu wanashauriwa kuweka Mara 3 kwa Mwaka yaani kila baada ya miezi 4. Na kwa wenye Nywele laini weka baada ya miezi sita.
Pia hakikisha dawa inawekwa kwenye Nywele iliyootea tu.

3. Fanya steaming baada ya wiki moja au mbili

4. Fanya protein treatment baada ya wiki 4 au 6

5. S**a mitindo ambayo haikati Nywele (protective hair style)

6. Hakikisha unaosha nywele zako mara kwa mara. Angalau mara 3 au nne kwa mwezi. Nywele zikijaa uchafu haziwezi kupumua vizuri hivyo zitakua kwa kusua sua sana.

7. Tumia mafuta rafiki na nywele zako. Mafuta yenye uwezo wa kutunza unywevu na kuzuia nywele kukatika. Mafuta hayo ni k**a vile Black castor oil, Coconut oil, Olive oil, jojoba oil nk

9. Punguza matumizi ya moto kwenye nywele.. Mfano .kupasi nywele au kukausha nywele na dryer. .Hii hufanya nywele kutokuwa na nguvu hivyo kuwa dhaifu sana hivyo unashauriwa usifanye mara kwa mara.

10. Tumia kofia ya satini au kitambaa cha safini wakati wa kulala , hii inasaidia nywele kufyonza mafuta ipasavyo na kumaintain Ph.

11. Kata ncha, hii husaidia kuzipa Nywele nafasi ya kukua vizuri na kuwa na muonekano mzuri

12. Tumia chanuo lenye uwazi mkubwa kuchana Nywele zako

13. Kula chakula bora na Maji ya kutosha

Photos from Urembo asilia na Biashara's post 16/06/2020

II. JINSI YA KUTUNZA NGOZI KAVU

Ngozi kavu husababishwa na vitu k**a;
*hali ya hewa kipindi cha baridi, hewa kukosa unyevunyevu hasa sehemu zenye ukame
* Joto, hasa maeneo yenye jua kali na hewa kavu
* kuoga maji ya moto kwa muda mrefu, tumia maji ya uvuguvugu kuoga
* matumizi ya sabuni yanayokausha mafuta au shampoo kwa mida mrefu
* Umri hasa kwanzia miaka 40

UTAJUAJE UNA NGOZI KAVU?
- ngozi ya uso kuvutika mara baada ya kuoga
- Ngozi kuuma
- ngozi kupas**a au kuwa na magamba
- Ngozi kubanduka
- Ngozi ya uso kutoa ungaunga

Zifuatazo ni njia za kutunza ngozi kavu;
1. Alovera, kata jani la Alovera kisha toa ute wake na upake usoni kaa dakika 20 kisha nawa.

2. Tumia mafuta ya jojoba, almond, n**i olive au mafuta ya vitamin E usiku. Nawa uso kisha paka mafuta kabla kulala ili kutunza unyevunyevu wa ngozi.

3. Ndizi mbivu na asali, saga ndizi mbivu kisha ongeza kijiko kimoja cha asali na kijiko kimoja cha mafuta ya olive changanya na upake usoni, Kaa dakika 20 kisha nawa. Husaidia kutunza unyevunyevu na kuondoa makunyanzi

4. Mdalasini na asali, changanya kijiko kimoja cha mdakasini na nusu kijiko cha asali paka usoni kaa dakika na unawe.

5. Mtindi na asali, maziwa mtindi yana madini ya zinc, vitamin B na lactic acid hivyo husaidia kuipa ngozi na kutunza unyevunyevu. Changanya robo kikombe cha maziwa mtindi na kijiko kimoja cha asali paka usoni kaa dakika 15 kisha unawe

6. Yai na olive oil, changanya kiini cha yai na kijiko kimoja cha mafuta ya olive kisha paka usoni kaa dakika 15 na unawe. Mafuta ya olive yana wingi wa vitamin E na ya vitamin A hivyo hufanya ngozi kuwa anga'vu na yenye afya . Tumia mchanganyiko huu mara mbili kwa wiki kupata matokeo mazuri

7. Parachichi na asali, changanya vijiko viwili vya parachichi lililosagwa na kijiko kimoja cha asali paka usoni kaa dakika10 kisha nawa na maji ya uvuguvugu.

