Jifunze NASI
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Jifunze NASI, Health/Beauty, Ud, Temeke.
:
1. Ujumbe wa mwisho wa Mungu ni wito wa kumwabudu Muumbaji.
π Ufunuo 14:6β7 β Malaika wa kwanza anatangaza injili ya milele na kuwaita wanadamu wote βmsujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji.β
2. Sabato ni kumbukumbu ya uumbaji wa Mungu.
π Kutoka 20:8β11 β Mungu aliagiza watu wake kuikumbuka siku ya Sabato kwa sababu βkwa siku sita Bwana alizifanya mbingu na nchiβ¦ akastarehe siku ya saba.β
3. Sabato iliwekwa tangu uumbaji wa dunia.
π Mwanzo 2:1β3 β Mungu alipumzika siku ya saba, akaibariki na kuitakasa.
4. Sabato ilitolewa kwa wanadamu wote, si kwa Wayahudi pekee.
π Marko 2:27β28 β βSabato ilifanywa kwa ajili ya mwanadamu, wala si mwanadamu kwa ajili ya Sabato.β
5. Sabato ni ishara kati ya Mungu na watu wake.
π Ezekieli 20:12, 20 β Mungu anasema Sabato ni ishara ya kutambua kuwa Yeye ndiye anayewatakasa watu wake.
6. Yesu Kristo ndiye aliyeshiriki katika uumbaji.
π Waefeso 3:9 (pia soma Yohana 1:1β3; Wakolosai 1:16) β Vitu vyote viliumbwa kupitia Kristo.
β‘οΈ Hivyo wito wa kumwabudu Muumbaji ni wito wa kumheshimu Yesu.
7. Yesu mwenyewe alishika Sabato kwa uaminifu.
π Luka 4:16 β K**a ilivyokuwa desturi yake, Yesu aliingia katika sinagogi siku ya Sabato.
8. Yesu alionyesha Sabato ingeendelea hata baada ya kifo chake.
π Mathayo 24:20 β Aliwaambia wanafunzi waombe ili kukimbia kwao kusitokee wakati wa Sabato wakati wa kuangamizwa kwa Yerusalemu (mwaka 70 B.K.).
9. Mitume waliendelea kuishika Sabato baada ya ufufuo wa Yesu.
π Matendo 13:42β44 β Wayahudi na watu wa mataifa walikusanyika siku ya Sabato kusikiliza Neno la Mungu.
π Matendo 16:13 β Paulo alikutana na waumini siku ya Sabato mahali pa kusali.
10. Yesu ni Bwana wa Sabato.
π Mathayo 12:8; Marko 2:28; Luka 6:5 β βMwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.β
11. Biblia inaonyesha wazi siku ya Sabato ni ipi.
π Luka 23:54β56; 24:1
03/03/2026
Uso uliong'aa #Melody of Angels Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.
03/03/2026
Melodies of Angels~Mkwezi girls secondary Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.
SALA YA BWANA. (Namna inavyoombwa)
Sala ya Bwana ni sala ambayo Bwana wetu Yesu Kristo aliwafundisha wanafunzi wake, kabla ya kuondoka kwake. Na kwa kupita sala ile, hakuwafundisha tu wanafunzi wake bali alitufundisha na sisi pia, maana yake ni kwamba, nasi pia tunapaswa tuombe k**a vile Bwana alivyowaelekeza wanafunzi wake.
Lakini ni muhimu kuielewa sala hii kwa mapana, ili kusudi tuisikose shabaha tunapoomba.. Kwa maana tusipoielewa vizuri basi tutajikuta tunaifanya k**a Mashairi (kwa kuirudia rudia k**a watu wa mataifa, wanavyofanya wanapoiomba miungu yao).. Sisi biblia imetuambia tusifanane na hao.(Mathayo 6:7).
Sasa sala ya Bwana Imegawanyika katika vipengele vikuu nane (8).. Na vipengele hivyo sio sala yenyewe bali ni k**a βmaelekezo ya salaβ. Sala yenyewe hatuwezi kuandikiwa, bali tunaomba kila mtu kulingana na anavyoongozwa au kujaliwa na Roho Mtakatifu.
Ni sawa mtu akupe vipengele saba vya kuombea, akakuambia ombea Familia, ombea Taifa, ombea Kanisa, ombea Marafiki.. Sasa kwa kukwambia hivyo huwezi kwenda kupiga magoti na kusema naombea Taifa, kanisa, ndugu na marafiki halafu basi uwe umemaliza!, Huwezi kufanya hivyo.. bali utakachofanya ni kuzama ndani kwa kila kipengele kukiombea..
