AFYA MTAJI
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from AFYA MTAJI, Health/Beauty, Posta, Tandika.
*YAJUE MATATIZO YA MENO*👇👇👇👇👇👇
Matatizo ya meno ni shida au magonjwa yanayohusiana na meno, karibia matatizo yote ya meno yanatokea baada ya bakteria na wadudu wengine kuwepo mdomoni, hii hufanya mtu kuwa na maumivu makali kwenye meno na mpaka kupelekea kutoa damu au halufu mbaya na kuathiri meno. Matatizo mengi ya meno yanazuirika na hutibika.
watu wengi wanatatizo la meno ila wanatofautiana wengine wanatatizo dogo wengine pia wanatatizo kubwa, tunawashauriwa wawe na tabia ya kuchunguza meno yao ili kujilinda na matatizo ya meno, tibu tatizo mapema ili usikuze tatizo likawa kubwa na tatizo lisipotibwa kwa wakati litakua kubwa na meno yataendelea kuharibika na mtu anaweza kuwa kibogoyo.
*AINA ZA MAGONJWA YA MENO*
Mdomo una magonjwa mengi ila meno ndio tatizo kubwa sana na ndio linaweza kuleta na matatizo mengine, aina za magonjwa ni k**a;
*Meno kutoboka*
– Hili ni tatizo linalotokea kwenye meno kwa kuwepo kwa bakteria kwenye meno na kuharibu meno, bakteria hao wanaweza kutokana na kuwepo kwa mabaki ya vyakula hasa vyenye sukari nyingi. Mabaki yasipoondolewa bakteria huzalisha acidi ambayo ndio huharibu meno na kutengeneza vijitobo.
*Meno kuvunjika*
– Hili ni tatizo ambalo huwatokea watu wakionekana meno yao kuna baadhi na vipande kutoonekana, jino laweza kuwa nusu au robo tatu, mara nyingi hili sio tatizo husababishwa na upungufu wa madini calsium , vitamin D hupelekea fizi kuathirika na linaweza kumnyima mtu uhuru wa kucheka na pia ulimi ukigusa unahisi k**a ni kitu chenye ncha
*Tatizo la fizi*
– Hili ni tatizo katika fizi kuna kuwa na maumivu, k**a vidonda au kutokwa damu, kuwa na usaa au uchafu. Mara nyingi hutokana na bakteria wanaokuwa kwenye mabaki ya chakula usipoyaondoa bakteria wanaanza kuvamia fizi na kuziharibu. Mtu mwenye hili tatizo hutoa harufu mbaya ya kinywaa
*Meno kuharibika*
, – Hili tatizo ni pale meno yanapoonekana sio ya kawaida; yaani yanakuwa yamebadilika rangi, fizi kuharibika, fizi kupungua, fizi kutoka damu na meno kulegea. Hili ni tatizo ambalo laweza kuwa kubwa usipilipatia ufumbuzi mapema
*Meno kufa ganzi*
_ Meno hushindwa kuhisi
– Hili ni tatizo huwakuta wengi katika mazingira ya baridi sana au joto sana, pia wakila baadhi ya vyakula vyenye uchachu, vyenye sukari na vingine. Tatizo hili ni dalili za kuharibika kwa jino ndani au nje
*Harufu mbaya*
– Hili tatizo hutokea kwa mtu kutoa harufu mbaya mdomoni na huwakela watu wengi, hii hutokea pale anavyokuwa na mfumo mbaya wa mmeng'enyo wa chakula na kutofanyia usafi meno na mdomo pia huweza kupelekea tatizo hili
*Mhozo au Utando* mdomoni – Hili ni tatizo ambalo mdomoni huwa na weupeweupe usioeleweka k**a ute, mara nyingi huwatotea watu wasio na kinga imara hasa wenye matatizo ya kiafya k**a kisukari, UKIMWI, Kansa (Saratani), Asthma. Hii hali huondolewa na dawa.
*Meno kuwa na rangi ya njano, kaki au kahawia* – Hili tatizo limeonekana kuchukua baadhi ya maeneo, ambapo idadi kubwa ya watu wameonekana wakiwa na meno yenye rangi inayoendana.
