Tala_shopy
Vipodozi(urembo) na afya
28/10/2022
# # # #
03/07/2022
ULAJI WA UDONGO KWA WAJAWAZITO.
Ulaji wa Udongo kwa Mjamzito ni hali ya kawaida na hujumuisha asilimia 20 ya Wajawazito wote Duniani, Mjamzito anaweza kupata tatizo hili katika Miezi Mitatu ya mwanzo ya Ujauzito, Japokuwa huweza kuwaathiri Wajawazito katika vipindi tofauti tofauti vya Ujauzito, Pamoja na hali hii ya kula Udongo kuna baadhi ya Wajawazito hupendelea kula vitu vingine visivyo na manufaa/mengenywa katika Mwili, hii inaweza kupelekea Mjamzito kupata matatizo mbalimbali ikiwemo kupata Minyoo kutoka kwenye Udongo au uchafu, Sumu, kuziba kwa Utumbo na nk.
Hali hii ya kula Udongo au Vyakula visivyo na manufaa katika Mwili,endapo ikizidi kiasi kwamba inaweza kudhuru afya ya Mama kwa namna yoyote ile huitwa Pica. Hali hii pia huweza kuhusishwa na Magonjwa ya kisaikolojia au Magonjwa ya akili,vile vile huweza kuathiri Watoto wenye umri wa zaidi ya miaka miwili kwa asilimia 25 hadi 30.
Pica ni Tatizo au Ugonjwa wa kisaikolojia au hali ya kula vitu ambavyo havina umuhimu au manufaa katika Mwili kuliko kawaida Mfano; Mjamzito kula vitu k**a Mchanga, Udongo,Mawe,Barafu,Mkaa, Majivu na nk kupita kiasi. Neno “Pica” lilitokana na neno “Magpie”, la Kilantini ambalo ni jina la Ndege mmoja mwenye tabia ya kula karibia kila kitu anachokutana mbele yake ndipo walifananisha na ugonjwa huu unapo muathiri Mwanadamu.
Ili Mtu aweze kuwa na Ugonjwa au tatizo hili anatakiwa kukidhi vigezo vinne ambavyo ni K**a ifuatavyo;
1.Kula vitu visivyo na manufaa katika Mwili k**a ilivyotajwa hapo juu kwa Muda wa kuanzia mwezi mmoja na zaidi.
2.Kula vitu hivyo ambapo ni tofauti na taratibu au utamaduni katika jamii husika.
Ulaji wa vitu visivyo meng’enywa au kuwa na manufaa mwilini bila kuhusisha ukuaji wa huyo Mtu.
Endapo Mtu huyo ana Magonjwa ya akili, Mjamzito au Usonji anatumia vitu hivyo zaidi ambapo huhatarisha hali yake kiafya kutokana na kula vitu hivyo na Mtu huyo huhitaji Vipimo au matibabu zaidi ijapokuwa alipata matibabu mwanzo kuhusiana na hali hiyo.
Jinsi ya kufahamu utumie kiasi gani kwa siku
Chukua kilo zako gawanya kwa 24
Mf una kilo 60÷24=2.5
Ivyo utatakiwa kutumia 2.5 kwa siku
Maji Ni uhai ambae hatak kuzeeka haraka kua na ngoz nzur afya bomba kunywa maji Safi kwa kiasi kinachotakiwa
Usinywe maji mda umetoka kula tulia nusu saa au saa zima ndipo unywe ❤️❤️❤️❤️❤️❤️
*FANGASI KWENYE DAMU(SYSTEMIC MYCOSES)*
Ni maambukizi ya fangasi kwenye damu ambayo huanzia kwa fangasi kuvamia mapafu ya mtu.Maambukizi haya yamegawanyika katika sehemu kuu mbili;
Maambukizi ya fangasi kutokana na fangasi wa kawaida kwa watu wenye afya njema (Systemic mycoses due to primary pathogens)
Maambukizi ya fangasi kwenye damu kutokana na fangasi nyemelezi kwa watu wenye upungufu wa kinga mwilini (Systemic mycoses due to opportunistic pathogens)
Maambukizi ya fangasi kutokana na fangasi wa kawaida kwa watu wenye afya njema (Systemic mycoses due to primary pathogens)
Maambukizi haya ya fangasi huanzia kwenye mapafu na kusambaa kwenye viungo vingine vya mwili.Yafuatayo ni maambukizi ya fangasi kwenye damu yanayoonekana sana kwa wagonjwa nayo ni;
Histoplasmosis
Blastomycosis
Coccidioidomycosis
Histoplasmosis
Husababishwa na fangasi Histoplasma Capsulatum, ambao huishi kwenye mazingira hasa kwenye mchanga na mtu huweza kupata maambukizi ya fangasi hawa kwa kuvuta hewa yenye mazalia ya fangasi (Fungal spores).Watu wenye maambukizi haya huweza kuambukiza watu wengine au hata kuambukiza wanyama. Maambukizi ya histoplasmosis ni hatari sana kwa watu wenye kinga dhaifu mwilini hasa k**a yatasambaa kwenye viungo vingine vya mwili.
