NENO La UZIMA

NENO La UZIMA

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from NENO La UZIMA, Health/Beauty, Morogoro.

29/10/2024

MUZIKI NA ANGUKO LA MWANADAMU. Seh 3

"Tazama, haya tumeyapeleleza, ndivyo yalivyo; Yasikie, uyajue, ili upate mema." Ayubu 5:27.

Na. Johanes J Ryoba

ya 3

Baada ya kutazama historia ya muziki na anguko la mwanadamu tangu edeni hadi kwa wana wa Israel; hebu sasa tupige hatua kidogo tuone ni aina gani ya muziki ambao ni hatari kupigwa kwenye nyumba za IBADA.

Charlie Gillett katika kitabu chake kiitwacho The Sound of the City 1970, uk 14 anaandika kuwa "Muziki aina ya blues, Jazz, Rock, Reggae, Rap na aina zingine za dansi ya kisasa ina mwingiliano wa karibu na isiyoepukika na mmomonyoko wa maadili, ulevi, madawa ya kulevya, K**ali, Umalaya na Uovu mwingine" Kwa kuthibitisho zaidi unaweza kujisomea mwenyewe

https://www.scribd.com/document/685172599/Sounds-of-the-city

Ni vigumu sana kutenganisha aina hizi za muziki na ngono, ulevi na madawa ya kulevya k**a bangi. Kwa mfano muziki wa Jazz ni jina linalosimama badala ya kujamiana (Sexual in*******se) ambalo lilichipuka miaka ya 1900s kule Marekani kwenye nyumba za makahaba.

utakuwa umepata jibu la swali hili "Kwa nini waimbaji wengi wa injili wanakumbwa na skendo ya uzinzi? Au kwa nini waimbaji wengi wa kwaya wanaanguka kwenye uzinzi? .

Graham Gray anasema kuwa kwenye aina zote za muziki wa POP, maneno au mashairi siyo kitu cha muhimu sana. Pop ni muziki wa hisia unaozungumza na mwili.

Kwahiyo aina hizo za muziki husisimua mwili wa mwanadamu na hazitoi nafasi ya mtu kutafakari mashairi au maneno yaliyoimbwa humo ndani. ni je aina hizo za muziki haziko kanisani leo hii? JIBU ZIPO NYINGI SANA.

Ukweli wote ni kwamba nyimbo nyingi zinazoitwa nyimbo za injili ni nyimbo za kidunia zenye mashairi yanayoonekana k**a ni ya kiroho. Mtu kuimba nyimbo yenye maneno ya kwenye Biblia haimanishi kuwa yupo sahihi katika uimbaji wake. Hata shetani alitumia maandiko kumjaribu Yesu; kwa kutumia kwake maandiko haikumaanisha kuwa alikuwa sahihi.

David Wells alifanya utafiti na kuchunguza nyimbo elfu moja *1,000* za sifa na ibada. MATOKEO YA UTAFITI HUO YALIKUWA K**A IFUATAVYO.....
60 za nyimbo za sifa na ibada zilizochunguzwa zilikosa sifa ya kuwa nyimbo za sifa na ibada kwa sababu ZILIKOSA MAFUNDISHO NA MAELEZO YA KINA.
# Nyimbo hizo za sifa zilikosa maelezo ya kwa nini mtu anasifu au kwa nini anaabudu.

mwingine unaonyesha kwamba waimbaji wengi hawajui kwa nini wanaimba na wengine hawajui hata wanachokiimba nini, kimetoka wapi na kina fundisha nini? (Hasa waimbaji wa kwaya). Yaani ni kana kwamba wanachokiimba hakiwahusu wao....
ni kwamba maana moja wapo ya kuimba kwa akili ni kuimba unachokijua.

ni ibada na k**a vile ambavyo kila fundisho lazima lipimwe kwenye neno la Mungu ndivyo ambavyo na kila nyimbo inayoitwa ya ibada inapaswa kupimwa k**a kweli inatokana na Neno la Mungu (Fundisho sahihi).