_Hii ni kwasababu ya vyakula na maji ya kunywa yanayopatikana maeneo hayo kuwa na uwingi wa aina flani ya madini hasa Fluoride yanawekwa Katika dawa mbalimbali za meno
*CHANZO CHA MAGONJWA YA MENO*
Chanzo cha magonjwa ya meno kwa asilimia kubwa ni mitindo ya maisha tukimaanisha usafi, ulaji, mazingira na tabia mbalimbali, mambo yanayoweza kukusababishia kupata matatizo ya meno ni k**a;
Kuto kusafisha mdomo pamoja na meno
Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi
Kuto kupata tiba ya kisukari na ugonjwa wa moyo
Kuvuta sigala
Kuwa na magonjwa yanayopunguza kinga ikiwemo na UKIMWI
Kubadilika kwa baadhi ya homoni
Umri
Utumiaji wa madawa yenye kemikali nyingi huharibu mfumo wa vimiminika vinavyofanya mmeng’enyo
Historia magonjwa yanayoambatana na meno katika familia
Mazingira
DALILI ZA MTU MWENYE TATIZO LA MENO
Mara nyingi dalili hujionesha wazi wengi hujijua kuwa tayari wanatatizo na mara nyingi huwa haiitajiki vipimo, zaidi huhitajika uchunguzi kujua chanzo, dalili zake ni k**a
Meno kuuma wakati wa kula au mda wa baridi au joto
Kutokwa na damu kwenye fizi
Meno kuanza kulegea na kuachana na fizi
Kutoa harufu mbaya mdomoni, hii huonesha kuna tatizo
Meno kubadirika rangi mfano nyeusi, njano, kahawia na rangi zingine zisizo za kawaida
Fizi huwa nyekundu k**a damu ikiwezekana kuna na vidonda
Mdomo kuwa mkavu
Meno kufa ganzi
Meno kuchomoka au kutikisika
*JINSI YA KUEPUKA MAGONJWA YA MENO*
Ondoa mabaki ya chakula kwa kusukutua mdomoni na maji baada ya kutoka kula pia Kunywa maji mengi dakika 30 baada ya kutoka kula
Safisha meno yako hata mara mbili kwa siku
Punguza mawazo
Usivute sigara
Punguza au acha kunywa pombe
Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali, vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi
Tatatua tatizo la mfumo wa mmeng'enyo wa chakula
*TIBA YA MATATIZO YA MENO*
Matatizo ya meno linatibika kufuatana na tatizo lenyewe mara nyingi wagonjwa wamekuwa wakizalau dalili za tatizo la meno na kudhani kuwa hakuna madhara makubwa.
Tuna dawa nzuri ya kutibu Meno ambayo ni ya asili isiyo na kemikali ambayo hufanya mtu kupona na kuimarika kabisa. Dawa hiyo hutibu na KUMALIZA tatizo lote
Huondoa chanzo pamoja na ugonjwa sio kituliza maumivu, ukianza kutumia ndani ya muda mfupi huanza kutibu na huonesha mabadiliko, pia utapata ushauri kuhusiana na mfumo wa maisha ambao inatakiwa uutumie kwasababu kuna mtindo wa maisha unaweza kusababisha tatizo kuendea
26/04/2022
Changamoto ya nguvu za kiume hii kiboko yake karibu upate bidhaa bora nicheki whatssap 0688667097.
*MADHARA YA UNENE*
Shirika la Afya Dunia (WHO) limeonya kuhusu ongezeko la watu wenye unene wa kupitiliza huku wakitaja hiyo kuwa ni sababu kuu ya watu wenye changamoto ya nguvu za kiume na maradhi ya *moyo , kisukari na Inni*
Pamoja na watu hawa kuitajika kufanya mazoezi ili kuounguza uzito wa miili yao wataalam wa chakula na lishe wanashauri kufanya mazoezi kula vyakula kulingana na kundi lake la damu na aina ya vyakula vinavyo paswa kula
*NAMNA YA KUPIMA UZITO WAKO*
Je unafahamu BMI yako ?
Body mass Index (BMI) ni kipimo kinacho tumia urefu na uzito wako k**a uzito ni sahihi unao takiwa kiafya
Kujua kupima BMI unacho stahili kuwa nacho unachukua Urefu wako kwa kipimo cha mita unatoa na mia moja
*MADHARA YA KUWA NA UZITO ULIO PITILIZA*
Ukiwa na uzito mkubwa madhara yafuatayo huweza kujitokeza
1_ Matatizo kwenye figo
2_ Uwepo wa michirizi mwilini
3_ Kupunguza hamu ya tendo la ndoa
4_ kuharibu mfumo mzima wa upumuaji
5_ kuharibu Inni
6_ Hupelekea kupata kisukari , tatizo la presha na kwenye guot
7_ Hupelekea changamoto kwenye mfumo wa moyo
8_ Hupelekea kuleta shida kwenye mfumo wa ubongo
9_ Hupunguza kasi ya kuishi
10_ Huleta shida kwenye mmeng'enyo wa chakula
11_ Maumivu kwenye viungo k**a vile magoti na kiuno
12_ Kuongeza kiwango cha mafuta mwilini
K**A UNA SHIDA HIYO NI VIZURI UNIAMBIE ILI TUWEZE KUIONDOA MAPEMA💪💪💪
03/04/2022
*Hello habari za leo ninadawa nzuri itakusaidia kwa wale wenye meno mabovu inasaidia kutoa bacteria wote walioko kwenye meno yalotoboka kung'arisha meno kuzuia harufu katika kinywa inayotoka ndani pia inaalovera kwa wingi karibuni nicheki kwa mawasiliano hapa 0744866392 au 0688667097.*
26/03/2022
Kwa mahitaji ya deodorant safi nicheki 0744866392.
