Afya.2011

Afya.2011

Share

best

07/10/2021

*YAJUE MAGONJWA YA MOYO NA JINSI YA KUJIKINGA*

Magonjwa ya Moyo ni magonjwa yanayoambatana na kuathiri moyo. Mara nyingi magonjwa ya moyo yanaambatana na mishipa ya damu kuwa na tatizo ambapo moyo hushindwa kufanya kazi, moyo hutegemea damu ambayo hubeba oxygen, madini, vitamins, kinga ya mwili, joto, homoni na vingine vingi.

Kwa mwaka 2015 pekee zaidi ya watu milioni 17.7 walifariki kutokana na magonjwa ya moyo na mfumo wa damu. Hii ni sawa na theluthi ya vifo vyote duniani. Zaidi ya theluthi ya vifo vyote vinavyotokana na ugonjwa wa moyo na mishipa ya damu hutokea ndani ya nchi zenye uchumi wa chini na uchumi wa kati

*AINA ZA MAGONJWA YA MOYO*

Zipo aina mbalimbali za magonjwa ya moyo hutofautiana japo yote huathiri moyo, nayo ni;

*Ugonjwa wa moyo unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu* _(Coronary artery disease)_:
Hili ni tatizo linalowakuta watu wengi, mishipa ya damu hupasuka na kuharibika hii hutokana na mishipa ya damu kuwa na uchafu na mafuta mengi na kufanya damu isipite vizuri

*Mapigo ya moyo kwenda tofauti* _(Heart Arrhythmias)_:
Hii hutokea pale mapigo ya moyo kwenda taratibu isivyo kawaida au kwenda haraka isivyo kawaisda, pia mapigo ya moyo kwenda ovyo. Hii ni hatari sana na huua sana

*Moyo kushindwa kufanya kazi* _(Heart Failure)_
Hii ni hali moyo hushindwa kufanya kazi yake k**a kupampu na kusambaza damu, kusambaza oxygen. Hii inaweza kutokea kwa mtu mwenye magonjwa k**a ugonjwa wa moyo wa misipa kuathirika, Shinikizo la damu, na magonjwa mengine.

*Magonjwa ya moyo ya kuzaliwa* _(Congenital heart disease)_: Haya ni magonjwa ambayo wengi huzaliwa nayo, yanaweza kuwa ni baadhi ya kasoro katika mwili k**a baadhi ya chemba za moyo kuziba au kupasuka, oxygen kupita kwa shida na vinginevyo.

*Ugonjwa wa valvu na misuli ya moyo* _(Heart Valve Disease & Cardiomyopathy (Heart Muscle Disease))_
Katika moyo kuna chema nne nazo zinapitisha damu na oxygen kutoka kwenye mapafu, valvu hufunguka na kufunga. Valvu na misuli ikiwa imepasuka na kuharibika husababisha tatizo la moyo.

*Moyo kutanuka.*
Hii hutokea pale damu ikiingia ndani ya moyo harafu mishipa ya kutoa damu ikiwa na tatizo ikashindwa kutoa damu nje ya moyo moyo utaanza kutanuka siku hadi siku. Kutanuka kwa moyo kunatokea usipotibu baadhi ya matatizo k**a shinikizo la damu, moyo kwenda mbio, valvu na misuli ya moyo n.k.

*Shinikizo la damu (B.P)* ni shinikizo la damu yako kwenye kuta za mishipa yako kwani moyo wako unasukuma karibu na mwili wako. Unaweza kuwa na shinikizo la damu (shinikizo la damu) kwa miaka bila dalili yoyote.

*Mshtuko/ Shambulio la moyo* _(Heart Attack)._
Ni kifo cha sehemu ya misuli ya moyo inayosababishwa na kuzuiwa wa usambazaji wa damu. Amana zilizo na mafuta huunda kwa wakati, na kutengeneza alama katika mishipa ya moyo wakoIkiwa baadhi ya misuli ya moyo inakufa, mtu hupata maumivu ya kifua na kukosekana kwa umeme kwa tishu za misuli ya moyo.

