Kassm Seif
Darsa
صوت قراءة الإمام فضيلة الشيخ، الإمام مسجد الأزهر الشريف مصر القاهرة.. ربنا يفتح له أبواب رحمته..🤲
قال الله تعالى:
"وقالوا لجلودهم لم شهدتم علينا قالوا أنطقنا الله الذي أنطق كل شيء وهو خلقكم أول مرة وإليه ترجعون"..
( سورة فصلت: آية 21 )
"Na watasema ( Makafiri ) Siku ya Qiama kuviambia viungo vyao, kwann mumetukalia ushahidi? ( mumetuchongea )! Viungo vitasema: aliyetusemesha ni Allah ( s.w ) ambaye ni mwenye uwezo wa kukisemesha kila kitu, na yeye ndiye aliyewaumba nyinyi mara ya kwanza na kwake mutarejeshwa.."
Yapatikanayo: Allah ( s.w ) ni muweza wa kufanya kila kitu ktk yale yanayoendana na ufalme wake, akili ya Binaadamu haina uwezo wa kufikia kikomo kwa kutafakari juu ya Uwezo wa Allah ( s.w), kila unavyofikiria juu ya uwezo wa Allah upo namna fulani basi uwezo wake upo zaidi ya ufikiriavyo..
Kila unalolifanya kwa siri au kwa dhahiri mwisho wa siku litabainika mbele ya Allah ( s.w ), hvy Binaadamu hatakiwi kuviamini hata viungo vyake vya mwili akidhani anafanya siri, viungo navyo vinaona na vina taaluma tosha ya kile ukifanyacho..
Dunia ni mapito tu, ila kwa Allah ( s.w ) sote ni lazima tutarejeshwa..
Aliposema neno "جلودهم" ni fumbo linalomaanisha utupu, endapo Mtu atautumia utupu wake kwa Njia za haram siku ya Qiama utupu huo utamkalia ushahidi.. والله أعلم
Uharamu wa Shirki..
قال الله تعالى:
"واضرب لهم مثل الحياة الدنيا كمآء أنزلناه من السماء فاختلط به نبات الأرض فأصبح هشيما تذروه الرياح وكان الله على كل شيء مقتدرا.." ( سورة الكهف: آية 45 )
"Wapigie mfano wa maisha ya Dunia ni k**a maji tunayoyateremsha kutoka Mbinguni, kisha yakachanganyika na mimea ya Ardhini, na ikawa mimea hyo ni chakavu kwa kupeperushwa na upepo, Na Allah ni mwenye uwezo wa juu ya kila kitu.."
Dokezo: Ameifananisha Dunia ( maisha ) na Maji, kwa sababu Maji hayatulii sehemu moja, halkadhalika Dunia haitabakia ipo siku muda wake wa kuwepo utakwisha, na hakuna atakayebakia.. au hakuna mwenye uwezo wa kuyakwepa maji kwa namna yeyote ile atayahitaji, halkadhalika hakuna atakayesalimika na fitna na Mitihani ya Dunia..
Kipato, Cheo, Umaarufu n.k. vina muda maalum, ndio maana ya kusema maji yanachanganyika na mimea ya Ardhini, na kuleta rangi nzr ktk mimea hyo pamoja na harufu nzr, kisha ghafla upepo unakuja kupeperusha majani yote baada ya kuchakaa kwake, hvyhvy Binaadam licha ya Umaarufu na cheo chake ipo siku vitafikia tamati na hatakua mwenye thamani tena Duniani..
Allah kua ni muweza wa kufanya lolote ni ktk Ukubwa wake, Utawala na Ufalme wake, yote yanayotendeka ni ktk Qadar zake na ni wepec kwake kila jambo..
عن ابن عباس رضي الله عنه، أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: "من وجدتموه يعمل عمل قوم لوط فاقتلوا الفاعل والمفعول به.." وفي رواية: "لعن الله من يعمل عمل قوم لوط" ثلاث مرات.. رواه الترمذي وأبو داود وأحمد
"Mutakayemkuta anafanya vitendo vya Watu wa Nabii Lut ( a.s )
( kuendeana kinyume n maumbile ), muuweni Mfanyaji na Anayefanyiwa kitendo hiko.."
