FPCT Njombe MJINI.

FPCT Njombe MJINI.

Share

wakati uliokubarika ndio huu wakumwabudu MUNGU. usisubiri giza liingie

11/05/2020

HATUA ZA MWANAADAMU ZINAIMARISHWA NA MUNGU.

Zaburi 37:23-24
[23]Hatua za mtu zaimarishwa na BWANA,
Naye aipenda njia yake.
[24]Ajapojikwaa hataanguka chini,
BWANA humshika mkono na kumtegemeza.

Hakuna mtu anayeweza kujiimarisha yeye mwenyewe bali anahitaji msaada wa MUNGU. Katika mapito yote anayopitia mwanadamu anamhitaji MUNGU ili kuimarisha mapito yake.

Bila YESU sisi hatuwezikufanya jambo lolote itakuwa nikujirisha upepo tu. Iwe unauchumi mzuri unamhitaji MUNGU aimarishe uchumi wako. Iwe ni uchumba unamhitaji MUNGU aimarishe uchumba wako. Iwe ni biashara unamhitaji MUNGU aimarishe biashara hiyo.

Maisha yetu ya WOKOVU yanaimarishwa na BWANA hakuna mtu anaweza kusimama mwenyewe bila ya nguvu za MUNGU. Huduma zetu zinaimarishwa na MUNGU bila MUNGU zitaonekana za hovyo saaana tunamhitaji MUNGU kwa kila jambo.

Hatuwa zetu si katika uwezo wetu. Shida ipo pale tunapoanza kumpa mwingine utukufu badala ya kumpatia MUNGU. MUNGU anachukia saana kutokumpa utukufu ndio maana watu wengi wamejikuta kuachwa na MUNGU.

MKIMBILIE MUNGU SOGEA NAYE ATAKUIMATISHA PALE UTAKAPOANZA KUMWAMINI.

28/04/2020

Kuwa na furaha ni siraha tosha ya kumdhoofisha adui usijinyime furaha.

Photos from FPCT Njombe MJINI.'s post 14/04/2020

KATIKA IBADA YA LEO SIKU YA JUMANNE YA MAOMBI IKIONGOZWA NA BISHOP

.

Maandiko matakatifu yalioongoza maombi ya leo yanatoka kitabu cha 1falme 8:48.. 52.

1 Wafalme 8:48-53
[48]watakaporejea kwako kwa mioyo yao yote, na kwa nia zao zote, katika nchi ya adui zao, waliowachukua mateka, wakikuomba, kwa kuikabili nchi yao, uliyowapa baba zao, na mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako;
[49]basi, uyasikie maombi yao na dua yao, huko mbinguni, makao yako, ukaitetee haki yao;
[50]ukawasamehe watu wako waliokutenda dhambi, na makosa yao yote waliyokukosa; ukawape kuonewa huruma mbele yao waliowachukua mateka, ili wapate kuwahurumia.
[51]Kwa kuwa ni watu wako, na urithi wako, uliowatoa katika Misri, toka katikati ya tanuu ya chuma.
[52]Macho yako na yafumbuke, na kuielekea dua ya mtumwa wako, na dua za watu wako Israeli, ukawasikilize kila wakati watakapokulilia.
[53]Kwa maana uliwatenga na watu wote wa dunia, wawe urithi wako, k**a ulivyonena kwa mdomo wa Musa, mtumishi wako, hapo ulipowatoa baba zetu katika Misri, Ee Bwana MUNGU.

●Bwana ayasikilize mahitaji yetu tunayompelekea.
● Bwana atimize ahadi zake alizoahidi kututendea.
●Bwana atuepushe dhidi ya magonjwa nyemelezi, yaliyotumwa toka kuzimu BWANA atuepushe nayo.
● Bwana aponye uchumi wetu usidolole bali uendelee kuchanua.

MUNGU AKUBARIKI MPENDWA KATIKA BWANA.

14/04/2020

RATIBA ZA IBADA HAPA KANISANI.

1. jumanne MAOMBI.
2. Jumatano KWAYA YA VIJANA.
3. Alhamisi KWAYA YA EBENEZER
4. IJumaa Ibada. BIBLE STUDY.
5. jumamosi MAZOEI. kusifu na kuabudu, kwaya ya Ebenezer, kwaya ya mwebrania.
6. Jumapili ibada kuu na maombezi.

KARIBUNI SAANA NA MUNGU AWABARIKI.

13/04/2020

YESU NDIYE UFUFUO NA UZIMA WEKA TUMAINI KWAKE UTAISHI.

13/04/2020

Tunamshukuru MUNGU kwa ibada nzuri tuliyokuwa nayo jana. Neema band wakiimba

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Njombe?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Chauging
Njombe