AFYA LEO center

AFYA LEO center

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from AFYA LEO center, Health/Beauty, michenzani mall, Zanzibar.

TUNA TOA TIBA KWA KUTUMIA TEKNOLOJIA MPYA YA STEM SELL INAYO TIBU CHANZO CHA TATIZO NA KULIMALIZA KABISA TOFAUTI NA TIBA ZINGINE ZINAISHIA KUTIBU DALILI ZA TATIZO

04/10/2022

SARATANI YA TEZI DUME
Moja ya maradhi yanayoshuhudia kampeni kubwa kukabiliana nayo katika miaka ya hivi karibuni duniani ni pamoja na saratani ya tezi dume kutokana na ukubwa wa athari inazosababisha.
Ni maradhi yanayoshika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vinavyotokana na saratani kwa wanaume duniani.
✍️Pia ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wenye umri wa miaka 70 na kuendelea.
Hata hivyo, satarani ya tezi dume kwa sasa inawapata zaidi wanaume kuanzia miaka 25.
✅Maana ya saratani
Saratani maana yake ni ukuaji holela bila mpangilio wa seli baada ya kuparanganyika kwa mfumo wa seli unaodhibiti ukuaji na uhai wake. Na uvimbe wa kawaida wa tezi maana yake ni kuwa seli zimetutumka tu lakini hakuna mparanganyiko wa seli wala kukua kwa kusambaa kiholela k**a ilivyo kwa saratani.
✍️Hivyo, ndio maana kuna tatizo la kuvimba tezi dume na wengine kupata saratani ya tezi dume kwa wanaume wenye umri mkubwa.
✍️Tezi dume ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume. Inaundwa na sehemu mbili ambazo zimeunganishwa na kufunikwa kwa nje kwa utando wa tishu.
✍️Tezi hii ipo mbele kidogo ya puru (re**um) na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra).
✅Kazi ya tezi dume
Mojawapo ya kazi za tezi dume ni kutoa majimaji yanayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) wakati wa kilele cha tendo la kujamiana. Mchanganyiko huu wa mbegu pamoja na majimaji hayo hutengeneza shahawa (semen).
✍️Majimaji hayo husaidia kuzipa mbegu za kiume nguvu ya kusafiri kwenye uke mpaka kufikia kwenye mirija ya uzazi, tayari kwa utungisho na yai la k**e.
✍️Vilevile husaidia kupunguza hali ya kitindikali iliyopo katika uke, ambayo isiporekebishwa, huua mbegu nyingi za kiume na kufanya utungisho kuwa wa tabu..
✅Vyanzo Vinavyopelekea Tezi Dume Kutanuka:
Tatizo la kutanuka kwa tezi dume limekuwa kwa kasi sana hii ni kutokana na mitindo ya maisha wanaume wengi wanayoishi. Pia na elimu ndogo iliyoko kwenye jamii kuhusu afya zao.
✍️📌Vifuatavyo ni vyanzo vya kutanuka kwa tezi dume:
- Ukosefu wa lishe kamili na Virutubisho muhimu mwilini.
- Uwepo wa sumu nyingi mwilini.
- Kutokufanya mazoezi.
- Matumizi ya pombe kali, na uvutaji wa sigara.
- Uzito mkubwa (uliopindukia, uliokithiri), na Kitambi.
- Kutokukaa sawa kwa vichocheo vya mwili (Hormone Imbalance).
- Msongo wa mawazo (Stress).
- Magonjwa ya zinaa.
- Umri mkubwa.
- Upasuaji wa korodani, kuzaliwa na korodani moja.
- Historia ya Familia (Kurithi).
- Mazingira (Ethnicity).