Dalili na Viashiria ya maambukizi ya Histoplasmosis
Homa kali
Uchovu
Kutetemeka (Chills)
Maumivu ya kichwa
Maumivu ya kifua
Maumivu ya mwili (Body aches)
Vipimo vya uchunguzi
Uchunguzi wa maabara kwa kutumia hadubini
Kuotesha fangasi maabara
Ugunduzi wa surface markers za fangasi aina ya Histoplasma Capsulatum kwenye mkojo
Vipimo vya damu vya kuangalia jinsi kinga za mwili zinavyojitahidi kukabiliana na maambukizi haya (Antibody response to histoplasma)
Tiba ya Histoplasmosis
Mara nyingi maambukizi haya hupona yenyewe kwa wale wanaopata maambukizi ya wastani
Kwa wale wenye kupata maambukizi hatari, uhitaji matibabu ya dawa za kutibu fangasi
Blastomycosis
Husababishwa na fangasi aina ya Blastomyces dermatitidis.Maambukizi haya hua
25/08/2021
Afya kwanza
Jali afya yako kwa virutubisho lishe asilia...wenye shida na matatizo yote karibu kwa ushaur na tiba 0744702026
25/08/2021
Karibu TALA natural product
Ushaur na tiba
23/08/2021
JINSI YA KUWA NA MUONEKANO MZURI WA MIGUU
1.Limao na mafuta ya mzaituni
Leo kwenye safu yetu hii ya urembo tunaona jinsi ya kuipata miguu mizuri yenye ngozi inayovutia kwa kutumia vitu asilia nyumbani kwako.
Vitu hivyo ni pamoja na limao ukichanganya na asali pamoja na mafuta ya zaituni au ukichukua limao ukachovya kwenye asali na mafuta ya mzaituni kisha ukasugua miguu yako.
Baada ya kuishugua acha kwa muda wa dakika 10-15 kisha paka mafuta au losheni unayoitumia.
2. Maziwa mgando kwa kuondoa sugu
Maziwa mgando ni kwa kuondoa sugu kwenye miguu cha kufanya chukua maziwa hayo paka kwenye miguu yako acha kwa muda wa dakika 10-15 kabla ya kuosha fanya hivyo kila unapokuwa na nafasi utaona jinsi utakavyokuwa na ngozi laini isiyokuwa na sugu, waka haina haja ya kwenda kuoshwa sehemu.
3.Maziwa na baking soda
Maziwa vikombe vitatu changanya na vijiko vitatu vya baking soda. Yapashe maziwa hayo uliyoandaa kisha changanya na baking soda ndani yake. Baada ya hapo loweka miguu hiyo kwenye huo mchanganyiko wako kaa kwa muda wa dakika 10, kisha osha bada aya hapo chukua maji ya vuguvugu osha miguu hiyo kuondoa uchafu wote..
4. Mafuta ya n**i kwa miguu iliyopasuka
Chukua mafuta ya n**i paka eneo lililopasuka taratibu fanyia masaji usiku, kazi ya mafuta ya n**i ni kulainisha ngozi yako na kuifanya ilainike.
Ukijaribu urembo huu utasahau kabisa kwenda kuosha miguu saluni.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Kihonda
Morogoro