AFYA NI MTAJ WAKO
Tutajifunza changamoto mbalimbal za kiafya ambazo zinawakumba wanawake kwa wanaume.
01/12/2022
*Sababu za kupata hedhi kidogo*
⏭️Matumizi ya baadhi ya njia ya uzazi wa mpango hasa zile zenye vichocheo ndani yake kwani hubadilisha vichocheo vya mwili.
⏭️Tatizo la mwanamke kushindwa kutoa yai au tatizo la ovaries kutofanya kazi vizuri hasa mwanamke akikaribia ukomo wa hedhi.
⏭️Tatizo la mwanamke kuwa na uzito mdogo sana wa mwili au mwanamke kupungua uzito kwa kiasi kikubwa.
Mabadiliko haya ya mwili husababisha kiwango cha mafuta mwilini kuwa kidogo sana hali ambayo huweza kuathiri utokaji wa yai kutokutoka kabisa.
⏭️Tatizo la msongo wa mawazo. Fahamu kwamba ukiwa na stress mzunguko wako wa hedhi unaweza kubadilika kabisa na moja ya mabadiliko ambayo unaweza kuyapata ni pamoja na hedhi kuacha kabisa kutoka au kutoka kidogo.
28/11/2022
*Sababu ya hedhi kutoka kwa muda mrefu*
⏺️Kuvurugika kwa homoni na mayai kupevuka.
⏺️Matumizi ya dawa yanaweza kupelekea hedhi kutoka muda mrefu.
⏺️Mimba kutunga nje ya kizazi.
⏺️Uvimbe Kwenye kizazi(Uterine fibroids or polyps).
⏺️Kutanuka kwa kizazi (adenomyosis).
⏺️Matatizo ya tezi ya thyroid(tezi ya shingoni).
⏺️Uzito Mkubwa na Kitambi.
⏺️Pelvic inflammatory disease(PID).
⏺️Saratani
Je unasumbuliwa na tatizo hili nina suluhisho lako, karibu tulimalize tatizo🤗🔥🔥
26/11/2022
*Dalili za upungufu wa nguvu za kiume*
Dalili za kuonesha kuwa una tatizo la upungufu wa nguvu za kiume karibia zote zinahusiana na hali itakayo onekana katika tendo la ndoa au mda wa kujamiiana, hizo dalili zake ni k**a;
⏩Kuwahi kufika kileleni.
⏩Kukosa hamu ya mapenzi.
⏩Kushindwa kurudia tendo la ndoa.
⏩Uume kusimama kwa uregevu au kushindwa kusimamisha.
⏩Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu; Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji.
⏩Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo.
⏩Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa).
⏩Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji.
26/11/2022
*CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME*
Tatizo la nguvu za kiume lina vyanzo vingi ambavyo mara nyingi wengi huvipuuza, hivyo vyanzo huathiri taratibu na vingine huathiri haraka, tunashauri watu kuwa makini sana ili kujiimarisha vizuri. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata tatizo la nguvu za kiume nayo ni pamoja na;
🙆♀️Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P) au ugonjwa wa moyo.
🙆♀️Kuvuta sigala na unywaji wa pombe.
🙆♀️Uzito kupita kiasi na unene uliozidi.
🙆♀️Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi.
🙆♀️Kisukari.
🙆♀️Kuwa na mawazo na wasiwasi.
🙆♀️Matumizi ya madawa mbalimbali.
🙆♀️Umri hasa wazee.
🙆♀️Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili.
🙆♀️Kuwa na tatizo la kibofu.
🙆♀️Tabia za kujichua kwa mda mrefu.
🙆♀️Kutopata usingizi kamili.
🙆♀️Matumizi makubwa ya dawa zenye kemikali za kutibia magonjwa k**a kansa, vidonda vya tumbo, moyo, kisukari, B.P, na magonjwa mengine.
23/11/2022
*Faida za kula papai*
Asili ya mpapai ni Amerika ya Kati na kuanzia kwa matunda, majani na utomvu wa mmea huu hutumiwa kutengenezea dawa maeneo mbalimbali duniani. Vilevile, matunda na utomvu wake hutumika kutengeneza pombe na mvinyo katika baadhi ya nchi, huku wengine wakitumia mpapai kutengenezea dawa kwa ajili ya mifugo na binadamu.