✅Dalili za saratani ya tezi dume ni zipi?
a) Dalili za awali
- Kukojoa mkojo uliochanganyikana na damu
- Kukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu
- Maumivu kwenye mfumo wa mkojo
- Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa
- Kuhisi kibofu kimeja mkojo muda wote na ukienda kukojoa mkojo hautoki, lakini ukirudi kukaa unahisi kukojoa tena.
- Homa
- Kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku
b) Dalili za mtu aliyeathirika
- Maumivu ya mifupa hasa chini ya mgongo, kiuno na mbavu
- Miguu kuwa dhaifu
-Kushindwa kumudu tendo la ndoa, au Kuhisi maumivu makali wakati unamaliza tendo la ndoa
- Kushindwa kuzuia mkojo, pindi unapohisi kukojoa
- Kushindwa kuzuia haja kubwa (kinyesi cha maji maji)
- Tumbo kuja gesi mara kwa mara
✅Vipimo gani vitathibitisha kuwa nina saratani ya tezi dume?
Utambuzi wa saratani ya tezi dume hujumuisha kufahamu historia ya mgonjwa pamoja na familia yake, kufahamu dalili alizo nazo mgonjwa pamoja na kufanya vipimo kadhaa. Vipimo vinavyoweza kufanywa ni pamoja na
📌Digital re**al exam: Daktari ataingiza kidole cha shahada katika puru (re**um) ili kuhisi tezi dume kupitia ukuta wa puru. Aidha atahisi pia sehemu zote zinazozunguka tezi dume kutambua iwapo tezi ni ngumu au k**a ina uvimbe wowote.
📌Kipimo cha damu kuchunguza Prostate Specific Antigen (PSA): PSA ni aina ya protein inayozalishwa na seli za tezi dume. Uzalishaji wake huongezeka wakati wa BPH, tezi dume inapopata uambukizi (prostitis) , na saratani ya tezi dume. DRE pamoja na PSA huonesha uwepo wa tatizo kwenye tezi dume lakini vipimo hivi havina uwezo wa kutofautisha iwapo tatizo hilo linamaanisha saratani au BPH. Hivyo basi, ili kuweza kutofautisha kati ya magonjwa hayo mawili, kipimo kiitwacho Prostate biopsy hufanywa.
📌Prostate biopsy: Kipimo hiki hufanywa kwa kuchukua kipande cha nyama (tishu) kutoka tezi dume kwa ajili ya uchunguzi maabara.
Kipimo kingine huitwa transre**al ultrasound ambacho husaidia kuonesha ukubwa na sura ya tezi dume lilivyo.
✍️Ili kutambua k**a saratani imesambaa sehemu nyingine za mwili vipimo vya CT scan, MRI pamoja na PET navyo vyaweza kufanyika pia.
✅Madhara ya Tezi Dume:
Yafuatayo ni madhara ya tezi iliyotanuka:
- Kibofu cha mkojo kuuma: hivyo hupelekea mkojo kurudi juu, na kuharibu figo na Ini … … n.k.
- Kufunga kwa njia ya mkojo kabisa
- Figo kushindwa kufanya kazi (Kidney Failure)
- Kushindwa kumudu tendo la ndoa (Ndoa zinavunjika)
- Ugumba (Infertility, Frigidity for men)
- Kutokea kwa majipu sehemu ya Tezi Dume
- Kifo
✅Saratani ya tezi dume inatibika?
Tiba kamili ya tezi dume ni kwa Kutibu chanzo cha tatzo kwa maana ya kukarabati seli ya tezi dume na kuondoa madhara yaliyo sababisha tezi kuasilika hivyo STEM CELL ndo jibu kamili unaenda tibu chanzo cha tatzo Pamoja na dalili zake tofauti na tiba zingine zinaishia Kutibu dalili pekee