ZINGATIA
1. Kunywa maji lita 2-3 kwa siku
2. Tumia moisturizer kabla kulala
3. Tumia mafuta au lotion yaliyotengenezwa kwa kutumia shea butter

24/05/2020
Photos from Urembo asilia na Biashara's post 22/05/2020

Photos from Urembo asilia na Biashara's post 07/05/2020

1. JINSI YA KUTUNZA NGOZI YENYE MAFUTA

Ngozi ya mafuta husababishwa na tezi ya ‘sebaceous’ inayozalisha mafuta zaidi ya kawaida. Pia umri, hali ya hewa hasa sehemu ya joto, ujauzito, lishe na uzito husababisha kuwa na ngozi ya mafuta usoni.
Zifuatazo ni mask au scrub ambazo mtu mwenye ngozi za mafuta anaweza kutumia kupunguza na kurekebisha mafuta kwenye ngozi;

I. Ute wa yai na limao
Limao lina citric acid hivyo husaidia kukausha mafuta yaliyozidi kwenye ngozi na ute wa yai unasaidia kusinyaa matundu ya ngozi uanayotoa mafuta. Chukua ute wa yai moja changanya na vijiko viwili vya juice ya limao kisha paka kwenye uso ulionawa kwa maji ya uvuguvugu na sabuni kaa dakika 15 na unawe

II. Alovera
Chukua kipande cha alovera Kata Kati Kati kwa kisu na uchukue ute wake na upake usoni kaa nusu saa kisha unawe.

III. Tango na limao
Majimaji ya tango yanayonya mafuta, kubana matundu ya ngozi na kucontrol uzalishaji wa mafuta. Changanya vijiko viwili vya juice ya tango na limao nawa uso kisha paka mchanganyiko huo usoni kaa dakika 20 kisha unawe.

IV. Nyanya na asali au limao na asali
Nawa uso kiss chukua kipande cha nyanya weka asali juu yake kidogo kaa dakika 20 na unawe
Au changanya asali kijiko kimoja na juice ya limao vijiko viwili paka usoni kaa dakika 20 kisha unawe.

MAFUTA MAZURI YA KUPAKA
Mtu mwenye ngozi ya mafuta anashauriwa kupaka cream au lotion ambayo sio nzito ili kuvipa vitundu vya ngozi nafasi na kuzuia kunata vumbi kirahisi. Unapoenda dukani nunua lotion iliyoandikwa FOR OILY SKIN

*Vitu muhimu vya kuzingatia
✔ Nawa uso kwa maji ya uvuguvugu na sabuni angalau Mara mbili kwa siku
❌Usipake cream nzito sana au lotion yenye mafuta
✔Tumia translucent powder kupaka makeup
✔Fanya scrubbing au facial mask walau mara mbili kwa wiki

05/05/2020

FAHAMU AINA ZA NGOZI

1. Ngozi kavu (Dry skin)
Hupauka na kukak**aa isipopakwa mafuta mara baada ya kunawa. Pia hutoa magamba kwa mbali na haitoi mafuta yoyote
Ngozi kavu inahitaji unyevunyevu na hukaa na powder au make up kwa musa mrefu

2. Ngozi ya mafuta (oily skin)
Huwa tepetepe, inang'aa na kutoa mafuta bola hata kupaka Chochote na matundu ya ngozi yako wazi.
Ngozi ya mafuta hupata vumbi kirahisi, chunusi na madoa

3. Ngozi mchanganyiko (Combination skin)
Ni aina ya ngozi ambayo ina mchanganyiko wa ngozi ya mafuta na kavu. Hutoa mafuta katika paji la uso kushuka hadi kwenye pua na huwa na ngozi kavu kwenye mashavu.

4. Ngozi ya kawaida (Normal skin)
Hii ni ngozi ambayo sio kavu wala haina mafuta Mengi na ukijifuta kwa karatasi nyeupe hutoa matone ya mafuta kwa mbali.

JINSI YA KUPIMA AINA YA NGOZI : Nawa uso kwa maji ya uvuguvugu na sabuni kisha kaa nusu saa na zaidi bila kujikausha, chukua karatasi au tissue jifute Kwenye ngozi ya uso ili kujua aina yako ya ngozi.

23/04/2020

Style mpya ya nywele

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Mbeya?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Mbeya