Seiph wa KO

Seiph wa KO

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Seiph wa KO, Health/Beauty, Tanga.

12/04/2026

WANANGU

Njaa haitangazi inakuja kimya kimya, Njaa haina ego lakini inakuambia ukweli mmoja hakuna anayekuja kukuokoa amka pigana🫡

Mwanangu najua Macho yamefunguka lakini Maisha Bado yamelala, wanasema hasiyefanya kazi na hasile, acha kuona aibu fanya kazi yoyote halali👊🏿

Najua mikono hipo hai lakini haina pakushika, ndoto kichwani lakini mifuko ni k**a jangwa bila mvua ila amka pigana👣

Mtandaoni kila mtu ni Tajiri, Kila mtu anayo stori ya mafanikio lakini hawatuambii kuhusu usiku waliolala njaa wala asubuhi ya kuamka bila matumaini🤔

Maisha sio shamba la Bibi hauvuni bila kulima na ukingoja bahati utazeeka ukisubiri upepo hubadili mwelekeo🚮

Mwanangu sikiliza Njaa uliyonayo sio Laana ni kingereza ni sauti inayokwambia amka, pigana na tafuta njia💪🏿

Leo unaweza ukawa hauna kitu lakini ukikataa kukata tamaa, kesho itakuogopa husisubiri Maisha yakutafutie njia kuwa njia, Kwasababu ukweli ni huu hakuna anayekuja na muda haukawii🫶🏿

25/03/2026

BRO TO BRO

K**a unafikiri hii Dunia ni tamu kwa Mwanaume, unajidanganya kuwa makini wasije waharibifu wakapita mlango wa nyuma👣

Dunia inamtambua Mwanaume k**a shujaa ukiona unataka kila unachosukuma kinakuwa laini tu, angalia tsije kubaki pungufu💪🏿

Hata maandiko yanasema tutakula kwa jasho na ndio utamaduni, Hata yule mwenye vya kurithi inabidi atulize akili ili ale vizuri🔨

Sipo hapa kukwambia unatakiwa kuteseka kwenye kila hatua zako, ila nakukumbusha ukihisi unataka kukata tamaa kumbuka wewe ni Mwanaume🙏🏿

Kanuni ni ile ile Mwanaume hatii huruma anatia aibu, Tengeneza njia zako na pambania ndoto zako, tutakusifia ukifika kwenye Matokeo kusifiwa kwenye mchakato sio sifa ya Mwanaume👊🏿

Mwanaume na Dunia🤝

21/03/2026

Nawatakia Eid Mubarak🎉

08/02/2026

BRO TO BRO

Jitahidi kuishi Maisha yenye uhalisia wako na kutosahau ulipotoka!

Kamwe usidhani wewe ni wa pekee na hauwezi kuguswa, Maisha hayana Kanuni leo juu kesho chini!

Ugonjwa unaweza kukuangusha, kifo kikagonga bila hodi, kazi ukapoteza ghafla, pesa ikakauka na wale uliowazoea wakakushusha thamani!

Sekunde tu kila kitu kikabadilika, meza ikapinduka, marafiki wakageuka wageni na mwisho ukabaki pekee yako!

Jenga nidhamu, heshima na kuwa mnyenyekevu na mwisho tambua sio kila shimo unamwaga mbolea!

Fanya ibada bila kuchoka, shukuru ukiwa juu na hata ukiwa chini, usijisahau na usidharau wengine!

Photos from Seiph wa KO's post 04/02/2026

Shukrani

ya hifadhi ya wanyamapori uyumbu

Ushirikishwaji wa jamii katika uhifadhi wa hifadhi ya wanyamapori ni muhimu kwaajili ya vizazi vya Leo na Vinavyokuja

(Facebook).

04/02/2026

*SIKU YA SARATANI DUNIANI*
*SARATANI - KANSA*

Je unajua saratani husababisha vifo takribani Million 12 Kila mwaka na idadi hiyo ni wengi zaidi kuliko jumla ya wote wanaokufa kwa Ukimwi, Malaria na Kifua kikuu🫳🏿

Je unajua ulaji usiofaa, kutoshughulisha mwili na matumizi ya pombe na tumbaku uchangia Magonjwa ya saratani🤔

Je unajua saratani ya mlango wa kizazi uchangiwa na Tabia hatarishi k**a vile: Kuanza ngono mapema -18, uvutaji wa sigara na tumbaku, kuwa na wapenzi wengi n.k🙌🏿

Je unajua Saratani ya Mlango wa kizazi husababishwa na kirusi kinachoitwa Human papilloma, Kirusi hiki huambukizwa kwa njia ya kujamiiana na mtu mwenye virusi hivyo🦶🏿

👌🏿
🤝

Photos from Seiph wa KO's post 25/01/2026

IRENTE - LUSHOTO
24.1.2026

Ulikuwa wakati mzuri k**a vijana tulipopata nafasi ya kutembelea vitu viwili vya watoto wenye uhitaji IRENTE - LUSHOTO

Sambamba na kupata wasaa wakutalii IRENTE VIEW POINT🙏

KOROGWE YOUTH GROUP x IRENTE LUSHOTO

10/01/2026

Mwandishi Mark Manson kupitia Kitabu chake cha "The subtle art of not giving a f**k:

Anamzungumia mtu mmoja anayejulikana k**a "Jimmy the Delusional: si kwa sababu ana ndoto kubwa, Bali kwa sababu haiwezi kukubali mapungufu na hali halisi ya Maisha🙌

Anajiamini sana, anajikubali sana na anapenda kuonekana k**a mtu aliyefanikiwa kwa sababu ni mtu anayejali sana alikuwa na Imani kubwa sana juu ya mafanikio lakini hakuwa na maarifa, ujuzi na juhudi za kweli🫳🏿

Jimmy the Delusional: Aliishi katika dunia ya ndoto na kujidanganya kwamba atafanikiwa bila kufanya au kukubali ukweli wa Maisha👣

Mark Manson: Anamtumia Jimmy the Delusional k**a mtu ambaye anatoa vipaumbele kwenye mambo yasiyo na msingi, anajali zaidi anavyoonekana kuliko ukweli wa Maisha yake👌🏿

Mwandishi anatukumbusha kuchagua kwa makini ni mambo gani ya kujali na kukubali ukweli wa Maisha ili kuweza kukua na kuwa mtu bora na mwenye afya imara ya akili🚮

08/01/2026

HERI YA MWAKA MPYA 2026

Tunapouanza mwaka mpya k**a jukwaa la AKILI PLATFORM TANZANIA mkoa wa TANGA tunapenda Kuwatakia heri na baraka tele tunapouingia mwaka huu 2026

Tuendelee kukumbushana kuhusu AFYA YA AKILI na CHANGAMOTO ZAKE k**a jamii Kila mtu anayo nafasi ya kutoa kile alichobarikiwa kwenye jamii inayonzunguka iwe ni Elimu au kusaidia watu wenye changamoto mbalimbali za akili, tuendelee kukumbushana changamoto za akili zipo na ndio sababu kuu ya vijana wengi kujitoa akili na kubwa zaidi tukumbushana k**a watu wenye malengo au matamanio makubwa kwenye Maisha kwamba inatupaswa kuweka malengo yanayofikika na pia kuweka kiasi kwenye Kila matamanio yako au malengo yako 2026 hili kuepukana na changamoto za akili!!!

AKILI PLATFORM TANZANIA tupo kwaajili yako tupo kwaajili ya kutengeneza jamii imara Leo na kesho itakayoweza kuepukana na changamoto za akili!!!

PLATFORM TANZANIA
YA AKILI
#2026

Photos from Seiph wa KO's post 06/01/2026

TAREHE 3.01. 2026

BONANZA LA VIJANA - MPIRA WA MIGUU KATA YA MAJENGO - KOROGWE MJINI🔥

Hongereni sana MAJENGO YOUTHS kwa kuibuka na ushindi wa GOLI 4 -2🔥🔥🔥

Wahenga wamekimbizwa hawaamini macho yao😀

Rasmi tumeuanza mwaka 2026 kwa kukutana pamoja uwanjani tukashuhudia burudani na Kupata muda wa kufurahi na kupiga stori kadhaa🙏🏿

Mungu awabariki sana Ndugu zangu tulioshiriki BONANZA hili Kwani linaendelea kujenga upendo na mshik**ano miongoni mwetu k**a vijana k**a vijana wa Kata ya Majengo Korogwe Mjini🙏🏿

Kwa kipekee namshukuru Mwenyekiti wa Vijana (W) Dr Birumo @⁨BiruMO MKT UVCCM (W)⁩ kwa kuwa nasi vijana wa KATA YA MAJENGO hasa sisi tunaopenda MPIRA WA MIGUU, umekuja kutupa GOLI BORA LA MECHI🙌🏿

Huu ni mwanzo tu k**a kijana mwenzenu na kiongozi ni waahidi tutafanya kila sikukuu Kadri mungu atakapotupa kibali Cha uhai🤲🏿

Acha Boli itembeeeeee🫳🏿
Majengoooo🔥

26/12/2025

Kumbukumbu🙏🏿

Ni kitu cha ajabu sana, Kuna siku tunacheka kwa kukumbuka siku tulizolia🙌🏿

Na Kuna siku tunalia kwa kukumbuka siku tulizocheka🤔

Photos from Seiph wa KO's post 20/12/2025

*Tunapoelekea mwisho wa mwaka* 👊🏿

Kwangu, *2025* itabaki kuwa mwaka wangu bora kwa kuendelea kugusa vijana wenzangu, hasa makundi mbalimbali ya kijamii na wanafunzi wa shule za msingi.

Kupitia majukwaa hayo, nimeendelea kutoa elimu kwa vijana wenzangu kuhusu *afya ya akili na changamoto zake*, *ukatili wa kijinsia na dhidi ya watoto*, na *elimu dhidi ya magonjwa yanayoambukiza*.

Jamii yetu kwa sasa inakumbwa na ongezeko la *vijana wengi kujikatisha uhai* kutokana na changamoto za kimaisha, familia, mapenzi, kazi, na namna ya kuigawa furaha 🤔

Tunaendelea kukumbushana k**a vijana — na hazina muhimu ya taifa hili — kuendelea kupambana na kujitafutia kesho bora. Ila, kwenye mapambano yetu tusisahau kuweka kiasi na kupunguza matamanio yasiyofikika au yaliyo nje ya uwezo wetu 🙏🏿





#2025 🙏🏿

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Tanga?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Culinary Team

Attire

Telephone

Website

Address


Tanga
ECKENFORDE