21/09/2022

Seli shina ni nini?

Mwili wa binadamu una mamia ya seli (chembechembe hai) za aina tofauti zenye umuhimu kiafya. Seli hizi zina jukumu la kuendesha mifumo mbalimbali ya miili yetu, kwa mfano, kuendesha mapigo ya moyo, kuwezesha fikra akilini, usafishaji wa damu kwenye figo, kutengeneza ngozi mpya, na kadhalika. Kazi ya kipekee ya seli shina ni kuwa chimbuko la kuzalisha aina nyingine ya seli. Seli shina pia hufanya shughuli ya ugavi wa seli mpya mwilini. Seli hizi zinapojigawanya huzidisha idadi ya seli shina nyingine au seli nyingine za kawaida. Kwa mfano, seli shina za ngozi zinauwezo wa kuzalisha seli shina zingine zaidi za ngozi au kuzalisha seli tofauti zenye kazi maalumu k**a kutengeneza melanin.

Kwanini seli shina ni muhimu kwa afya yako?

Tunapoumia ama kupata maradhi, seli zetu pia huumia au kufa. Hali hii ikitokea, seli shina huanza kufanya kazi. Seli shina zitaponya majeraha mwilini na pia kujaza nafasi ya seli zinazokufa mara kwa mara. Kwa njia hii, seli shina zinatuweka katika hali ya afya nzuri na kudhibiti mwili kudhoofika mapema. Seli shina ni k**a jeshi la matabibu wanaoonekana kwa hadubini pekee.

Kuna aina ngapi tofauti ya Seli Shina?

Seli shina huwa katika aina au mifumo mbalimbali. Wanasayansi wanaamini kuwa kila kiungo mwilini kina seli shina zake maalumu. Kwa mfano, damu hutengenezwa na seli shina za damu (hematopoietic stem cells). Hata hivyo, seli shina huwepo kuanzia hatua za awali kabisa za uumbaji wa mwanadamu, na pale wanasayansi wanapootesha aina hizi za seli ndipo hufaamika k**a “seli shina za kiinitete”. Sababu inayowafanya wanasayansi kuhusiana karibu na seli shina za kiinitete ni umuhimu wake katika kujenga kila kiungo cha mwilini wetu wakati wa uumbaji. Hii humaanisha ya kuwa seli shina za kiinitete, tofauti na seli shina komavu, zina uwezo wa kubadilika na kuwa seli yoyote kati ya mamia ya seli za binadamu. Kwa mfano, kwakuwa seli shina za damu zinauwezo wa kutengeneza seli za damu tu, seli shina za kiinitete zinauwezo wa kutengeneza seli za damu, mifupa, ubongo, na kadhalika. Pamoja na hayo, seli shina za kiinitete zimepangwa kiasili kujenga seli shina nyingi na hata viungo, wakati seli shina komavu hazina uwezo huu. Hii inamaanisha ya kwamba seli shina za kiinitete zina uwezo asilia mkubwa zaidi kurekebisha viungo majeruhi. Seli shina za kiinitete huzalishwa kupitia mabaki ya viinitete vichanga kwenye vituo vya matibabu ya uzazi, matumizi ambayo ni muhimu la sivyo viinitete hivi hutupwa pasipo ya matumizi yake kwa ajili ya tafiti za tiba.

SSS au Seli Shina Shawishi ni nini?

Wanasayansi na matabibu duniani kote wamepata mategemeo mazuri kuhusu ujio wa Seli Shina Shawishi (SSS). Sababu kuu ni kuwa SSS zina sifa karibu zote za seli shina za kiinitete, ila hazizalishwi kutoka kwa viinitete. Hivyo basi, hakuna pingamizi za kiimadili kuhusu matumizi ya SSS. Zaidi ya haya, SSS hutengenezwa na seli ambazo siyo Seli Shina kutoka kwa mgonjwa mwenyewe, hivyo kuzipa SSS uwezo wa kurudishiwa kwa mgonjwa bila hatari ya kushambuliwa na mfumo wa kinga wa mwili. Jambo hili ni la umuhimu katika tiba yoyote ya upandikizwaji wa Seli Shina.

Kuna mategemeo yapi kuhusiana na Seli Shina na jinsi ambavyo zitaleta mapinduzi katika tiba?