Kila mwanaume anazaliwa na Tezi dume. Tezi dume siyo ugonjwa bali ni kiungo k**a viungo vingine mwilini. Tezi dume inapatikana katika mfumo wa uzazi wa mwanaume katika shingo ya kibofu cha mkojo.
Kazi yake kubwa nikutengeneza majimaji ya uzazi wa mwanaume (shahawa), ambayo husaidia kurutubisha mbegu za kiume zilizo tengenezwa kutoka kwenye Korodani; na husaidia mbegu za kiume kubaki hai kwa muda unaostahili.
Tatizo linakuja kiungo hiki kinapoanza kutanuka. Kiungo hiki kinatanuka taratibu taratibu mnoo. Hili ni tatizo linalo wakumba wanaume wengi. Takwimu zinaonesha kwamba kati ya wanaume 10, wa 5 na kuendelea wana dalili za kutanuka kwa Tezi dume.
Ukuwaji wa Tezi dume ni ile hali ya chembe chembe hai katika tezi ya kiume kukua bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili katika eneo linalo zunguka mirija ya kupitisha mkojo na mbegu za kiume. Tatizo hili kwa sasa linawapata wanaume kuanzia umri wa miaka 25 na kuendelea, tofauti na awali lilikuwa miaka zaidi ya 50.
Takwimu kutoka kwenye shirika la CHRP (Centre for Human Right Promotion), zinaonesha kwamba kiujumla kila mwanaume katika maisha yake ana 16% za kugundulika na saratani ya Tezi Dume, mtu 1 kati ya watu 6 analo hili tatizo; 3% (1 kati 33) wanakufa kwasababu ya Saratani ya Tezi Dume. Saratani hii inaua mwanaume mmoja kila baada ya dakika 13.
a) Dalili za awali
- Kukojoa mkojo uliochanganyikana na damu
- Kukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu
- Maumivu kwenye mfumo wa mkojo
- Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa
- Kuhisi kibofu kimejaa mkojo muda wote na ukienda kukojoa mkojo hautoki, lakini ukirudi kukaa unahisi kukojoa tena.
- Homa
- Kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku
b) Dalili za mtu aliyeathirika
- Maumivu ya mifupa hasa chini ya mgongo, kiuno na mbavu
- Miguu kuwa dhaifu
- Kushindwa kumudu tendo la ndoa, au Kuhisi maumivu makali wakati unamaliza tendo la ndoa
- Kushindwa kuzuia mkojo, pindi unapohisi kukojoa
- Kushindwa kuzuia haja kubwa (kinyesi cha maji maji)
- Tumbo kuja gesi mara kwa mara
* VYANZO VINAVYOPELEKEA TEZI DUME KUTANUKA
Tatizo la kutanuka kwa tezi dume limekuwa kwa kasi sana hii ni kutokana na mitindo ya maisha wanaume wengi wanayoishi. Pia na elimu ndogo iliyoko kwenye jamii kuhusu afya zao.
Vifuatavyo ni vyanzo vya kutanuka kwa tezi dume:
- Ukosefu wa lishe kamili na Virutubisho muhimu mwilini
- Uwepo wa sumu nyingi mwilini
- Kutokufanya mazoezi
- Matumizi ya pombe kali, na uvutaji wa sigara
- Uzito mkubwa (uliopindukia, uliokithiri), na Kitambi
- Kutokukaa sawa kwa vichocheo vya mwili (Hormone Imbalance)
- Msongo wa mawazo (Stress)
- Magonjwa ya zinaa
- Umri mkubwa
- Upasuwaji wa korodani, kuzaliwa na korodani moja,
- Historia ya Familia (Kurithi)
- Mazingira (Ethnicity)
MADHARA YA KUTANUKA TEZI DUME
Katika hatua za awali, tezi inapotanuka hugundulika kwa kupimwa kwa njia ya kidole. Hii ni njia ambayo daktari huingiza kidole kwenye njia ya haja kubwa ili kuweza kubaini k**a tezi imetanuka. Kipimo hiki ndicho rahisi kinacho kubalika duniani kote na kisicho na gharama.