1 Wathesalonike 5:21-22 "Jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema; jitengeni na ubaya wa kila namna."

Changamoto nyingine inayozikumba kwaya zetu ni hii ya kuimba wimbo ambao hauwendani na tukio. utakuta ni wakati wa matoleo wao wanaimba wimbo wa wafu au ubatizo 🙄 alafu wala hawaoni aibu.
bora kutokuimba kuliko kuimba wimbo ambao hauwendani na tukio linaloendelea kwenye ibada. K**a kwaya hazina nyimbo kwa nini zisitumie nyimbo za tenzi za rohoni zinazoendana na tukio?

mengine ya hovyo ambayo shetani amefanikiwa kuyapenyeza kwenye ibada ya nyimbo ni aina ya mionekana ya waimbaji. waimbaji hawajui kuwa na wao ni wahubiri wa neno la Mungu kupitia muziki? K**a wanajua kwa nini mavazi yao hayamtukuzi Mungu?.

"Ni kweli sana kwamba heshima kwa nyumba ya Mungu imekaribia kutoweka. Mambo matakatifu na mahali patakatifu havitambuliwi. Je hatuna sababu ya kuwa na kicho kwenye nyumba ya Mungu? Tuna sababu nyingi .......lakini adui amekuwa akifanya kazi kuharibu imani yetu katika utukufu wa ibada ya kikristo" Child Guidance P. 541.

.........
[email protected]

27/10/2024

Na. Johanes J Ryoba

Maombi siyo majibu, majibu yako anayo Yesu. YESU NDIO JIBU LA CHANGAMOTO YAKO. Lakini maombi ni njia ya kukutana na Yesu mwenye majibu yako.

Hivyo, ukiona unaomba na bado huoni badiliko, usiache kuomba, endelea kuomba hadi ukutane na Yesu. Na hakuna mtu aliyewahi kukutana na Yesu na akabaki k**a alivyo.

Unapoomba siyo kwamba Mungu hakusikii, ANAKUSIKIA ila anataka uendelee kuomba maana kadri unavyoomba ndivyo unavyozidi kumsogelea Mungu. Na kadri unavyozidi kumsogelea Mungu ndivyo unavyozidi kumsikia kwa ukaribu.

unapoomba Mungu husikia ila kuna wakati Mungu huongea lakini hatusikii kwa sababu tuko mbali naye.

Ayubu 33:14 "Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali."

Sasa, kadri unavyozidi kuomba na KUOMBA na kuomba ndivyo tunavyozidi kuwa karibu na Mungu kiasi cha kumsikia Mungu.
Ukiona unaomba na huoni JIBU_usiache kuomba huenda uko mbali sana na Mungu, endelea kuomba hadi uwe karibu naye.

Maombi hayamshushi Mungu chini bali humuinua mwombaji kuelekea juu karibu na Mungu.
MAOMBI ni fursa ya kumkaribia Mungu.

Waebrania 4:16 "Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji." Namna pekee ya kukikaribia kiti cha enzi ni kwa KUOMBA.

mmoja wapo wa maombi ni KUOMBA BILA KUKOMA Luka 18:1, Yakobo 5:17-18.

kuomba.

23/10/2024

USIPENDE BILA KUFIKIRI KWANZA

Na. Johanes J Ryoba

Hakuna mtu duniani anayeweza kuharibu kwa ufanisi mkubwa furaha ya mwanamke, na kumfanya kuwa na majuto na maumivu k**a mume wake mwenyewe.
Na hakuna mtu anayeweza kuzima ndoto, malengo, mipango, matumaini, imani ya mwanaume na kuua nguvu zake k**a mke wake mwenyewe.

Ingawa unaweza kupenda, usipende bila ya kufikiri kwanza; nasiyo kufikiri tu bali kufikiri kwa makini.
ambako kutakupelekea kujiuliza maswali magumu kabla ya kukubali kuingia kwenye ndoa.