*Chembe ya Moyo.* Hii ni maumivu ya upande wa moyo maeneo ya kifua hutokea wakati unafanya kazi au hata k**a umekaa k**a ni yenye kukubuhu. Maumivu haya huambatana na kutokwa jasho na kukosa hewa. Hutokana na moyo kukosa damu ya kutosha.

*CHANZO CHA MAGONJWA YA MOYO*
Magonjwa ya moyo hutokea pale ambapo moyo huathiriwa na kuharibiwa kwa vitenda kazi vyake. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata magonjwa ya moyo nayo ni pamoja na;

•Kuwa na Lehemu (Cholesterol) na •Shinikizo la damu (B.P)
•Kuvuta sigala
•Uzito kupita kiasi na unene uliozidi
•Kisukari
•Kukaa sehemu kwa mda mrefu bila kuufanyisha kazi mwili
•Umri mkubwa
•Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi
•Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili
•Historia magonjwa yanayoambatana na moyo katika familia

*DALILI ZA UGONJWA WA MOYO*
Mara nyingi dalili hujionesha wakati mtu kakaa na ugonjwa kwa mda mrefu kidogo, ila kuna zingine zinatangulia na mara nyingi wengi huwa wanazipuuzia. Uonapo baadhi ya dalili fanya mawasiliano na daktari wako wa familia au nipigie simu.

👉🏿Moyo kwenda mbio (Moyo kudunda kwa nguvu isivyo kawaida )
👉🏿Uchovu uliopitiliza, mwili kuwa dhaifu na kuchoka haraka hata kwenye shughuri ndogo
👉🏿Maumivu ya kifua hasa yanayotembea mpaka kwenye mabega, shingo au taya
👉🏿Kushindwa kulala vizuri hasa kushtuka usingizini kuhisi k**a unakabwa na kukosa pumzi
👉🏿Tumbo kujaa, kichefuchefu na kutapika
👉🏿Kukosa pumzi au kushindwa kupumua vizuri hasa unapolala chali
👉🏿Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji

*JINSI YA KUEPUKANA NA MAGONJWA YA MOYO*
1• Fanya mazoezi – Angalau dakika 30 kwa siku
2• Usile vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi
3• Usitumie chumvi mbichi au chumvi nyingi
4• Punguza (balansi) kiwango cha Lehemu (choresterol)
5• Balansi usito wako
6• Usivute sigara
7• Punguza au acha kunywa pombe
8• Punguza mawazo
9• Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali
10• Lala vizuri kwa muda mzuri – masaa 6 hadi 8

*TIBA YA MAGONJWA YA MOYO*
Magonjwa ya moyo yanatibika kwa hali tofauti, pia kufuatana na mda wa tatizo, mara nyingi wagonjwa wamekuwa wakikata tamaa na kuwa wabishi, hii hufanya wengi kufa kutokana na kuto kuwa makini na kile tunacho waeleza
Wapo watu huitaji kufanyiwa biopsy na wengine hufanyiwa operation ya kawaida.

*MATIBABU YA LISHE*
Kiungo hiki cha moyo huitaji lishe yenye viosha sumu, amino acids, madini mbali mbali k**a chuma, potassium, calcium, fatty acid k**a omega 3, gas, chembechembe za Co enzyme Q10 ambavyo hupatikana kwa kula vyakula fulani hasa matunda, mbogamboga na viumbe wengine.
Pia unaweza kupata mahitaji yote hayo kupitia virutubisho maalumu vya afya ya moyo na mfumo wa damu *(cardiovascular health nutritional pack)*

Wasiliana nami 0755325722

06/08/2021

TIBA SAHIHI YA UGONJWA WA U.T.I, FANGASI SUGU NA MIWASHO UKENI.
0755325722

Fangasi Inasababishwa na jamii ya fungi anaitwa CANDIDA. Seli za fangasi na bacteria wazuri huishi ukeni bila tatizo lolote. Tatizo linakuja endapo ukuaji wa fangasi hawa ukeni watakuwa wengi kushinda wazuri. Basi hapo ndio inapotokea ugonjwa wa fangas na miwasho mingi.