Lakini kimekuwa kikipata upinzani kutoka kwa wanaume kutokana na imani potofu ya wahusika wa tatizo hili kuona ni udhalilishaji.Kipimo kingine ni kipimo cha damu. Damu huchunguzwa aina ya protein inayozailishwa na seli za tezi dume, kiitwacho Prostate Antigen (PSA). PSA huonesha kuwapo kwa tatizo kwenye Tezi Dume, lakini kipimo hiki hakina uwezo wa kutofautisha endapo tatizo hilo linamaanisha saratani.
Yafuatayo ni madhara ya tezi iliyotanuka:
- Kibofu cha mkojo kuuma: hivyo hupelekea mkojo kurudi juu, na kuharibu figo na Ini … … n.k.
- Kufunga kwa njia ya mkojo kabisa
- Figo kushindwa kufanya kazi (Kidney Failure)
- Kushindwa kumudu tendo la ndoa (Ndoa zinavunjika)
- Ugumba (Infertility, Frigidity for men)
- Kutokea kwa majipu sehemu ya Tezi Dume
- Kifo
IV. SULUHISHO KWA TEZI ILIYOTANUKA
a) Suluhisho Linalopendwa
Watu wengi hukimbilia hospitali pindi wanapopatwa na madhara ya Tezi dume na kujikuta wakipewa tiba ambazo huficha tatizo hilo kwa muda mfupi kisha tatizo hujirudia kwa kasi kubwa.
Tezi iliyotanuka haiwezi kutibika kwa njia za madawa yenye makemikali au mitishamba, lakini madawa au upasuaji hupunguza maumivu ya dalili na kuzifanya zisizidi sana.
Kuna njia 3 za kudhibiti Tezi iliyotanuka
1. Kusubiri na kufuatilia kwa ukaribu na Daktari:
2. Madawa
3. Upasuaji
Inashauriwa kwamba kwa tatizo hili ni bora kuendelea kulichunguza bila kukimbilia tiba kali k**a madawa, upasuaji na Tiba kemikali, mpaka pale mtu atakapoona hakuna njia mbadala.
“Baadhi ya madawa wanayopewa wagonjwa wa saratani ya tezi Dume yaligunduliwa miaka 30 iliyopita, yanasababisha athari kwenye Ini, Moyo na kuvimbisha magoti. Yamepigwa marufuku katika Nchi haswa za Ulaya.”
– Johnathon Waxman, Cancer Specialist, Hammer Smith Hospital, London
Njia hii ambayo madaktari hutumia inapelekea “70% ya wagonjwa kuwa mahanithi baada ya upasuaji, na 40% wanashindwa kuzuia mkojo kutoka wanapo banwa na haja ndogo.”
– Johnathon Waxman
Inasikitisha kuona wanaume wanapasuliwa bila uhakika wowote kwamba huo upasuaji utakuwa na manufaa.
b) Suluhisho la kudumu (Bora)
1. Kula mboga mboga na matunda kwa wingi kulingana na kundi la damu yako.
2. Punguza au acha kuvuta sigara
3. Punguza au acha utumiaji wa pombe kali.
4. Punguza kukaa masa nane kwa siku.Fanya mazoezi kwa wingi.(Sitting is a new smoking)
5. Kutovaa nguo za kubana
6. Vaa chupi za cotton na sio material yeyote.
7. Kuhakikisha Uume uwe una erect mara kwa mara
8.Na cha mwisho ambacho ni muhimu kuliko vyote ni utumiaji wa virutubisho (supplements).Tezi Dume inatanuka kwasababu ya upungufu wa madini na virutubisho mwiliunavyohitaji.
Kwa watu wenye changamoto hii ya kutanuka kwa Tezi Dume, na mfumo wa uzazi mwanaume, Kampuni tumewaandalia program ya lishe kamili na virutubisho muhimu. Bidhaa hizi ni vyakula, siyo dawa wala mitishamba. Zimetengenezwa kutoka kwenye vyakula ambavyo tungefaa kula kila siku, na vina lishe kamili na virutubisho muhimu katika miili yetu inavyo hitaji ili iweze kutengeneza yenyewe afya bora na nadhifu.