Watu wengi huingia kwenye ndoa kwa kujiuliza maswali rahisi sana; wengi hujiuliza JE ANANIPENDA au LA! na kuingia kwenye ndoa.
Hebu jiulize maswali magumu na ya msingi yatakayokusaidia.

Kwa kuwa maisha ya ndoa huathiri maisha ya mtu katika ulimwengu huu wa sasa na ule ujao, nivizuri ukajiuliza maswali yafuatayo.....
, huyu mtu anafaa kuwa mume au mke wangu? Je, anafaa kuwa baba au mama watoto wangu? Je, nitakuwa na amani watoto wangu kuwa na baba au mama k**a huyu?
, atanifanya kuwa bora zaidi ya nilivyo leo?

tena; Je, muunganiko huu utanisaidia kwenda mbinguni? Je, utaongeza upendo wangu kwa Mungu? K**A JIBU NI NDIO SONGA MBELE K**A SIYO MPIGE NA KITU KIZITO muache apambane na hali yake.

Moja ya swali muhimu la kila binti kutafakari, kuuliza, kupeleleza na kujua NI MAHUSIANO KATI YA KIJANA WA KIUME (Mchumba wako) NA MAMA YAKE MZAZI k**a yupo hai (mama mkwe wako mtarajiwa). hili utalia kilio kikuu...
binti yangu jiulize swali hili.....Je, mchumba wangu ana mama? Je mahusiano ya mchumba wako na mama yake yakoje?
, anamjali mama yake? Ikiwa hamjali na kumstahi mama yake aliyemzaa atakujali wewe? ACHA KUJIDANGANYA, mwanaume ambaye hamjali mama yake hawezi kumjali mke wake. IKIMBIE LAANA HIYO KWA MIGUU YAKO YOTE.

anaye beti, anayekunywa pombe, asiyeamini huyo MPIGE BLOCK. Ndio muache, kwani unafurahia watoto wako kuwa na baba mlevi?

LA MUHIMU kwa kijana wa kiume kujiuliza ni hili... Je, mchumba wangu ana baba? Yupo wapi? Mahusiano yake na familia yake yakoje? Ikiwa mchumba wako ana baba na wanaishi pamoja lakini maamuzi yote yanafanywa na mama.... UTAJUA MWENYEWE 😀😀😀 usuke au unyoe.

bora kuvunja uchumba wa mchongo, kuliko kuvunja ndoa. Maumivu, gharama na hatia ya kuvunja uchumba ni asilimia 0.5/100% lakini uchungu, gharama, hatia ya kuvunja ndoa ni asilimia 100/100%. MAUMIVU YA KUVUNJA NDOA yana anza kukuathiri wewe mwenyewe, watoto na watu wote waliokuwa wanaizunguka ndoa yenu.

la hatari unaloweza kulifanya ni kuingia kwenye ndoa bila kujua familia ya mchumba wako. hapa umekwisha unaweza kuoa au kuolewa na katoto ka mkuu wa wachawi na labda ndiyo kamerithishwa tunguli......UTAJUA KUWA HUJUI. mwangu.

akili kuingia kwenye ndoa, na usipomtanguliza Mungu kwenye hatua za awali, maisha ya ndoa yatakuwa magumu. Utaimba sana bora ugali mlenda kwenye amani kuliko wali nyama kwenye vita.

ya kueleza yote haya bado kuna kabinti kataendelea kumganda Msela mwenye dalili hatarishi...... na kuna boi ataendelea.... 😂 kweli sikio la kufa halisikii dawa.
USIJE KUSEMA HUKUAMBIWA, NINAKWAMBIA HAYA KABLA HUJAOA AU KUOLEWA.

**a umeoa au bado Jipatie nakala ya kitabu cha FIKIRIA NDOA kabla na baada ya ndoa kitakusaidia. Kina kurasa 204. Sura 12 marejeo 40. Mawasiliano 0714054430 call/Whatssap.

