Afya kwanza
tunatoa huduma za afya na ushaur wakiafya, pia tunatibu magonjwa mbali mbali, tupigie 0672004414 asanten na karibun.
12/08/2020
Ugonjwa Wa Kansa Ni Nini? Chanzo Cha Saratani Na Aina Za Saratani
ugonjwa wa kansa
K**a umekuwa ukisikia kuhusu ugonjwa wa kansa au saratani na ukawa unajiuliza ni nini ugonjwa huu wa kansa, pitia ukurasa huu ambamo tutatazama maana ya ugonjwa huu, chanzo chake, madhara anayoweza kupata mtu mwenye ugonjwa huu na tiba ambazo hutolewa kukabiliana na tatizo la kuumwa na ugonjwa huu wa kansa.
Kansa (saratani) ni neno lililotolewa kwa kundi la magonjwa yanayosabahiana. Kuna aina tofauti zaidi ya 100 ya magonjwa yanayoitwa kansa au saratani. Katika aina zote hizi za saratani, baadhi ya seli za mwili huanza kujigawa bila kusimama na kuenea kwenye maeneo ya karibu ya mwili. Kansa huweza kuanza kwenye sehemu yo yote ya mwili. Kwa kawaida seli za mwili hujigawa na kuzalisha seli mpya kulingana na mahitaji ya mwili, seli za zamani zikiharibika au kuzeeka, seli mpya huchukua nafasi ya seli hizo.
Saratani inapotokea, mpangilio huu huvurugika. Kadiri uvurugikaji huu unavyozidi, seli za zamani zinaendelea kuishi badala ya kufa na seli mpya hutengenezwa bila mahitaji ya mwili. Seli hizi za ziada huendelea kujigawa na kujenga uvimbe (tumors). Saratani za aina nyingi hujenga uvimbe isipokuwa saratani za damu, k**a leukemia, ambapo ugonjwa huu huzuia ufanyakazi kazi wa kawaida wa damu kwa kusababisha kugawanyika kwa seli za damu kusiko kwa kawaida.
saratani ni nini
Uvimbe unaotokana na saratani ni hatari kwa maisha, huweza kuenea kwenye maeneo ya karibu ya mwili na kadiri unavyokua baadhi ya seli huweza kujitoa kutoka eneo moja zikasafiri kupitia mfumo wa damu hadi eneo jingine la mwili na kuanza kujenga uvimbe mpya kwenye eneo hilo jipya mbali kabisa na eneo la awali. Uvimbe wa saratani huweza kukua na kuvuruga utendaji kazi wa mfumo wa mmeng’enyo wa chakula, ubongo na mfumo wa damu. Uvimbe unaotokana na saratani ukiondolewa, huweza kurudia kujijenga upya kabisa.
Chanzo Cha Kansa
Kansa ni ugonjwa unaotokea katika viini vya mwili vinavyohusika na kurithisha tabia kutoka kizazi kimoja hadi kingine (genes) – ni ugonjwa unaotokana na kubadilika kwa genes zinazohusika na ufanyaji kazi wa seli za mwili, na hasa zile zinazohusika na namna seli zinavyokua na kujigawa.
Mabadiliko katika genes yanaweza kuwa ya kurithi kutoka kwa wazazi au yanaweza kutokea katika kipindi cha maisha ya mtu kutokana na hitilafu zilizotokea wakati wa kugawanyika kwa seli au kutokana na uharibifu wa DNA uliotokana na vitu vilivyopo kwenye mazingira viitwavyo carcinogens. Vitu vya kwenye mazingira vinavyosaidia kuharibu DNA na kukua kwa kansa (carcinogens) ni k**a kemikali zilizopo ndani ya moshi wa tumbaku, asbestos, arsenic, mionzi ya gamma, X-rays, moshi wa magari na mionzi ya jua (UV rays).
20/03/2020
U.T.I NI HATARI UNAWEZA KUKOSA KABISA UZAZI.
DALILI ZA U.T.I
1.Kukojoa mara kwa mara na maumivu wakati wa kukojoa.
2.Kuhisi kuunguzwa na mkojo kwenye kibofu au mrija wa mkojo.
3.Maumivu ya misuli na tumbo
4.Mkojo kuwa na harufu mbaya na pia kubadilika rangi kuwa nyeusi au rangi ya mawingu n.k
5.Kwa mtu aliyeathiriwa figo anaweza kuwa na maumivu mgongoni au kwenye mbavu pia kichefuchefu na kutapika.
6.Kushikwa na hamu ya kukojoa ila mkojo unatoka kidogo kidogo uku unapata maumivu kwenye njia ya kupitisha mkojo.