Hizo bidhaa zina mchanganyiko wa vitu vifuatavyo: Proteins, Vitamins, Minerals, Essential Fat Acid and Trace minerals.Pia Program zetu za lishe zimethibitishwa na mashirika ya kuthibiti ubora wa viwango vya bidhaa duniani. Na kwa hapa Tanzania, zimethibitshwa na mamlaka ya chakula na madawa (TFDA)
Kwa yeyote anayehitaji hii program ya kuboresha na ushauri wa kuimarisha afya yake ya Tezi Dume (Prostate Gland) na mfumo mzima wa uzazi wa mwaume tucheki 0744866392.
21/03/2022
MADHARA YA KUTUMIA VIDONGE VYA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME (VIAGRA/VEGA)
Hivi ni vidonge vinavyotumiwa sana na miongoni ya wanaume au vijana wengi kwa lengo la kuongeza uwezo wao wa kufanya mapenzi. Dawa hizi hutumiwa zaidi na wanaume wasioweza kusimamisha uume vizuri(low libido) kwa leo la kumuwezesha kukidhi haja zake au za mwenza wake wa k**e. Lakini pia zimekuwa zikitumiwa na vijana wengi kwa lengo la kumkomoa mwanamke au wengine hufanya kwa kuiga kutoka kwa waigizaji video za ngono(pornograph). Madhara ya vidonge hivi ni mengi, leo tutayajua
JINSI VINAVYOFANYA KAZI
Vi**ra haimfanyi mtu kupata hamu ya ngono bali yenyewe hufanya kazi endapo tu mtu atakuwa na hamu ya kufanya ngono. Hebu tugusie kidogo kuhusu uume unavyoweza kusimama.
Pindi mwanaume anapopata hamu ya kufanya ngono, mishipa ya fahamu iliyoko katika misuli ya uume hutoa chemicals zinazoitwa "nitric oxide" ambayo huamrisha viamshi(enzymes) kuzalisha chemicals nyingine tena zinazoitwa "messenger cyclic guanoside monophosphate". Hali hii huifanya misuli laini ya uume kujiachia na kutanuka ambapo matokeo yake huiruhusu damu kuingia na kujaa vizuri katika mishipa midogomidogo iliyoko katika uume(cappilaries), hapo ndipo uume unakuwa umesimama vizuri.
Hivyo basi, Vi**ra hufanya kazi ya kusawazisha kiwango cha hii kemikali inayoitwa Cyclic guanosine Monophosphate.
SASA TUONE MADHARA YA VIDONGE HIVYO
Kwa mara ya kwanza dawa hii ilitumika kutibu tatizo la Presha, lakini ilionyesha maajabu pale ilipooneka kuwafanya wagonjwa kuwa na nguvu nyingi za kusimamisha maumbile yao ya uzazi. Baada ya hapo zikazuiliwa kutumika mahospitalini lakini baadae zikafanyiwa uchunguzi na zikaanza rasmi kutumika kwa wanaume wenye matatizo ya kusimamisha. Kipindi hicho watu wenye matatizo ya kusimamisha walikuwa wakipewa dawa hii chini ya uangalizi wa Daktari huku wakipewa ushauri wa kutosha kwamba wataweza kusimamisha na hivyo Saikolojia hiyo ikawakaa na wakasimamisha, lakini baada ya muda fulani, mgonjwa wa tatizo hurudi katika hali yake ya kutosimamisha.
MADHARA
=>Mtu anayetumia vidonge hivi bila usha wa Daktari huku akiwa na matatizo mengine ya Kiafya k**a Presha yuko hatarini kupoteza uhai wake.
=>Matumizi makubwa ya dawa hizi hufanya tatizo kuwa kubwa zaidi kwa sababu dawa hizi humfanya mtu kusimamisha kwa muda tu kwani akihitaji kufanya mapenzi siku nyingine inampasa ameze tena. Hali hii ya kuzimeza kila wake inamfanya kuwa dependant(tegemezi) na kumfanya azidi kuongeza dozi zingine na mwiso wa siku hutengeneza sumu mwilini na kuua kabisa nguvu za kiume.
=>Madhara mengine ni kupoteza uwezo wa kusikia(ukiziwi) pamoja na kupoteza uwezo wa kuona,,,,
JE UNASUMBULIWA NA TATIZO LA KINYWA KUTOA HARUFU MBAYA NA MENO KUTOBOKA!
SOMA HAPA UJIFUNZE!
Harufu mbaya mdomoni huathiri maisha ya mtu kimahusiano katika jamii sio katika mapenzi tuu Ila hata kwa ndugu na jamaa.
Mara nyingi tatizo hili humpata mtu pasipo yeye kujijua mpaka pale atakapoambiwa au atakapoamua kujitambua k**a anatoa harufu au la.