[email protected]

18/01/2024

UNATAKA KUWA MKUU? BASI USIKWEPE HAGHARAMA

"Vya bure havina thamani, havina baraka, havina amani, haviwezi kukutoa. Vya bure siyo vya kutamani"



Waswahili wanamsemo usemao cha kuazima hakisitiri makalio
k**a ndivyo basi cha bure ni zaidi ya cha kuazima.

Katika juhudi yangu ya kutafuta maarifa nimekuja kugundua kuwa moja ya kizuizi kinachotuzuia tusifike mahali tunapotamani kufika ni kupenda vya bure.
Kupenda kupewa vya bure ni laana kwa sababu dunia hii haijasanifiwa kwa namna ya kutoa vitu bure. Dunia hii inaongozwa na kanuni ya nipe nikupe.

Kupenda vya bure ni ishara ya kukwepa kulipa gharama. Tusichokijua ni kwamba vitu tunavyotaka tupewe bure wenzetu wametumia gharama kuvipata.

Jenga tabia ya kutambua juhudi za wenzako kwa kulipia gharama ya muda wao, bidhaa zao n.k. Ukijifunza kununua au kulipia kitu utakithamini mno. Ukipewa bure hautaona thamani yake na kwa namna moja au nyingine utakuwa umepitwa na fursa na baraka iliyoambatana na kitu hicho.

Ukisoma Biblia utagundua kuwa watumishi wa Mungu wengi walikwepa mtego wa kupewa vitu na wanadamu wenzao bila kulipia gharama.

Ibrahimu baada ya kufiwa na mkewe sara akiwa nchi ya ugenini. Aliwaomba wageni wampe mahali pa kuzikia apanunue kwa gharama elekezi. Hata wageni wa mji walipompatia ardhi bure Ibrahimu alikataa kupokea bure bali alitoa fedha na kununua kwa bei elekezi. Mwanzo 23:1-16.

Daudi
Kuna wakati Daudi alikuwa anatafuta eneo la kumjengea Mungu madhabahu. Mtu mmoja aitwae Arauna akamwambia Daudi kuwa achukue eneo analotaka bure ili amjengee Mungu madhabahu lakini Daudi alikataa kupokea bure bali alinunua kwa gharama elekezi kwa wakati huo 2Sam 24:18- 25.

Mtume Paulo nae aliandika kuwa
2 Wathesalonike 3:7-8
[7]Mwajua wenyewe jinsi iwapasavyo kutufuata; kwa sababu hatukuenda bila utaratibu kwenu;
[8]wala hatukula chakula kwa mtu ye yote bure; bali kwa taabu na masumbufu, usiku na mchana tulitenda kazi, ili tusimlemee mtu wa kwenu awaye yote.

UMEJIFUNZA NINI KWA IBRAHIMU, DAUDI & PAULO?

[email protected]

29/04/2023

SHETANI NA WATUMISHI WATATU

Shetani akawatokea watumishi watatu na kuwaambia: K**a ningewapa nguvu ya kubadili jambo lililotokea siku za nyuma, mngefanya nini?

Wa kwanza kati yao, aliyekuwa na kibali sana cha utume, akajibu: "Ningalikuzuia usimdondoshe Adam na Hawa dhambini ili binadamu wasimuasi Mungu."

Wapili, mtu aliyejaa rehema, akamwambia: "Ningalikuzuia usizipate rehema za Mungu na ungalikuwa kifungoni milele."

Watatu kati yao aliyekuwa mwepesi kuliko wote, badala ya kumjibu mjaribu wake, alipiga magoti, na kufanya ishara ya msalaba na kusema: "Ee Mungu niepushe na jaribu la kuwaza kile ambacho kingalitokea ambacho hakikutokea."

Shetani, akatoa kilio kikubwa cha uchungu huku akiwa na maumivu makali, akapotea.

