Augen kikande Hadithi

Augen kikande Hadithi

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Augen kikande Hadithi, Health/Beauty, Morogoro.

06/02/2021

KIVURUGE
SEHEMU YA KWANZA
Mwandishi: Augen Kikande

Jackson mwanga ni makazi wa tabata jiji dar es salam. Yeye ni mwalimu wa sekondari pia anaumri wa miaka 27. Anafanya kazi mkoani tanga, ni kijana wa busara sana. Huwa hapendi mambo ya utaniutani wala uongongo. Jakson ni kijana mzuri sana, msafi hapendi mambo ya uchafuuchafu. Pia alipendwa na watu wengi sana. Aliweza kubahatika kumuoa mwanamke nesi aliyekuwa anafanya kazi huko huko mkoani shinyanga. Waliishi pamoja lakini katika maisha ya ndoa yao hawakufanikiwa kupata mtoto. Jakson aliachana na mke wake kisa aliikuta meseji kwenye simu ya mke wake. Meseji iliyotumwa kwenye simu ya mke wake ilikuwa ni ya kutatanisha sana. Ilionyesha wazi kuwa mke wake anatoka na jamaa. Lakini haikuwa hivyo kumbe jamaa aliyetuma meseji alikuwa anamtongoza mke wake hawakuanza na uhusiano k**a alilivyofikilia Jackson. Ugomvi ulidumu katika ndoa ya Jackson kwa muda wa miezi mitatu, kila mmojaakawa anaishi kivyake. Kipindi jackson anafanya hivyo, yeye alikuwa anamahusiano ya kimapenzi na wanafunzi aliyejulikana kwa jina la Jenista. Ni binti wa kidato cha 4 katika shule hile aliyokuwa anafundisha jackson. Walipenda sana wakati mwingine jenista alidai mwalimu jackson amrudishe mke wake ili amuoe yeye. Ni jambo gumu sana kwa mwalimu jackson.

Maisha ya jackson na mke wake yalikuwa ya ugomvi sana, hapakuwa na amani hata mara moja, wakati mwingine mwalimu jackson hakulala nyumbani kwake. Alilala kwa jenista. Zikawa zimesalia siku chache mahafali ya kidato cha nne yafanyike. Mwalimu jackson aliamua kumtimua mke wake. Ndoa ilivunjika bila kujali hata mwenyewe alikuwa na makosa. Maana mke wake alitumiwa meseji ya kimapenzi lakini hakushiriki tendo na aliyetuma meseji. Lakini yeye alikuwa anashirikiana na jenista mwanafunzi wa kidato cha nne. Mke wa mwalimu aliachika, mwalimu jackson alibaki huru.
Siku ya mahafali ilifika, jenista alipendeza sana siku hiyo. Watu wengi sana walikusanyika katika sherehe, hata mke wa mwalimu alikuwepo katika sherehe hile. Wakati wa kutoa zawadi, mwalimu jackson alitoa zawadi kwa mpenzi wake huku wazazi wa jenista wakiwa hawajui k**a mtoto wao anakaa na yule mwalimu. Lakini baadhi ya walimu walikuwa wanajua kinachoendelea kati ya mwalimu jackson na jenista. Pia usiku wa sherehe hile mwalimu jackson walicheza sana musiki na jenista na baadae walienda kulala nyumbani kwa mwalimu jackson.

Baad ya wiki mbili mbele, mtihani wa kidato cha nne ulifanyika, Jenista hakukaa bweni alikuwa anakaa kwa mwalimu Jackson. Ratiba ya mtihani uliisha, jenista alienda kusalimia wazazi wake kisha alirudi kwa mwalimu jackson. Alikaa huko. Walimu wakawa wanashangaa na kumsema mwalimu jackson. Yeye mwenyewe akiwa ajui. Mwalimu jackson alinogewa na penzi la jenista mtoto wa kitanga. Alienda kutoa taarifa kwa wazazi wa jenista. Wao waliipokea taarifa ya mwalimu jackson, pia walifurahi sana mtoto wao kuolewa na mwalimu. Hasa pale walipoikumbuka bahasha ya mwalimu jackson ilikuwa na sh 40,000 k**a zawadi. Waliweza kuwekeana makubaliano, endapo jenista atafahuru mtihani, mwalimu jackson amsomeshe jenista.
Mwalimu jackson hakukalika shuleni, kila muda alienda nyumbani kwake, ili akaonane na jenista. Ilionekana wazi mwalimu jackson alimpenda sana jenista.

Siku moja mwalimu jackson aliingia ofisini alichukua kitabu chake, kisha alitoka na kuelekea chumba cha kidato cha tatu kufundisha. Walimu wenzake walikuwa ndani ya ofisi hile, yeye alipotoka, na kuelekea chumba cha kidato cha tatu walimu walianzisha mjadara.

Mwalimu ned : Jamani mnamuona kijana mwenzenu jinsi anavyopagawa na
Vitoto vya kitanga?
Mwalimu musa: Tunamuona bwana, ameamua kumtimua mke wake
Kisa kile kidumbwili jamani.
Mwalimu ned : Siku hizi mhajiriwa hakaliki shuleni, yaani kila muda nyumbani.
Akikaa shuleni masaa mawili yaani k**a mwaka mzima.
Kweli ujana unachangamoto zake.
Mwalimu musa: Yaani huyu jamaa ni mtu wa ajabu sana, anadhani hivi vitoto
Vinaweza kupanga maisha. Shahuli yake.
Madam msafi: ha ha ha ha haaaaaaaaa, nyie watu mi nawashangaa.
Mwalimu musa: Unatushangaa kivipi tena, alafu kicheko kikaliiiiiiiii alafu cha
dharau! Kulikoni tena.
Madam msafi: Mimi naona k**a mnamuonea wifu mwenzenu, au kwa kuwa
Nyie wazee ndio maana mnamsengenya mwenzenu?
Mwalimu ned: Uzee wapi wewe! Mimi nikitaka kuoa hata wanawake 1000 naoa.
Lakini si kwa kidumbwili k**a kile.