Zifuatazo ni faida za kula papai:
⏺️Papai ni katika matunda yanayoingiza afya sana kwenye mwili wa binadamu. Papai lina vitamin C na vitamini A kwa wingi pia kuna potassium na folate. Pia tafiti zinaonesha kuwa antioxidant aina ya lycopene iliyomo kwenye papai husaidia katika kuzuia kupata saratani.
⏺️Tunda hili pia lina vitamin B, vitamin E na vitamin K. Pia lina madini ya calsium (kashiam) potassium, mgnessium na copper. Pia punje za papai ni dawa kwa baadhi ya matatizo ya ini na figo. Pia kwenye papai kuna protelytic enzymes hii husaidia katika kuuwa bakteria na minyoo pamoja na wadudu wengine hatari ndani ya tumbo (mfumo wa kumeng’enya chakula).
⏺️Papai linatambulika kwa kuwa na uwezo wa kuulinda mwili na maradhi ya uzee k**a macho, misuli na kuzeheka kwa haraka. Ndani ya papai kuna Zeaxanthin hii ni anti oxidant ambayo inakazi ya kuchuja miale hatari ya jua. Pa inaaminika kuwa antioxidant hizi husaidia katika afya ya macho na husaidia katika kudhibiti kudhoofu kwa misuli.
⏺️Vilevile papai huaminika kusaidia kupunguza hatari ya kuwa na ugonjwa wa pumu. Hupunguza hatari ya kuuguwa pumu. Ndani ya papai kuna virutubisho vingi, lakini uwepo wa beta-carotene ndani ya papai husaidia kwa wagonjwa wenye pumu.
⏺️Ulaji wa antioxidanti zilizopo kwenye papai mfano beta-carotene husaidia katika kupunguza athari za kupata maradhi ya saratani kwa vijana. Ulaji wa tunda hili husaidia katika kudhibiti upatikanaji wa saratani ya kwenye via vya uzazi hasa saratani ya korodani.
22/11/2022
*Umuhimu wa kitunguu maji*
Ni aina ya mboga ya yungiyungi na inatajwa kuthibitika kisayansi kuwa na manufaa makubwa sana katika afya ya mwanadamu. Kiungo hicho kimekuwa kikitibu na kuponya maradhi mbalimbali, zifuatazo ni faida zake:
🔘Ina madini ya salfa ambayo ni nzuri hasa kwenye ini na husaidia kuponya kansa kwenye utumbo na kinywa, kutokana na kuwa na virutubisho vingi vya Vitamin C.
🔘Kitunguu maji kinaweza kutengeneza juice na kukikatakata na kisha kukisaga kwa blenda kwa kuchanganya na maji ya kunywa mara unapojisikia vibaya hasa kwa watu ambao wanaosumbuliwa na kifua mara kwa mara.
🔘Piah unaweza kuchanganya na asali na kunywa nayo itakusaidia kwa kiasi kikubwa kutibu maumivu ya tumbo na uvimbe mwilini. Maji ya kitunguu kwa mujibu wa wataalamu wa tiba wanasema yanatibu macho.
🔘Juice yake inauwa vijidudu vya kifua kikuu. Kuna tafiti za kisayansi zinazobainisha kuwa na mchango katika kuwa na uwezo wa kuua vijidudu vinavyosababisha maradhi ya kifua kikuu (baada tu ya mgonjwa kunusa moshi wake).
🔘Kinasaidia tatizo la kukosa haja kubwa huku kikipikwa na kuliwa pamoja na samli, kusaidia kuongeza nguvu za kiume.
🔘Upande wa kinamama, kikitengenezwa supu pamoja na nyama, huongeza hamu ya tendo la ndoa.
21/11/2022
*Umuhimu wa kula karoti*
Mtaalamu wa Lishe kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH), Scholastica Mlinda anasema ulaji wa karoti zinaumuhimu ufuatao:
1️⃣Husaidia kuondoa sumu mwilini na kuongeza kinga ya mwili.
2️⃣Mlinda anasema karoti ina vitamin ambayo husaidia kusafirisha mafuta mwilini na kuboresha afya ya ngozi ya mtumiaji.
3️⃣Pia, ina vitamin A ambayo huboresha uwezo wa kuona na hulinda macho kukumbwa na matatizo yanayotokana na uzee.