DALILI ZA FANGASI

1. Kukojoa mara kwa mara.

2. Mkojo kuwa na harufu kali.

3. Maumivu ya misuli na tumbo hasa chini ya kitovu.

4. Maumivu ya kiuno.

5. Kuwashwa sehemu za siri.

6. Kuhisi maumivu wakati wa kujamiiana.

7. Kupata vidonda vya ukeni.

8. Kuvimba na kuwa mwekundu kwa mdomo wa inje wa uke.

9. Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri baada ya tendo la ndoa.

10. Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au kijivu unaoweza kuwa mwepesi au mzito au majimaji.

VISABABISHI VYA FANGASI.

1. Mabadiliko ya homoni katika kipindi cha upevushwaji wa mayai kwa mwanamke kipindi cha ujauzito, utumiwaji wa uzazi, wa mpango na kukoma kwa hedhi.

2. Upungufu wa kinga mwilini: Mtu mwenye upungufu wa kinga mwilini k**a vile mwenye kuugua kansa, ukimwi, magonjwa mbalimbali yenye kupunguza kinga ya mwili.

3. Kukosa usingizi stress, vidonda sehemu za siri,matumizi ya antibiotics, kuweka marashi sehemu za siri.

4. Watu wanaougua kisukari ambao hawawezi kudhibiti kwa kutumia dawa za kisukari, inakuwa kwenye damu na hicho kisukari ndiyo chakula kikuu cha hao fangasi.

Hata wanawake ambao wanapenda kula vyakula vya sukari nyingi k**a vile chocolates, soda, na vingine vyenye sukari nyingi ambavyo ni chakula cha fangasi.

5. Mazingira ya joto hii inamaanisha nguo ambazo tunatakiwa kuvaa k**a vile chupi za cotton hasa kwa wanawake, hazihitaji joto sababu bacteria wabaya wanakuwa wengi sana na kusababisha miwasho na FANGASI

6. Kondomu na mbegu za kiume huharibu hali ya asidi iliyopo ukeni ambayo ni ya muhimu sana maana inasaidia kukinga uke usiingiliwe na bacteria wabaya.

MADHARA MAKUBWA YA FANGASI

Kupatwa kwa ugonjwa wa Pelvic Inflammatory Disease (PID) maambukizi katika via za uzazi na kupelekea kuwa mgumba, ndio maana wanawake wengi ni wagumba, cancer kwenye shingo ya uzazi, mirija ya uzazi kuziba n.k

NAMNA YA KUJILINDA NA U.T.I NA FANGASI.

1. Tumia viini lishe na virutubisho i.e food supplements.

2. Kunywa maji mengi angalau glasi nane kwa siku.

3. Epuka matumizi ya pombe na kahawa.

4. Kunywa maji kabla ya kufanya mapenzi na kojoa baada ya kufanya mapenzi.

5. Jitawaze kuanzia mbele kwenda nyuma. (Front to Back)

6. Kata makucha marefu kwa sababu unavyokwenda chooni kujitawaza huwa baadhi ya uchafu unabaki kwenye makucha na ndio chanzo cha wanawake wengi kuwa na U.T.I inayojirudia mara kwa mara.

7. Tumia pads ukiwa kwenye period.

8. Ebuka kujipulizia pafyumu kwenye sehemu za siri.

9. Vaa nguo za ndani za pamba na epuka nguo zilizobana sana.

SULUHISHO LA WENGI.

Watu wengi wanapokuwa na U.T.I huenda kupewa antibiotics ambazo huenda kuua bakteria wazuri na matokeo yake baada ya muda U.T.I inarudi kwa kasi sana.

SULUHISHO LA KUDUMU.

•Tumia supplement/ Tiba lishe za asili ambazo hazina kemikali ndani yake.