Wale wawili wakashikwa na butwaa, wakamwambia: "Mtumishi, mbona umekuwa hivyo?"
Akajibu: "Kwanza kabisa: HATUPASWI kujadiliana na adui. Pili: HAKUNA anayeweza kubadili yaliyokwisha kutokea. Tatu: Shetani hakunuia kuangalia kupima imani yetu, bali kutunasa kwenye siku zilizopita, ili tuupoteze wakati tulionao sasa, wakati pekee ambao Mungu hutupa neema yake na tunaweza kushirikiana nao kutimiza mapenzi yake."

Katika mapepo yote, yanayowanasa watu wengi na kuwazuia kuwa na furaha ni lile la "Nini kingaliweza kutokea na hakikutokea."

Yaliyopita huachwa kwenye rehema za Mungu na yajayo pia tunamuachia yeye. Ni wakati wa sasa pekee ulioko mikononi mwetu.

19/12/2022

THE REASON WHY GOD CREATED TITHING - Dr.Myles Munroe

Tithing has nothing to do with giving God money,God doesn't need nothing from you, He can't even give God nothing.
Everything on the Earth already belongs to God, you don't need nothing from us, so when God's sets something up is not because he needs it.

Tithing and offering is God's management training program for human kind,God doesn't need a penny from us and yet He tells us 100 percent of everything is mine, we only think of money and that's our problem.

-If you get 10 shoes, one of them ain't yours.
-If you get 10 dresses, one of them ain't yours.
- If you get 10 oranges, one of them is not yours.
-If you get 24hours a day, 2hours 40minutes does't belongs to you.

You are a thief everyday if you don't give your 2hours 40minutes for God, a time theif,you spend 2hours, 4hours,8hours watching cable television you can't even give God the 2hours 40minutes that belongs to Him, you can't even manage the 2hours and 40minutes.
God can in anytime and any minutes command you to give that dress away, it doe's belongs to you.

So tithing and offering is not about money, is about management.
Can you consistently give tithe.
God said,put aside 10 percent of everything for my purposes, that's tithing.
100percent of everything belongs to God and God says put aside 10percent for His work leaving 90percent,which still belongs to God.
So then if God owns everything, why will He allow you to put aside 10 percent if all things belongs to Him, Is because is not about the money, is about your ability to put it aside, your will, your control, your discipline to put it aside, HE IS AFTER YOUR DISCIPLINE.

If you can manage the 10percent properly, then He is happy to trust you with the 90percent but because you have been unfaithful with the 10percent, you keep loosing the 90percent and end up with NO PERCENT.

WHAT TITHING DOES TO YOU - Dr. Myles Munroe
Each of this words is management.
1. Accountability - if you keep paying you tithe , you must have first become accountable.
2. Discipline - for you to put aside the 10 percent every single time, you take control.
3. Honesty - for you to be a tither, that means no one is watching except God and God knows if you are paying 10 percent or not, that means you can lie to anybody else but God knows.
It makes you honest and managers must be honest.
4. Diligence - it means you work hard consistently to make sure you don't steal God's 10percent.
5.Faithfulness - most managers are unfaithful and it takes faithfulness to tithe.
6.Trustworthiness - for you to manage your tithe, God is going to trust you every time.

I just gave you the characteristics of a manager.
they are ACCOUNTABLE, DISCIPLINE,HONEST DILIGENT FAITHFUL AND TRUST WORTHY.

MANAGEMENT AND PRAYER - Dr. Myles Munroe
God will not give you what you pray for, only what you can manage.
You pray for a 1,000 dollars and God says I give you a 100 dollars yesterday you can't even pay 10 dollars tithes.
You pray for a big house and the house you are renting, you keep it dirty, you can't manage another person's property ,how can I give you a property of your own.
You pray for a bigger church and you can't manage the church you are renting.
You pray for souls and and the people you get, you can't manage. God protects them from You.

If you get the million dollars you are praying for, it will kill you, You cannot manage 500 dollars.
You spend 200 on your dress ,150 on your hair and you put 20 in the offering box and you ask God for a million dollars, is God stupid or what...

(Tithing will not give us salvation but the promises attached to it.)

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Morogoro?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Morogoro