Mara mwalimu jackson aliingia, walimu wenzake walikatisha stori mwalimu ned alizuga kwa kuongea.
" jamani mnajua marehemu babu yangu alikuwa rafiki wa mwalimu nyerere, Waliwai kwenda uganda, uingereza, ujerumani. Alikuwa anaambiwa rafiki yangu ukitaka kuoa wanawake wakila kabira we oa. Babu yangu kusikiliza mazungumzo ya mwalimu nyerere naye alioa wanawake 12, tena wa kumi na tatu alimtimua bibi yangu mimi akamuoa huyo wa 13"........

ITAENDELEA

05/02/2021

KOBE NA BIBI KIZEE
SEHEMU YA 01
Mwandishi : Augen kikande

Hapo zamani zakale palikuwepo na bibi mmoja aliyekuwa na maajabu sana. Yeye aliweza kumiliki upembe ambao alikuwa anaupuliza pindi akitaka mvua, chakula k**a vile ugali nyama. Maji ya kunya, sabuni na vinginevyo vingi sana. Bibi huyo hakuwa na njaa kwani aliishi peke yake, hakuwa na mjukuu wala mtoto. Maisha yake yalikuwa mazuri sana. Bibi huyo alikuwa anaiahi pembezoni mwa msitu uliyokuwa mnene sana. Lakini baadae aliweza kumpekea mgeni kobe baada ya kupata shida msituni.

Mwanzo, kobe hakuwa na mabaka mabaka k**a alivyo kuwa hivi sasa, alikuwa safi sana. Mabaka ya kobe yalitokana na moto. Pia kobe na sungura walikuwa marafiki sana. Waliweza kula pamoja na kutembea pamoja. Lakini walikuja kupoteana baada ya moto kuwashwa katika hule msitu. Sungura na kobe walipoteana, sungura alimimbia mpoto lakini kobe hakuweza kukimbia. K**a unavyojua mwendo wa kobe ni polepole sana. Kipindi moto unawaka wanyama wengi waliweza kukimbia lakini yeye hakuweza kutoroka. Kobe aliungua moto, alikuwa na vidonda mwili mzima nusu afe.

Siku moja kobe aliyaona maisha ya polini ni magumu sana, chakula hakipatokani wala maji ya kunywa. Aliamua kuondoka msituni ili akatafute maisha mbele ya safari. Aliweza kujikokota na kidonda chake cha moto kilichokuwa kinanuka sana. Maana hapakuwepo na maji ya kuoshea kidonda chake. Safari iliumana kupita kutafuta chakula na maji ya kunywa. Kobe alipita huku na kule hakuweza kuona mto wenye maji wala chemichemi yoyote mito yote ilikakamia, hapakuwepo na maji. Pia hata chakula hakuweza kukiona. Katika pitapita yake akiwa kwa mbali aliweza kuona kibanda kikitoa umoshi. Kobe alitabasamu huku akisema
" Mungu saidia, naonaa pale mbele k**a kunabinadamu anaishi. Ngoja niende uenda akanisaidia chakula au maji ya kunywa.

Kobe alijikokota aliweza kukifikia kibanda alichokuwa anaishishi yule bini kizee mwenye upembe wenye kutoa chakula pindi aupulizapo. Maombi ya kobe yalijibu

Kobe : odi, odi.
Bibi kizee : karibu, pita ndani.
Kobe anaingia ndani huku kidonda chake kikitoa usaa sana na inzi wakimfuata kwa nyuma. Bibi kizee anavumilia harufu kali ya kidonda
Bibi kizee : Karibu. Kobe anakaribishwa huku bibi kizee akivuta kiti. Kobe anakaa huku akiwa ametumbua jicho kwa bibi kizee.
Kobe : Shikamoo bibi
Bibi kizee : Maaraba ujambo.
Kobe : Sijambo bibi naomba msaada
Bibi kizee : msaada hupi mjukuu wangu.
Kobe : bibi angalia hali niliyokuwa nayo, kwanza ninanjaa sana pia k**a kunauwezekano wa dawa naomba unisaidie kidonda kinanisumbia sana.

Bibi kizee aliingi ndani, alitoka na pepe, akarudi pale alipokaa akaupuliza akiomba maji. Maji yakabubujika, akayajaza katika kifaa kiitwacho pisi.
Pisi ni kifaa cha chuma kinachofanana na dumla, mara nyingi kilikuwa kinatumiwa na watu wa zamani. Maji yalijaa katika kifaa kile, kisha alipuliza tena na kuomba sabuni. Ikaja sabuni ya kuogea. Akamuosha kobe kidonda chake kisha alitoka na kurudi na majani. Aliyapondaponda kisha akayagandika katika kidonda cha mr kobe. Baada ya hapo harufu ilitoka kabisa baada ya kuosha kile kidonda. Kisha aliupuliza upembe akaomba chakula, chakula kilitoka kobe alikula na kushiba.

Baada ya wiki moja kidonda cha kobe kilipona, akawa anamshukuru mungu. Aliishi kwa yule bibi kizee kwa furaha sana. Pia alipata wazo la kwenda kumtafuta rafiki yake ili wote waishi pale kwa bibi kizee

ITAENDELEA

20/11/2020

KAA TAYARI KUIFUATILIA SIMULIZI KALI SANA.
NI KISA CHA UKWELI

šŸ”„SITOSAHAU NILICHOKIONA MOCHWARIšŸ”„

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Morogoro?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Morogoro