Jukumu la seli shina ni kubadilisha seli zenye majeraha, ugonjwa au seli zilizokufa. Wanasayansi wamepata wazo la kutumia seli shina katika tiba kwa ajili ya wagonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Wazo lao kuu ni kuwapa wagonjwa seli shina au seli komavu zilizozalishwa na seli shina. Kwa namna hii wanatumia nguvu asilia ya Seli Shina kutibu na kumrudisha mgonjwa katika hali ya afya tena. Kwa mfano, k**a mgonjwa amepata shinikizo la moyo, tiba itakayotumika ni kupandikiza seli shina kwa mgonjwa ili kutibu majeraha kwenye moyo. Kwa kawaida idadi ya seli shina tulizonazo mwilini zina uwezo mdogo kurekebisha majeraha. Tukirudi kwenye mfano wa shambulizi wa moyo, seli shina za moyo hazina uwezo wa kutosha wa kuponya majeraha yanayotokana na shinikizo la damu, lakini pale mamilioni ya seli shina za moyo zitakapopandikiwa uwezo wa tiba huongezeka maradufu. Hivyo basi kwa kuwapandikiza wagonjwa kutumia seli shina tunaongeza uwezo wa mwili kuponya zaidi ya uwezo mdogo wa kiasilia. Changamoto chache bado zipo kabla matibabu ya seli shina kuwa tiba ya kidesturi, kwa mfano changamoto za usalama kwasababu ya uwezo wa baadhi ya seli shina kutenegeneza uvimbe wa saratani, na pia changamoto ya mashambulio ya mfumo wa kinga wa mwili. Hata hivyo seli shina huenda zikaleta mageuzi makubwa kwenye matibabu, na pengine baada ya muongo au miongo miwili wengi wetu, pengine hata sisi wenyewe, tutakuwa tunafahamu mtu aliyetibiwa kwa kupandikizwa na seli shina. Seli shina zimeshikilia ahadi ya kuwa na uwezo wa kutibu magonjwa mengi yanayomsibu binadamu k**a saratani, magonjwa ya moyo, ugonjwa wa Parkinson, Uzulufu mwingi, kiharusi, ugonjwa wa Huntington, majeraha ya uti wa mgongo na magonjwa mengine mengi.

Ni tiba gani ya Seli Shina inayopatikana kwa sasa, na kwanini matabibu wengi wanashauri uzingatie tahadhari aina hii ya tiba iwe chaguo la mwisho?

Hivi sasa, kuna tiba chache zinazotumia seli shina zilizo na ufanisi pamoja na uthibitisho wa usalama. Mfano bora zaidi ni upandikizaji wa uhogo wa mfupa. Hata hivyo, tiba mbalimbali za seli shina hutangazwa na kunadiwa dunia kote. Mara nyingi tiba hizi hutangazwa zaidi kwenye vyombo vya habari, hasa pale ambapo watu maarufu k**a wanamichezo wanapopata tiba za aina hizi. Kiujumla, wanasayansi na matabibu kwenye fani ya seli shina hutoa tahadhari kuhusu tiba hizi kwasababu bado haijafahamika iwapo aina hii ya tiba ni salama na ni fanisi. Wagonjwa wengi wamefariki kutokana na tiba ya aina hii. Pamoja na kuwa ni jambo la busara kuzingatia njia zote unapopatwa na maradhi au magonjwa yasiyotibika, tunashauri uzingatie tiba hii k**a chaguo la mwisho na iwe baada ya kushauriwa na mganga wako.