Kwamfano Katika kipengele cha kuombea Taifa utaombea Viongozi wote na Hali, na hali ya Taifa, na ya Imani kwa ujumla katika Taifa zima, jambo ambalo linaweza kuchukua dakika kadhaa au masaa kadhaa, vile vile katika Familia, na katika kanisa utafanya hivyo hivyo..zitahitajika dakika nyingi kwasababu kuna watu wengi katika familia, na kuna matatizo mengi ambayo ukianza kuyataja mbele za Mungu, huenda yakachukua dakika nyingi au masaa mengi.. Hivyo kwa vipengele tu hivyo vichache unaweza kujikuta unasali hata masaa 6.
Vile vile katika sala ya Bwana, ni hivyo hivyo, vile alivyoviorodhesha Bwana ni vipengele tu, na sio sala yenyewe, maana yake Mitume hawakuchukua hiyo sala na kuikariri k**a shairi na kisha kuirudia rudia kila wakati kabla na baada ya kulala, k**a inavyozoel
"Mwenyezi Mungu ndiye taa na Nuru ing'aayo gizani"
asili ya Giza Ni mtu kushindwa kuona Chochote kinachomzumzunguka haijalishi Ni kibaya au kizuri. hivyo huwezi kutembea, kushika, au kufanya Chochote kwa Uhuru ukiwa gizani kwa kuhofia hatari.
lakini katika yote, tunashauriwa kutumia mwanga utakaotusaidia kuona mbele au Chochote huku tukiepuka kugusa au kushika vitu vibaya au vyenye madhara.
Vivyo hivyo, ukimtumaini Mungu na kuruhusu awe kiongozi katika maisha yako, atakuongoza na kukuepusha kwa yote yanaweza kuleta madhara kwako.
mfanye Mungu kuwa taa maishani mwako nawe utabarikiwa!!
UTATA UTATANI!
Je, YESU ni Mungu au NI binadamu? Kivp?
Tumekuwa tukijiuliza maswali mengi kuhusu YESU, au UUNGU WA YESU au KWANINI MUNGU ILIBIDI AUTWAE UBINADAMU? KWANINI na ilikuwaje?
Rejea yetu ni BIBLIA TAKATIFU agano JIPYA na KALE.
*Mwanadamu alipotenda dhambi, Ubinadamu wake haukuwa na uwezo wa kujiokoa Bali Uungu pekee ambao haupatikani na mauti. Hivyo Basi, Ubinadamu ukaunganishwa na Uungu.
Mungu + Binadamu=Mwana-damu(Yesu Kristo, Masihi).
UUNGU WA YESU:
Isaya 9:6....hutueleza kuzaliwa kwa mtoto mwanamume, Mungu mwenye NGUVU na BABA wa milele.
Yohana 1:1-3....Hutueleza bila Neno (Mungu) aliye Muumbaji, hakuna chochote kingefanyika.
Isaya 44:6...... hutueleza Bwana mfalme, Mkombozi, Bwana wa Majeshi ndiye wa KWANZA na wa MWISHO.
Ufunuo 1:14-18, ....... Hutueleza aliyekufa na Sasa Yu Hai, ndiye wa KWANZA na wa MWISHO.
UBINADAMU WA YESU:
Isaya 9:6..... Waebrania 2:16 ....... hutueleza Yesu kuutwaa mwili wa kibinadamu( mwili wa Ibrahimu).
Warumi 8:3-4 ....... hutueleza jinsi mwili wa kibinadamu usivyoweza kujiokoa, na ni YESU pekee(lmanuel, Mungu pamoja nasi) mwenye asili ya Uungu usiyokufa, ndiye mwenye uwezo wa kutuokoa na kututoa KATIKA dimbwi la dhambi.
Barikiwa Sana unapotafakari haya yaliyo machache na makuu maishani mwetu.
Eti NI kwa Nini wewe uko hivyo ulivyo? Kwa Nini yule Yuko vile? Kwa kweli huwa hatufananii kitabia ila tunaeza kuendana tu!
Cha kufahamu NI kwamba Kila mtu Ana Haiba na tabia yake.
Jifunze nasi itakuletea Aina kuu mbili za Haiba za mwanadamu ambazo NI EXTROVERT na INTROVERT kila moja imegawanyika Mara mbili ambazo NI SANGUINE, CHOLERIC, MELANCHOLI pamoja na FLAGMATIC. Kila Moja ana mtindo wake wa maisha.
Hii itatusaidia kuishi vema katika jamii zetu, lakini pia wale wanaohitaji wenzi watajua NI mwenzi wa aina gani anaweza kuwa chaguo kwakee.
Tubarikiwe sote.
22/03/2022
Laiti Mungu angekufunulia ujionee mambo makubwa anayokutendea hakika hakuna haja ya kuhofu chochote.
Kumtegemea Mungu na kufanya wajibu wako katika maisha huleta mafanikio makubwa sana, kiroho, kiafya na kimwili pia.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Website
Address
Ud
Temeke