Tafiti zinaonesha kwamba zaidi ya asilimia 85% ya watu wenye tatizo hili chanzo chake ni kinywa chenyewe na 15% ni vyanzo vingine.
Pia hueleza kuwa harufu hii hutofautiana kwa muda yaani asubuhi mchana na usiku.
SABABU ZA HARUFU MBAYA MDOMONI .Kutokufanya usafi wa kinywa yaani kupiga mswaki vizuri hali ambayo hupelekea mabaki hayo kuoza na kuleta harufu mbaya mdomoni.Uvutaji wa sigaraMpangilio wa meno katika kinywa ambao hupelekea kuwepo kwa mabaki ya chakula katika kinywa na hivyo kuleta harufu mbaya mdomoni.Kuwepo kwa bacteria katika jino lililotoboka na hivyo hupelekea kutoa harufu. Pia inasemekana kuwepo na zaidi ya aina nyingi zaidi ya bacteria katika kinywa wanaopatikana katika ulimi,fizi, na kuzunguka meno.Kulala mdomo wazi hali ambayo hupelekea tabaka la juu la mdomo kuoza na hupelekea mdomo kutoa harufu mbaya.Matumizi ya pombe na vitu vyenye sukari sana kwa mda mrefu pia hupelekea kuwepo kwa harufu mbaya mdomoni.Pia athari ya magonjwa mengine k**a vile magonjwa ya fizi kutoa damu, kisukari, n.k
JINSI YA KUJITAMBUA
Wanasayansi wanakiri kwamba ni vigumu sana kwa mtu kufahamu kwamba anaharufu mbaya lakini ni rahisi sana kutambua harufu inayotoka katika kinywa cha mtu mwingine
Hivyo unaweza tambua harufu mbaya kwa kumwuliza mtu unayemwamini.Wengine hupumua mbele ya kiooKwa kulamba nyuma ya kiganja na kunusa.Pia unaweza kutumia kijiti cha kuchokonolea meno na kukinusa.Kisayansi unaweza kutumia vifaa k**a vile Halimeter Gas Chromatography and BANA test.
TIBA YAKE
Kutokana na tatizo hili kuwa kubwa tafiti zimefanyika na kuweza kutengeneza dawa ambayo zinauwezo wa kuondoa tatizo hilo kwa mtumiaji wa dawa hizo na hutumiwa na watu wa rika zote yaani Watoto, watu wazima na wazee pasipokuwa na athari yoyote kwa mtumiaji kwani bidhaa hii haina kemikali ndani yake.
FAIDA ZA BIDHAA HII
Humsaidia mtumiaji kusafisha meno na kung'arisha pasipo kuchuna tambala la juu la meno.(ENEMEL)Humsaidia mtumiaji kuondoa bacteria wanaopatikana katika kinywa yaani katika ulimi, fizi na kuzunguka meno.Hupenya katika matundu yote ya meno wakati wa kutumia na kuponya vidonda vya mdomoni.Huimarisha fizi na kwa mtu mwenye matatizo ya meno kuchimbika au kuwa na matobo hii ni tiba tosha kwake.
Kwa maelekezo zaidi kuhusu bidhaa hizi
Comment namba zako hapo tutawasiliana nawe au
WASILIANA NASI KWA NAMBA
0744866392 &0688667097..............................
WhatsApp/calls and text
16/03/2022
UGONJWA WA BAWASIRI
( HEMORRHOIDS)
MIWASHO, MAUMIVU NA VIMBE KATIKA TUNDU LA HAJA KUBWA
Bawasiri ni ugonjwa ambao unatokana na kuathirika kwa mishipa ya sehemu ya ndani na nje ya tundu la haja kubwa na hupelekea wakati mwingine kutoa damu wakati wa kutoa haja kubwa.
Ugonjwa huu unasababisha muwasho na maumivu makali katika tundu la haja kubwa.
Mara nyingi tatizo hili huwapata watu kuanzia umri wa miaka 25 – 70.
Ila kwasasa ugonjwa huu unawaathiri mpaka watoto wa umri wa chini kabisa:
Kuna aina mbili za bawasiri:
Bawasiri ya Ndani:
Hiki nikinyama kinachootea ndani kabla ya Kutokea nje
Huanza kwa mtu kukosa choo, Maumivu wakati wa kujisaidia
Pia uvimbe huanza kujitengeneza kwa kutoka ndani ya tundu la haja kubwa hasa pale wakati wa kujisaidia
Bawasiri ya Nje:
Hii ni Bawasiri ambayo hujitokeza sehemu ya nje ya tundu la haja kubwa. Hutokea nje baada ya bawasiri ya ndani kujiimarisha zaidi,
Wapo watu ambao huathirika nje moja kwa moja na hutegemea ni chanzo gani ambacho kimepelekea kuathirika na tatizo hilo.