19/09/2022

MLO WA MAMA ANAYE NYONYESHA
Mama anayenyonyesha anahitaji kuangalia sana vyakula anavyotumia, ikizingatiwa huchangia pakubwa hali yake ya afya. Unachokula wakati wa kunyonyesha ni muhimu sana katika kurejesha afya yako katika hali nzuri baada ya kujifungua. Hali hiyo pia itachangia kiwango cha maziwa kitakachozalishwa mwilini.
✍️Hivi hapa ni vyakula bora zaidi zinazoimarisha afya ya akina mama wanaonyonyesha:
1. Maji
Kunywa maji safi kunasaidia kuongeza maziwa yanayotoka mwilini. Bila maji, utapungukiwa na maji mwilini na kukosa nguvu. Kunywa maji unapohisi kiu, vinywaji ambavyo havina kafeini, vinywaji ambavyo havijaongezwa sukari, supu, sharubati na mboga.
2. Samaki
aina ya salmon Salmon ina vitamin B12 na aside za omega 3 zenye mafuta ambazo utafiti umeonyesha husaidia kumaliza matatizo ya hisia baada ya kujifungua. Kulingana na mtaalamu wa vyakula na mapishi yenye afya Rose Kagengo, salmon ina vitamin D ambayo wanawake wengi hukosa.
3. Nafaka
Vyakula vya nafaka k**a mkate, mchele, pasta na chakula kilichotengenezwa kwa shayiri vina vitamini B, madini na kumbi. Kumbi, kwa kimombo ‘faiba’ husaidia mama kujihisi ameshiba na kumsaidia kupunguza uzito uliotokana na uja uzito. Pia kumbi husaidia katika kusagwa kwa vyakula tumboni na kuimarisha viwango vinavyostahili vya sukari mwilini. Nafaka k**a quinoa, faro, spelt, shayiri na teff humpatia mama protini zaidi. Mama anayenyonyesha anastahili kula vyakula vyenya afya ili kumsaidia kuzalisha maziwa mengi kwa mtoto na kurejesha mwili wake katika hali ya kawaida.
4. Nyama
Akina mama wanaonyonyesha wanahitaji zaidi madini ya zinki na nyama huwapa madini hayo. Nyama ina protini nyingi na bora na ina vitamin B na iron inayosaidia kuimarisha nguvu. Ikiwezekana, tumia nyama kutoka kwa mnyama aliyelishwa kwa nyasi asili kwa kuwa nyama hiyo ina asidi za omega 3 zenye mafuta.
5. Mayai
Mayai yana kolini, luteini, vitamin B12 na D, riboflavin (Vitamini B2) na Folate (vitamin B 9) yanayoupa mwili virutubisho tosha.
Utafiti wa hivi punde umeonyesha kuwa mayai hayawezi kuongeza kiwango cha kolestro mwilini.
6. Mboga ya rangi ya kijani kibichi
Mboga zina vitamin A, C, E na K na viwango vya chini vya kalori. Vina kumbi au ‘fiber’ na kemikali zinazozuia chakula kuoza zinaposagwa. Kuna mboga angalau mara moja kwa siku na uzichanganye na mayai.
7. Kunde na maharagwe Vyakula hivi vina protini na kumbi, madini na kemikali za ‘phyto’. Unaweza kula maharagwe ya aina yoyote kwa kuzichanganya na kunde.
8. Njugu na mbegu tofauti Njugu zina protini, madini, vitamin, chemikali za kuzuia vyakula kuoza zinaposagwa na mafuta yenye afya. Vyakula hivi huzuiwa ugonjwa wa moyo, kuzeeka, hunyoosha ngozi na kukushibisha nyakati ambazo sio za kula. Tumia lozi, mchanganyo wa njugu na mbegu tofauti, tofaa na mafuta ya lozi.

19/09/2022

Niliwaambia wanangu wasihangaike tena na mimi juu ya tatizo langu kwani walitumia gharama nyingi sana kunisaidia ili niondokane na tatizo hili na nilifanyiwa upasuaji mara ya kwanza nkajua nimepona ila baada ya mda wa miaka miwili tatizo lilianza tena
Nilitumia kila aina ya njia kujaribu ili nipone lakini niliambulia kupoteza pesa zangu tu. Ndipo nilipo wazuia wanangu kuhangaika namie tena juu ya tatzo langu la kuvimba kwa tezi dume pamoja na presha
Binti yangu alikuja kuniambia sku moja kuwa kakutana na njia nyepesi yakuweza kutatua tatizo langu kwamda mfupi nitapona, nilimkatalia kabisa kwani nilijua atatoa pesa tu huko na nisipone nikijiangalia na umri wangu miaka 53 skuona haja tena
Aliendelea nisisitiza sana nkaona acha nijaribu kutumia ili nimlizishe tu
Skuamini kabisa wiki ya tatu tangu nitumie njia hii maumivu wakati wa haja ndogo yaliisha naskupata haja ndogo mara kwa mara tena wala mkojo kutoka kidogo kidogo,pia nilikua nakojoa mkojo umechanganyikana na damu, hata uvimbe kupungua kabisa na baada ya wiki kadhaa wakanipeleka hospitali kuangalia nikaambiwa sina tena tatizo lile, skuweza kuamini kwakweli namshukuru Mungu kwa msaada wa suhulisho hili
Ngelipenda nawazee wezangu waijue njia hii kwa kuwasiliana na huyu MAMA alie weza kunisaidia kupitia njia hii nyepesi mpigieni awasaidie 0788203871

19/09/2022

afya ndo mtaji wako hakikisha afya yako ni imara

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Zanzibar?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Address


Michenzani Mall
Zanzibar