Mapokezi mengine:"Allah amemlaani mwenye kufanya vitendo vya Watu wa Nabii Lut ( a.s ).."
Alirejea neno hilo Mara tatu..
Yaliyomo: Vizazi vingi vinaharibiwa kwa kitendo hiki cha kuendewa kinyume na Maumbile ( Liwat ).. na kusababisha Ukosefu wa Maadili kwa Vijana ambao ndio tegemeo kubwa la Maisha ya mbele..
Mfanyaji na mfanywaji wa kitendo hiki hukmu yake ni kuuliwa kwa Upanga ili kufarakanishwa Kichwa na Mwili wake.. hii ni makubaliano ya Wanazuoni wengi..
Maana ya kulaaniwa na Allah ni kutolewa na kuwekwa mbali na rehma zake, kila Mja anahitaji rehma za Allah, mwenye kufanya au kufanyiwa kitendo hiki amewekwa mbali na rehma za Allah..
Note: Kwa Watoto wadogo waliyo chini ya Umri wa Balegh endapo watafanya au kufanyiwa kitendo hiki, hakuna hukmu ya kuuliwa dhidi yao, ni vyema wakaonywa au kuchukuliwa hatua M-badala wasije wakarudia, kwa sababu hawaandikiwi madhambi kwa umri huo..
Tunamuomba Allah avilinde vizazi vyetu kwa hili na jengine yenye kusababisha kuharibika kwa vizazi vyetu hadi Taifa kwa Ujumla..Ameen🤲
قال الله تعالى:
"الذي خلق الموت والحياة ليبلوكم أيكم أحسن عملا وهو العزيز الغفور" ( سورة الملك: آية 2 )
"Allah (s.w ) ndiye ambaye ameyaumba Mauti ( kifo ) na Uhai, kwa Lengo la kuwajaribu ni yupi miongoni mwenu mwenye matendo mazuri zaidi, na yeye ni mwenye nguvu na mwenye kusamehe.."
Yapatikanayo: Ameyatangauliza Mauti dhidi ya Uhai kwa sababu kifo kipo karibu zaidi hadi kufika kwa Allah kuliko Uhai... au ameyatanguliza Mauti kabla ya Uhai kwasababu kila kitu kimebeba hukmu ya kifo kabla ya kuwepo kwa kitu hiko, Wanaadamu hawakuwepo, wala Majini, Wanyama na viumbe vyote asili yetu tumebeba hukmu ya kifo kwakuwa hatukuwepo..
Kipimo cha kumjua ni yupi Mkweli na yupi Muongo& muovu au mwema, ni kipindi cha matatizo na shida ( mitihani ), hapa hujulikana Mtu uhalisia wake namna alivyo..
Allah ( s.w ) ni mwenye nguvu na mkali dhidi ya Waliyopinga maagizo yake, pia ni msamehevu na mwenye huruma kwa Waliyofuata maamrisho yake na kujiweka mbali na makatazo yake..
قال الله تعالى
"مثل الذين اتخذوا من دون الله أوليآء كمثل العنكبوت اتخذت بيتا وإن أوهن البيوت لبيت العنكبوت لو كانوا يعلمون.. ( سورة العنكبوت: آية 41 )
"Mfano wa wale ambao wenye kujifanyia vya kuabudia ( Masanamu & wasimamizi wa mambo yao ) kinyume na Allah, ni k**a mfano wa Buibui aliyejitengenezea Nyumba, na kwahakika nyumba duni ( dhalili ) zaidi ni Nyumba ya Buibui lau wanagaliyajua hayo..
Mafunzo: Mwenye kumtegemea Kiumbe mwenzake na Kumuacha Allah ( s.w ), Kiumbe huyo hana Dhamana maana yeye pia ameumbwa, hvy muda wowote anaweza kuondoka ktk Maisha ya Duniani..
Nyumba duni au dhalili ni ya Buibui, na mwenye kuitengeneza Nyumba hyo ni Buibui mwenye jinsia ya k**e.. ( Buibui Mke )..
Buibui mwenye jinsia ya k**e ( Buibui Mke ) akishajua kwamba ameitengeneza yeye nyumba, anachokifanya ni kumfukuza ( kumtimua ) Buibui dume ndani ya Nyumba yake, Mfano wake ukimtegemea Kiumbe kwa kila jambo mwishowe atakuacha patupu ili apate kuendelea na harakati zake pasi na kusumbuliwa na yeyote..