UKIWA NA DALILI ZA HAPO JUU JIPATIE FERMICARE KWA MATIBABU ZAIDI.
KAZI ZA FERMICARE NI;
•Hutibu U.T.I Sugu
•Hutibu Miwasho
•Huimarisha Ulinzi Dhidi ya Bacteria
•Huzibua mirija ya uzazi iliyoziba
•Ni Tiba dhidi ya Miwasho
•Hutibu Fangasi
•Huondoa Harufu Mbaya Ukeni
•Ni Njia ya Kusafisha uke bila Kemikali
•Hukufanya Uwe Huru Na Mwenye Furaha muda wote
•Ni Rahisi kutumia
•Huondoa Kutokwa na Uchafu Ukeni
•Huondoa Maumivu wakati Wa hedhi
•Hurekebisha Mzunguko Wa Hedhi.
WASILANA NASI KWA NAMBA
JIUNGE NA GROUP LETU KWA TAARIFA ZAIDI KUHUSU AFYA.
0672004414
20/03/2020
Mfumo wa mkojo huundwa na figo, njia ya mkojo inayotoka kwenye figo hadi kwenye kibofu(yureta),kibofu cha mkojo na njia ya mkojo inayotoka kwenye kibofu hadi nje ya mwili(yurethra).Maambukizi ya bacteria huweza kuathiri sehemu yoyote ya mfumo huu. Maambukizi ya mfumo wa mkojo ni ya pili ukiangalia maambukizi yote ya mwili.
Dalili za maambukizi ya mfumo wa mkojo ni zipi?
Dalili hutofautiana kulingana na ukali wa maambukizi,umri na sehemu iliyoathirika.
Dalili zinazojitokeza mara nyingi pakiwa na maambukizi (UTI):
Uchungu au kuwashwa unapokojoa.Kuhisi kukojoa mara nyingi.Homa na uchovu .Mkojo wenye harufu mbaya na si safi (cloudy).
Dalili zinazotokana na maambukizi ya kibofu
Maumivu katika upande wa chini wa tumbo.Kukojoa mkojo kidogo , wenye maumivu na mara nyingi.Dalili za homa kidogo. Bila maumivu ya mbavu.Damu kwenye mkojo.
Dalili zinazotokana na maambukizi ya upande wa juu wa njia ya mkojo
Maumivu ya upande wa juu wa mgongo na mbavu.Kuwa na homa na kuhisi kibaridi. Kichefuchefu, kutapika, uchovu na kujihisi mgonjwa kwa ujumla.Kuchanganyikiwa kwa wazee.
Maambukizi haya ni hatari sana yasipotibiwa vyema na haraka. Aidha yanaweza hata kuhatarisha maisha.
Kuwashwa na kukojoa mara nyingi ni dalili za maambukizi ya sehemu za mfumo wa mkojo.
Chanzo
Nini kinachosababisha maambukizi ya mara kwa mara ya njia ya mkojo?
1. Kuziba kwa njia ya mkojo.
2. Maumbile ya k**e Kwa sababu njia ya yurethra ya wanawake ni fupi kuliko ya wanaume,basi huwezekano wa kupata maambukizi ni mkubwa zaidi kuliko wanaume.
3. Maingiliano/ Kujamiiana: Wanawake wanaoshiriki tendo la ndoa huweza kupata maambukizi mengi zaidi kuliko wenzao wasioshiriki tendo hilo.
4. Mawe Mawe kwenye figo, njia ya kuelekea kwenye kibofu cha mkojo (ureta) au ndani ya kibofu chenyewe yanaweza kuzuia mtiririko wa mkojo na hivyo kusababisha maambukizi.
5. Mpira wa katheta Watu waliowekewa katheta wana uwezekano mkubwa wa kupata maambukizi kirahisi.
6. Kasoro za kimaumbile Watoto wenye kasoro za kimaumbile k**a mkojo kurudi nyuma k**a kwenye kibofu na hivyo kwenda kwenye yureta ( vesicoureteral reflux) au k**a njia ya yurethra valve inafungukia nyuma, hupata maambukizi kwa urahisi sana.
7. Kuongezeka ukubwa wa tezi dume Wanaume walio na umri wa miaka zaidi ya sitini wanaweza kupata maambukizi kwa sababu ya kukua kwa tezi dume.
8. Kinga ya mwili iliyodhoofika Wagonjwa wa kisukari,UKIMWI au saratani.
9. Sababu nyingine: k**a njia za yureta na yurethra kuwa nyembamba,tibi (TB) kwenye njia ya mkojo, neurogenic bladder,diverticulumnk
0672004414
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Morogoro