Huambatana na Miwasho ya mara kwa mara, Maumivu katika sehemu ya nje ya tundu la haja kubwa, Damu kutoka wakati wa kujisaidia na baada ya kujisaidia
II.CHANZO CHA UGONJWA WA BAWASIRI.
Bawasiri ni tatizo linaloanzia kwenye mfumo wa mmeng'enyo wa chakula. Huu mfumo ukishakua mbovu hupelekea kutokupata choo vizuri(Haja kubwa)
Mfumo mbovu wa mmeng'enyo wa chakula unasababisha chakula kisimeng'enywe vizuri kwenye utumbo mdogo na hivyo kupelekea chakula kupiliza kwenda moja kwa moja k**a kilivyo kwenda kwenye utumbo mkubwa ambapo maji maji kutoka kwenye chakula hufyonzwa na kuacha chakula kikiwa kikavu.Inapofikia wakati wa kupata choo; choo kinakua kikavu hivyo unatumia nguvu nyingi kukisukuma choo kitoke.
Hali hii hupelekea misuli ya haja kubwa kutanuka na kupelekea kukwanguliwa na choo kigumu na hivyo kinyama kuanza kujitengeneza, Hivyo husababisha kuanza kusikia maumivu na miwasho kwa ndani, na mara nyingine kupata choo chenye damu.
Hivyo basi kadri unavyoendelea kupata choo kigumu misuli ya tundu la haja kubwa huendelea kuathirika zaidi k mpaka kinatokeza.
Mtu mwenye afya nzuri anapata choo kulingana na milo aliopata kwa siku. K**a unauwezo wakupata milo mitatu kwa siku, unasitahili kupata choo mara tatu kwa siku, tena choo chako kitoke na urefu sawa wa ndizi mbivu, bila kujikatakata k**a kile cha mbuzi.
Bawasiri pia huweza kusababishwa na:
-Kufanya mapenzi kinyume na maumbile,
- Ujauzito
- kuhara kwa mda mrefu
-Kutopata choo kwa mda mrefu
III. DALILI ZA UGONJWA WA BAWASIRI
- Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa. Huu muasho unakuja kwa kujirudia mara kwa mara baada ya muda furani.
- Kukatishwa kwa haja kubwa na kurudi ndani wakati wa kujisaidia. Kitendo hiki huongeza msuguano katika mishipa ya ndani ya tundu la haja kubwa.
- Kujitokeza kwa uvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa. Uvimbe huu unaanza kuota k**a upele na huambatana na miwasho na maumivu makali.
- Kujitokezea kwa kijinyama katika tundu la haja kubwa. Kinyama hiki kinaanzia ndani ya tundu la haja kubwa na kutokea nje ya Tundu la haja kubwa. Hatua hii huashiria tatizo limesha kuwa kubwa na una hili tatizo la bawasili kwa muda mrefu, na linaweza kusababisha vifo vya gafla kwa sababu mishipa inayosafirisha damu ndio inakwanguliwa na mwishowe kuathirika.
Chukua tahadhari mapema kabla hujaathirika sana au upoteze maisha; kwasababu hiki ni chanzo cha kupatwa na magonjwa mengine mengi ya kiafya.
- Kujisaidia kinyesi chenye damu na kunuka kwa harufu mbaya sana
- Kupumua na kushindwa kuzuia kinyesi wakati ukipumua(kujamba na kutoa haja kubwa)
IV. MADHARA YA UGONJWA WA BAWASIRI
Upungufu wa damu mwilini
Kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa na kusababisha mishipa ya sehemu ya haja kubwa kukwanguliwa.
Kuna uwezekano mkubwa wa kupata saratani ya utumbo (Cancer) kwasababu kile kinyama kinakaa k**a kidonda
Kutopata hamu ya tendo la ndoa kwa jinsia zote. Yaani Mwanamke na Mwanaume.
Kuathirika kisaikolojia na hupelekea kuptojiamini katika hadhara ya watu hasa pale miwasho inapoanza.
Kuvuja damu, maumivu ya mda mrefu na hupelekea kushindwa kukaa.
Maumivu ya mgongo ya mara kwa mara na kiuno.