4️⃣Karoti ni chanzo kizuri cha nyuzi nyuzi zenye virutubisho ambazo husaidia kumeng’enya chakula na kurahisisha upatikanaji wa haja kubwa.
5️⃣Anasema pia hulikinga tumbo na magonjwa hasa kuzuia saratani ya utumbo na huimarisha afya ya kinywa.
6️⃣Mlinda anasema ulaji wa karoti hufanya kinywa kuwa chenye harufu nzuri na huimarisha fizi zisishambuliwe na magonjwa ya kinywa.
7️⃣“Karoti unaweza kuitengeneza juisi, saladi kwa kuchanganya na matunda, mbogamboga au kachumbari, lakini unaweza kuitumia k**a kiungo katika mapishi yako.” Mbali na faida hizo, anasema kiungo hicho kinapokuwa mwilini husaidia kusaga sumu zilizopo katika ini na kusafisha kibofu.
8️⃣Anasema pia husaidia kudhibiti kiwango cha sukari katika damu kwa kuwa carotenoids iliyopo ndani ya karoti husaidia kudhibiti kiwango cha sukari.
9️⃣Ni muhimu kula karoti katika kila mlo ili kupata kuupa mwili nguvu na kuepuka kupata magonjwa ya kinywa na saratani ya utumbo mpana.
19/11/2022
*Madhara ya PID*
🔘Mimba kutunga nje ya kizazi.
🔘Ugumba.
🔘Maumivu sugu ya nyonga.
🔘Tubo-ovarian abscess. Hii ni kutunga kwa usaha katika via vya uzazi.
19/11/2022
*Je mwanamke huambukizwaje PID?*
Kuna njia kadhaa ambazo mwanamke anaweza kuambukizwa PID. Njia hizo ni pamoja na
✅Kufanya ngono isiyo salama.
✅Maambukizi ya njia ya uzazi hasa kipindi mara baada ya kujifungua (au postpartum period)
✅Maambukizi ya njia ya uzazi mara baada ya kutoa mimba kwa njia zisizo salama (post abortion) au mara baada ya mimba kutoka (miscarriage)
✅Kutumia vipandikizi vya ndani ya mfuko wa uzazi (IUCD) k**a njia mojawapo ya uzazi wa mpango.
✅Kuambukizwa kupitia damu iliyo na vimelea vya PID.
18/11/2022
*Dalili za PID ni zipi?*
Zipo dalili kadhaa za ugonjwa huu wa PID. Miongoni mwa dalili hizi ni :-
✅Mwanamke kuhisi maumivu ya tumbo hasa maeneo ya chini ya kitovu
✅Kupata maumivu ya mgongo.
✅Mwanamke kupata utoko mchafu sehemu za siri. Utoko huu huambatana na harufu mbaya.
✅Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa.
✅Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa.
✅Kutoka damu bila mpangilio wakati wa hedhi.
✅Kupata homa.
✅Wakati fulani kuhisi kichefuchefu na
Pia kutapika.
18/11/2022
🛑 *UJUE UGONJWA WA P.I.D*
Maambukizi katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kitaalamu Pelvic Inflamatory Diseases au kwa kifupi PID, ni moja ya matatizo ambayo huwaathiri sana wanawake. Kwa kawaida maambukizi haya huusisha shingo ya uzazi (cervix) hali ambayo hujulikana k**a cervicitis, nyama ya mfuko wa uzazi (endometrium) ambayo kitaalamu huitwa endometritis, na mirija ya uzazi (fallopian tubes) hali ijulikanayo kitabibu k**a salpingitis.
*_PID husababishwa na nini?_*
Pamoja na aina kadhaa za vimelea kuhusishwa na PID, vimelea vya jamii ya Neisseria Gonorrhoeae pamoja na Chlamydia trachomatis ndivyo vinavyoongoza kwa umaarufu zaidi katika kusababisha PID kwa akina mama.
16/11/2022
*Chanzo cha Arthritis*
Ugonjwa wa arthritis unasababishwa na hitilafu yoyote katika capsule, cartilage na ligaments yaani maungio ya mifupa. Inaweza kuwa gegedu inalika, upungufu wa ukano (synovial fluid), maambukizi ya vijidudu katika moja ya maeneo hayo au mchanganyiko wa matatizo.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Telephone
Website
Address
Tabata