•Unapaswa wewe mwanamke usijioshee kila siku badala ya kuweka marashi au sabuni za chemical, zaidi huuwa bacteria wazuri na kuwaacha wale wabaya. Na pia kutumia dawa bila ushauri kutoka kwa daktari ni hatari kwa afya yako pia kwan kuna wengine wanatumia dawa za kuweka ukeni na baada ya muda ujikuta uchafu unaanza kutoka na mwisho wa siku tatizo uwa kubwa na kupelekea PID.

HITIMISHO;

JE, UNA DALILI TAJWA HAPO JUU AU UNA TATIZO ILI LA FANGASI SUGU AU UTI?

K**a una tatizo hili au unamfahamu mtu mwenye tatizo na ameshindwa kulipatia ufumbuzi, wasiliana nasi kwa ushauri na msaada zaidi. Kwani tunavyo virutubisho/ supplement ambayo imekuwa msaada kwa wanawake wengi ambao walikuwa wamekataa tamaa kwa kutafuta ufumbuzi muda mrefu bila mafanikio.
0755325722

15/07/2021

Wanaume wengi wamekumbwa na changamoto hii, sasa hunabudi kuchukua hatua.

Fuatana na Mimi leo hiii hii yawezekana hii ikawa suluhisho lako hata ikawa ukombozi wa rafiki na jamaa zako.

*TATIZO LA AFYA YA UZAZI NA UTENDAJI WAKE & TATIZO KATIKA UZALISHAJI BORA KWA AFYA YA UZAZI KWA WAUME* 0755325722

*MBEGU ZA KIUME DHAIFU*

Mbegu za kiume dhaifu au chache, hizi Ni mbegu ambazo huwa nyepesi na mala nyingi huwa Zina maji mengi na haziwezi kutungisha Mimba.

VISABABISHI VYA MBEGU ZA KIUME KUWA DHAIFU AU CHACHE
👉Ulaji mbovu wa chakula ambavyo havina madini muhimu hasa ya Zink, Selenium, Vitamin E, Folic Acid, Vitamin B12, Vitamin C
👉Kuwepo kwa sumu Mwilini
👉Kujichua(punyeto)
👉Joto kali kupita kiasi
👉Mafadhaiko(Stress)
👉Unywaji wa pombe uliokithiri
👉Vinywaji vyenye sumu au kemikali na homones

DALILI ZA MBEGU ZA KIUME KUWA DHAIFU AU CHACHE
👉Mbegu kuwa nyepesi
👉Mbegu zikiingia ukeni hazikai, baada ya dakika chache mwanamke anaanza kuhisi mbegu kutokana kwa Njia ya kuchurizika K**a maji
👉Mwanamke hashiki mimba kwa haraka
👉Hazina uwezo wa kuogelea ukeni hufia njiani
👉Hutoka chache na nyepesi K**a maji
👉Huwa na rangi nyeupee

UTAZIJUAJE MBEGU ZA KIUME ZILIZO BORA
👉Hutoka nyingi
👉Huwa nzito na kuchelewa kuyeyuka
👉Hutungisha mimba kwa haraka zaidi
👉Zina uwezo wa kuogelea kwa haraka zaidi
👉Huwa na rangi ya gray K**a Maziwa

TAHADHARI
👉Jiepushe na ulaji wa vyakula vya wanga na sukari nyingi Mara kwa Mara
👉Punguza Matumizi ya soda
👉Acha unywaji wa pombe
👉Jiepushe mazoea ya ulaji wa keki na vyakula vya kwenye makopo
👉Jiepushe Kujichua au punyeto

MWANAMKE KUTOSHIKA MIMBA SIO TATIZO LA MWANAMKE, INAWEZEKANA MWANAUME MWENZANGU TATIZO LIPO KWAKO, KWA USHAURI ZAIDI NA TIBA KARIBU TUZUNGUMZE ZAIDI, 0755325722

07/07/2021
02/07/2021

Karibu upate suluhisho la tatizo lako. Usikae na maumivu ..pia unaweza utasababisha ulemavu wa kudumu.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Pretoria?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Pretoria