V. JINSI YA KUDHIBITI TATIZO HILI LA BAWASIRI (HEMORHOIDS ) KABLA HALIJAKUPATA
Jitahidi kupata mlo kamili kila siku. Tutumia matunda na mboga za majani kwa wingi (kila mlo).Kunywa maji ya kutosha. Angalau lita 3 kwa siku.Epuka kukaa chooni kwa mda mrefu
Jiepushe na vilevi
Usiwe mpenzi wavitu vya viwandaniJenga utaratibu wa kusafisha mwili wako kwakutumia Cleansing Program, ili utoe taka mwili zote, na uondoe sumu mwilini; k**a vile unavyooga zaidi ya mara mbili kwa siku. (Wasiliana na si kwauhitaji wa program ya kusafisha mwili, kuondoa sumu na kupunguza mafuta mwilini)
VI. NJIA ZAKUONDOA TATIZO HILI
a. Tiba yake hospitalini Ugonjwa huu tiba yake ni opereation (kukukata uvimbe uliojitokeza katika tundu la haja kubwa ili usiendelee kukua na kusababisha magonjwa mengine.
Tiba hii huwa na Changamoto ya kujirudia tena kwa hilo tatizo baada ya mda fulani hasa pale mgonjwa akosapo kinga tosha mwilini.
Pia hupelekea maumivu makali kwa mgonjwa na kutokwa damu kwa mda mrefu hasa wakati wa kujisaidia na mara baada ya kujisaidia,
Tiba hii huondoa uvimbe pekee na haiboreshi mfumo wa chakula kuanzia ndani ambako ndo hasa chanzo cha Tatizo hili na kupelekea
baadae tatizo hili kujirudia tena.
SULUHISHO LA UGONJWA HUU NA LA KUDUMU.
Tiba nzuri ni kutumia lishe na virutubisho (mwili utajitengenezea kinga bora tena yakudumu)
Tiba nzuri ni kuanda utaratibu wa kusafisha mfumo wako mzima wa mumeng’enyo wa chakula (Digestive System) kwa kuulisha mwili Virutubisho muhimu.
Chanzo cha magonjwa yote tunayoyapata Hasa huu wa BAWASIRI hutokana na mfumo mbovu wa mumeng’enyo wa chakula,
mzunguko wa damu (Poor Blood Circulation) na Mwili kuwa na sumu nyingi. Kila siku tunaoga zaidi ya mara mbili au mara tatu kwa siku nje ya mwili wetu, Vivyo hivyo tunapaswa kuanda utaratibu wakusafisha mili yetu ndani ya miili yetu na kuhakikisha sehemu kuu tatu za mili yetu zinafanya kazi vizuri.
Hivyo ipo Programu maalumu ambayo husaudia katika kuboresha afya kuanzia ndani na kuondoa changamoto hii ya Bawasiri ya ndani.
Programu hii husaidia katika kuondoa vimbe za ndani na kuboresha upataji wa choo laini,
Husaidia kuondoa upataji choo ngumu na uvimbe kwa upande wa ndani.
Lakini pia program hiyo ina tube maalumu za kupaka ambazo husaidia katika Kuondoa vimbe za nje ya tundu la haja kubwa.
Pia husaidia katika kuondokana na maumivu, miwasho na kulainisha na kuondoa uvimbe uliojitokeza katika tundu la haja kubwa.
VII. Umuhimu wa programu hii katika kuboresha na kuimarisha afya yako.
1. Digestive System (Mfumo mzima wa mumeng’enyo wa chakula)
2. Blood Circulation (Mfumo mzima wa mzunguko wa damu)
3: Kuboresha kinga ya mwili na kuongeza virutubisho muhimu mwilini.
Programu hii hujumuisha Virutubisho vyenye Carbohydrates & Proteins, Vitamins & Mineral, Essential Fatty Acids, Trace Elements. Miili yetu huhitaji kuvipata ili uzidi kutengenza kinga ya mwili kwajili ya kuondokana na Ugonjwa huu.
Programu hii
imeandaliwa kitaalamu zaidi na hazina kemikali yenye madhara kwa mtumiaji
BAWASIRI NI UGONJWA HATARI K**A HUTOUCHUKULIA HATUA YA TIBA MAPEMA. Kwamawasiliano 0744866392.
11/03/2022
✓Kuongeza hamu ya kula(appetite).
✓Kuongeza kinga ya mwili.
✓Kuondoa sumu mwilini (free radicals)
✓Kuboresho mmeng'enyo wa chakula.
✓Kusaidia tatizo la kutopata choo kwa watoto.
✓Huboresha macho na kusaidia kuona vizuri mchana na usiku.
✓Kumwepusha mtoto na maradhi mbalimbali.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Website
Address
Posta
Tandika