قال الله تعالى
"نحن أعلم بما يقولون ومآ أنت عليهم بجبار فذكر بالقرءان من يخاف وعيد" ( سورة:ق آية:45 )
"Sisi tunayajua zaidi wasemayo ( Washirikina ), na hukuwa wewe ni mwenye kuwalazimisha kwenye Imani ili wakuamini, basi kumbusha kwa kutumia hii Qur-ani italeta manufaa kwa mwenye kuogopa Adhabu za Allah.."
تفسير البيضاوي
Faida: Ukumbusho ni wenye kuleta manufaa kwa wenye Imani ya Kweli.. ni dhahiri kwa Mlinganiaji asichoke kutokana na kashfa au dharau anazozipata dhidi ya wanaompiga vita..
Dini ya Uislam ni ya Allah ( s.w ), hvy kuishi kwa Kumtegemea Allah ndio sehemu ya mafanikio ya Mja duniani na Akhera..
Hakika ya Allah ( s.w ) ni Mkali wa kuadhibu, hakuna awezae kuhimili vishindo na ukubwa wa Adhabu za Allah miongoni mwa Viumbe vyake..
Maneno mazuri na sahihi zaidi ni Qur-an, kwa mwenye kuisoma na kuifanyia kazi ni Uongofu kwake ktk Maisha yake ya Dunia na Akhera..
عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: "الرجل على دين خليله فلينظر أحدكم من يخالل"
Amesema صلى الله عليه وسلم "Mtu hufuata mwenendo wa rafiki yake, basi na aangalie mmoja wenu ni nani wa kumfanya rafiki.."
Mafunzo: Kujua tabia ya Mtu usimuulizie yeye binafsi, muulizie rafiki yake wa karibu, kwa sababu rafiki humfuata rafiki yake..
Ni jukumu la Wazazi kuhakikisha wanamchagulia Mtoto/Watoto wao marafiki wa kua nao ktk harakati zao kuepusha marafiki waovu..
Majuto yatapatikana siku ya Qiama endapo Mtu atajichagulia rafiki muovu..
. ياليتني لم أتخذ فلانا خليلا.."
Baada ya kuiona Jahannam iko mbele yake Mtu atasema.."Ole wangu! Natamani leo, fulani nisingalimfanya kua ni rafiki yangu kule duniani.."
عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول: "والله إني لأستغفر الله وأتوب إليه في اليوم أكثر من سبعين مرة" رواه البخاري
"Nawaapia kwa Allah kwahakika Mimi ninaomba Msamaha kwa Allah na kutubia kwake kwa Siku moja mara zaidi ya Sabiini 70.."
Mafunzo: Kutaka Msamaha kwa Allah ni Wajibu wa kila Mja kutokana na dhambi alizozifanya iwe kwa makusudi au kwa kutokujua..
Nguo ikiwa chafu inafuliwa ili isafike, hvy Mja anatakiwa aombe Msamaha kwa Mola wake hatak**a ni mwenye kuyarudia makosa yale ya Kibinaadamu na sio kukata tamaa..
Kiumbe Bora kuliko wote ni Mtume wa Allahصلى الله عليه وسلم na hvy hakua nyuma kuomba Msamaha kwa Mola wake, kinachotakiwa ni mimi na wewe tuzidishe jambo hilo..
عن أبي سعيد الخدري رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: "الحسن والحسين سيدا شباب الجنة وأبوهما خير منهما"..
"Hassan na Hussein ni mabwana wawili wa Vijana wote Peponi, na Baba yao
( Imaam Ali r.a ) ni bora kuliko wao..
( Hassan na Hussein )
Note: Hassan na Hussein ni Wajukuu wa Mtume Muhammad ( s.a.w ).. na Baba yao Mzazi ni Imaam Ali ( r.a ) ambaye ni bora zaidi yao.. kwa nafasi aliyokua nayo mbele ya Allah na Mtume wake, pamoja na jitihada kubwa aliyoifanya katika kuipeleka dini ya Allah mbele..
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Zanzibar